1
أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيطَانِ الرَّجِيمِ, وَاتْفُلْ عَلَى يَسَارِكَ ( ثلاثاً)
Najilinda kwa Mwenyezi Mungu, kutokana na shetani aliyelaaniwa. ...kisha utatema vijimate vichache, upande wa kushoto mara tatu. Imepokewa kutoka kwa Uthman Ibn Al-Ass (r.a) amesema: 'Nilimwambia Mtume (s.a.w): Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu hakika shetani amenikalia kati yangu na kati ya swala yangu na kisomo changu, ananitatiza. Mtume (s.a.w) akasema: Huyo ni shetani aitwae ''Khanzab'' ukimuhisi amekuijia, basi muombe hifadhi Mwenyezi Mungu, na tema vijimate vichache, kushotoni mwako mara tatu. ....nikafanya hivo, Mwenyezi Mungu akaniondoshea.
Chanzo: Muslim 4/1729.