Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Ma'arij
70

Al-Ma'arij — Ngazi za Kupandia

المَعَارِجِ
Za Makka Aya 44
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍۢ وَاقِعٍۢ

Sa ala saaa'ilum bi'azaa binw-waaqi'

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,

Aya 2

لِّلْكَٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌۭ

Lilkaafireen laisa lahoo daafi'

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -

Aya 3

مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ

Minal laahi zil ma'aarij

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

Aya 4

تَعْرُجُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍۢ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍۢ

Ta'rujul malaaa'ikatu war Roohu ilaihi fee yawmin kaana miqdaaruhoo khamseena alfa sanah

Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!

Aya 5

فَٱصْبِرْ صَبْرًۭا جَمِيلًا

Fasbir ssabran jameelaa

Basi subiri kwa subira njema.

Aya 6

إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًۭا

Inaahum yarawnahoo ba'eedaa

Hakika wao wanaiona iko mbali,

Aya 7

وَنَرَىٰهُ قَرِيبًۭا

Wa naraahu qareebaa

Na Sisi tunaiona iko karibu.

Aya 8

يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ

Yawma takoonus samaaa'u kalmuhl

Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.

Aya 9

وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ

Wa takoonul jibaalu kal'ihn

Na milima itakuwa kama sufi.

Aya 10

وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًۭا

Wa laa yas'alu hameemun hameemaa

Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

Aya 11

يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ

Yubassaroonahum; ya waddul mujrimu law yaftadee min 'azaabi yawma'izim bibaneeh

Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,

Aya 12

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

Wa saahibatihee wa akheeh

Na mkewe, na nduguye,

Aya 13

وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ

Wa faseelathil latee tu'weeh

Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,

Aya 14

وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًۭا ثُمَّ يُنجِيهِ

Wa man fil ardi jamee'an summa yunjeeh

Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

Aya 15

كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

Kallaa innahaa lazaa

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

Aya 16

نَزَّاعَةًۭ لِّلشَّوَىٰ

Nazzaa'atal lishshawaa

Unao babua ngozi ya kichwa!

Aya 17

تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Tad'oo man adbara wa tawallaa

Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.

Aya 18

وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ

W jama'a fa aw'aa

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

Aya 19

۞ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

Innal insaana khuliqa haloo'aa

Hakika mtu ameumbwa na papara.

Aya 20

إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًۭا

Izaa massahush sharru jazoo'aa

Inapo mgusa shari hupapatika.

Aya 21

وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا

Wa izaa massahul khairu manoo'aa

Na inapo mgusa kheri huizuilia.

Aya 22

إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ

Illal musalleen

Isipo kuwa wanao sali,

Aya 23

ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ

Allazeena hum 'alaa Salaatihim daaa'imoon

Ambao wanadumisha Sala zao,

Aya 24

وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّۭ مَّعْلُومٌۭ

Wallazeena feee amwaalihim haqqum ma'loom

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

Aya 25

لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ

Lissaaa 'ili walmahroom

Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;

Aya 26

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

Wallazeena yusaddiqoona bi yawmid Deen

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

Aya 27

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ

Wallazeena hum min 'azaabi Rabbihim mushfiqoon

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

Aya 28

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍۢ

Inna 'azaaba Rabbihim ghairu maamoon

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.

Aya 29

وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَٰفِظُونَ

Wallazeena hum lifuroo jihim haafizoon

Na ambao wanahifadhi tupu zao.

Aya 30

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ

Illaa 'alaaa azwaajihim aw maa malakat aymaanuhum fainnahum ghairu maloomeen

Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -

Aya 31

فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ

Famanib taghaa waraaa'a zaalika fa ulaaa'ika humul 'aadoon

Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.

Aya 32

وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَٰنَٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ

Wallazeena hum li amaa naatihim wa 'ahdihim raa'oon

Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

Aya 33

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ

Wallazeena hum bishahaadaatihim qaaa'imoon

Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

Aya 34

وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ

Wallazeena hum 'alaa salaatihim yuhaafizoon

Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

Aya 35

أُو۟لَٰٓئِكَ فِى جَنَّٰتٍۢ مُّكْرَمُونَ

Ulaaa'ika fee jannaatim mukramoon

Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.

Aya 36

فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ

Famaa lil lazeena kafaroo qibalaka muhti'een

Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?

Aya 37

عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ

'Anil yameeni wa 'anish shimaali 'izeen

Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

Aya 38

أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍۢ

Ayatma'u kullum ri'im minhum anyyudkhala jannata Na'eem

Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?

Aya 39

كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ

Kallaaa innaa khalaq nahum mimmaa ya'lamoon

La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.

Aya 40

فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَٰرِقِ وَٱلْمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ

Falaaa uqsimu bi Rabbil mashaariqi wal maghaaribi innaa laqaadiroon

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza

Aya 41

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًۭا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ

'Alaaa an nubaddila khairam minhum wa maa Nahnu bimasbooqeen

Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

Aya 42

فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ

Fazarhum yakhoodoo wa yal'aboo hattaa yulaaqoo yaw mahumul lazee yoo'adoon

Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,

Aya 43

يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًۭا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍۢ يُوفِضُونَ

Yawma yakhrujoona minal ajdaasi siraa'an ka anna hum ilaa nusubiny yoofidoon

Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,

Aya 44

خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌۭ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ

Khaashi'atan absaaruhum tarhaquhum zillah; zaalikal yawmul lazee kaanoo yoo'adoon

Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.