Noor
Kiswahili
Noor / Dua / Kumsifu Allah / Fadhila ya Subhanallah, Alhamdulillah, La ilaha illallah na Allahu Akbar

Fadhila ya Subhanallah, Alhamdulillah, La ilaha illallah na Allahu Akbar

Kumsifu Allah · 12 dua

Fadhila ya Subhanallah, Alhamdulillah, La ilaha illallah na Allahu Akbar 0:00
Sikiliza
1

قَالَ صلى الله عليه وسلم مَنْ قَالَ: سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ فِي يَوْمٍ مِائَةَ مَرَّةٍ حُطَّتْ خَطَايَاهُ وَلَوْ كَانَتْ مِثْلَ زَبَدِ الْبَحْر

Amesema Mtume (s.a.w): ''Mwenye kusema: ''Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema zote ni zake.'' Kwa siku mara mia, atafutiwa madhambi yake hata kama yalikuwa mfano wa povu la bahari.

Chanzo: Al-Bukhari 7/168, Muslim 4/2071.

2

وَقَالَ صلى الله عليه وسلم: مَنْ قَالَ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ, لَهُ الْمُلْكُ, وَلَهُ الْحَمْدُ, وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ عَشْرَ مِرَارٍ, كَانَ كَمَنْ أَعْتَقَ أَرْبَعَةَ أَنْفُسٍ مِنْ وَلَدِ إِسْمَاعِيلَ

Na Mtume (s.a.w) amesema: ''Atakaesema:'' ''Hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu hali ya kuwa peke yake, hana mshirika, ni wake Ufalme, na ni zake kila sifa njema, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza.'' ......Mara kumi, ni kama (thawabu za mtu) aliyeacha huru nafsi nne katika wana wa Ismail.

Chanzo: Al-Bukhari 7/67, Muslim 4/2071.

3

وَقَالَ صلى الله عليه وسلم: كَلِمَتَانِ خَفِيفَتَانِ عَلَى اللِّسَانِ, ثَقِيلَتَانِ فِي الْمِيزَانِ, حَبِيبَتَانِ إِلَى الرَّحْمَنِ: سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ, سُبْحانَ اللَّهِ الْعَظِيمِ

Na amesema Mtume (s.a.w): Kuna maneno mawili ni mepesi mno juu ya ulimi, mazito mno katika mizani, yanapendeza mno mbele ya Rahmani (Mwenye kurehemu) nayo ni: ''Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni zake, ametakasika Mwenyezi Mungu aliye Mtukufu.''

Chanzo: Al-Bukhari 7/168, Muslim 4/2072.

4

وَقَالَ صلى الله عليه وسلم: لَأَنْ أَقُولَ سُبْحَانَ اللَّهِ, وَالْحَمْدُ لِلَّهِ, وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ, وَاللَّهُ أَكْبَرُ, أَحَبُّ إِلَيَّ مِمَّا طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمسُ

Na amesema Mtume (s.a.w): ''Kusema kwangu: ''Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa.'' .....Ni bora kwangu kuliko kila kilicho angaziwa na jua.

Chanzo: Muslim 4/2072.

5

وَقَالَ صلى الله عليه وسلم: (أَيَعْجِزُ أَحَدُكُم أَنْ يَكْسِبَ كُلَّ يَوْمٍ أَلْفَ حَسَنَةٍ) فَسَأَلَهُ سَائِلٌ مِنْ جُلَسَائِهِ كَيْفَ يَكْسِبُ أَحَدُنَا أَلْفَ حَسَنَةٍ؟ قَالَ: (يُسَبِّحُ مِائَةَ تَسْبِيحَةٍ, فَيُكتَبُ لَهُ أَلْفُ حَسَنَةٍ أَوْ يُحَطُّ عَنْهُ أَلْفُ خَطِيئَةٍ)

Na amesema Mtume (s.a.w): ''Hivi anashindwa mmoja wenu kuchuma kila siku thawabu elfu? Mtu mmoja miongoni mwa waliokaa akamuuliza: Atachuma vipi mmoja wetu thawabu elfu? (Mtume s.a.w) Akamjibu: Aseme: (Subhana LLah). ''Ametakasika Mwenyezi Mungu.'' ...Mara mia moja, basi ataandikiwa thawabu elfu moja, au atafutiwa madhambi elfu moja.

Chanzo: Muslim 4/2073.

6

مَنْ قَالَ: سُبْحَانَ اللَّهِ الْعَظِيمِ وَبِحَمْدِهِ غُرِسَتْ لَهُ نَخْلَةٌ فِي الْجَنَّةِ

Na amesema Mtume (s.a.w): ''Atakaesema: ''Ametakasika Mwenyezi Mungu aliye Mtukufu, na sifa njema zote ni zake.'' ....Hupandiwa mtende peponi.

Chanzo: At-Tirmizi 5/511, and Al-Hakim.

7

وَقَالَ صلى الله عليه وسلم: (يَا عَبْدَ اللَّهِ بْنَ قَيْسٍ أَلاَ أَدُلُّكَ عَلَى كَنْزٍ مِنْ كُنُوزِ الْجَنَّةِ)؟ فَقُلْتُ: بَلَى يَا رَسُولَ اللَّهِ, قَالَ: (قُلْ لاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللَّهِ)

Na amesema Mtume (s.a.w): ''Ewe Abdallah bin Qais, hivi nikufahamishe (nikuonyeshe) hazina miongoni mwa hazina za pepo? Nikamwambia: Ndio Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, akaniambia, Sema: ''Hakuna uwezo wala nguvu ila za Mwenyezi Mungu,'' (ila kwa kuwezeshwa na Mwenyezi Mungu).

Chanzo: Al-Bukhari, Muslim 4/2076.

8

وَقَالَ صلى الله عليه وسلم: أَحَبُّ الْكَلاَمِ إِلَى اللَّهِ أَرْبَعٌ: سُبْحَانَ اللَّهِ, وَالْحَمْدُ لِلَّهِ, وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ, وَاللَّهُ أَكْبَرُ, لاَ يَضُرُّكَ بِأَيِّهِنَّ بَدَأتَ

Na akasema Mtume (s.a.w): ''Bora ya maneno kwa Mwenyezi Mungu ni manne'': ''Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa.'' ....Si vibaya kuanza kwa lolote katika hayo.

Chanzo: Muslim 3/1685.

9

جَاءَ أَعْرَابِيٌّ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: عَلِّمْنِي كَلاماً أَقُولُهُ: قَالَ: (قُلْ: لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ, اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيراً, وَالْحَمْدُ لِلَّهِ كَثِيراً, سُبْحَانَ اللَّهِ رَبِّ العَالَمِينَ, لاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ) قَالَ: فَهَؤُلاَءِ لِرَبِّي, فَمَا لِي؟ قَالَ: (قُلْ: اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي, وَارْحَمْنِي, وَاهْدِنِي, وَارْزُقْنِي)

Alikuja mtu mmoja wa shamba kwa Mtume (s.a.w) akamwambia, nifundishe maneno nitakayo yasema, Mtume (s.a.w) akamwambia: Sema: ''Hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu hali ya kuwa peke yake, wala hana mshirika wake, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa tena sana, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu tena nyingi sana, Ametakasika Mwenyezi Mungu Mwenye Kutukuka, Mwingi wa Hekima.'' ......Yule mtu kisha akasema, Haya ni ya Mwenyezi Mungu, ni yapi yangu? Mtume (s.a.w) akamwambia, Sema: ''Ewe Mwenyezi Mungu, nisamehe, na unirehemu, na uniongoze, na uniruzuku.''

Chanzo: Muslim 4/2072.

10

كَانَ الرَّجُلُ إِذَا أَسْلَمَ عَلَّمَهُ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم الصَّلاَةَ ثُمَّ أَمَرَهُ أَنْ يَدْعُوَ بِهَؤُلاَءِ الْكَلِمَاتِ: اللَّهُمَّ اغْفِرِ لِي, وَارْحَمْنِي, وَاهْدِنِي, وَعَافِنِي وَارْزُقْنِي

Aliku mtu akisilimu, Mtume (s.a.w) anamfundisha kuswali kisha anamuamrisha kuomba kwa matamshi haya: ''Ewe Mwenyezi Mungu, nisamehe, na unirehemu, na uniongoze, na unipe afya njema, na uniruzuku.''

Chanzo: Muslim 4/2073.

11

إِنَّ أَفْضَلَ الدُّعَاءِ الْحَمْدُ لِلَّهِ, وَأَفْضَلَ الذِّكْرِ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ

Bora ya dua ni mtu kusema: (Alhamdu liLLahi). ''Kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu.'' Na bora ya utajo (uradi) ni mtu kusema: (Laa ilaha ila LLah). ''Hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu.''

Chanzo: At-Tirmizi\n 5/462, Ibn Majah 2/1249, and Al-Hakim.

12

الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ: سُبْحَانَ اللَّهِ, وَالْحَمْدُ لِلَّهِ, وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ, وَاللَّهُ أَكْبَرُ, وَلاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللَّهِ

Mema yasioisha ni: ''Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, na hakuna uwezo wala nguvu ila za Mwenyezi Mungu, (ila kwa kuwezeshwa na Mwenyezi Mungu).''

Chanzo: Ahmad (Hadith no. 513).