Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Qalam
68

Al-Qalam — Kalamu

القَلَمِ
Za Makka Aya 52
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

نٓ ۚ وَٱلْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ

Noon; walqalami wa maa yasturoon

Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,

Aya 2

مَآ أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍۢ

Maa anta bini'mati Rabbika bimajnoon

Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

Aya 3

وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍۢ

Wa inna laka la ajran ghaira mamnoon

Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.

Aya 4

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍۢ

Wa innaka la'alaa khuluqin 'azeem

Na hakika wewe una tabia tukufu.

Aya 5

فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ

Fasatubsiru wa yubsiroon

Karibu utaona, na wao wataona,

Aya 6

بِأَييِّكُمُ ٱلْمَفْتُونُ

Bi ayyikumul maftoon

Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.

Aya 7

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِٱلْمُهْتَدِينَ

Innaa Rabbaka Huwa a'lamu biman dalla 'an sabeelihee wa Huwa a'lamu bilmuhtadeen

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.

Aya 8

فَلَا تُطِعِ ٱلْمُكَذِّبِينَ

Falaa tuti'il mukazzibeen

Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.

Aya 9

وَدُّوا۟ لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ

Waddoo law tudhinu fa-yudhinoon

Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.

Aya 10

وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍۢ مَّهِينٍ

Wa laa tuti' kulla hallaa fim maheen

Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,

Aya 11

هَمَّازٍۢ مَّشَّآءٍۭ بِنَمِيمٍۢ

Hammaazim mash shaaa'im binameem

Mtapitapi, apitaye akifitini,

Aya 12

مَّنَّاعٍۢ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ

Mannaa'il lilkhairi mu'tadin aseem

Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,

Aya 13

عُتُلٍّۭ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

'Utullim ba'da zaalika zaneem

Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.

Aya 14

أَن كَانَ ذَا مَالٍۢ وَبَنِينَ

An kaana zaa maalinw-wa baneen

Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

Aya 15

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ

Izaa tutlaa 'alaihi aayaatunaa qaala asaateerul awwaleen

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!

Aya 16

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلْخُرْطُومِ

Sanasimuhoo 'alal khurtoom

Tutamtia kovu juu ya pua yake.

Aya 17

إِنَّا بَلَوْنَٰهُمْ كَمَا بَلَوْنَآ أَصْحَٰبَ ٱلْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا۟ لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ

Innaa balawnaahum kamaa balawnaaa As-haabal jannati iz 'aqsamoo la-yasri munnahaa musbiheen

Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.

Aya 18

وَلَا يَسْتَثْنُونَ

Wa laa yastasnoon

Wala hawakusema: Mungu akipenda!

Aya 19

فَطَافَ عَلَيْهَا طَآئِفٌۭ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَآئِمُونَ

Fataafa 'alaihaa taaa'i fum mir rabbika wa hum naaa'imoon

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

Aya 20

فَأَصْبَحَتْ كَٱلصَّرِيمِ

Fa asbahat kassareem

Likawa kama usiku wa giza.

Aya 21

فَتَنَادَوْا۟ مُصْبِحِينَ

Fatanaadaw musbiheen

Asubuhi wakaitana.

Aya 22

أَنِ ٱغْدُوا۟ عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَٰرِمِينَ

Anighdoo 'alaa harsikum in kuntum saarimeen

Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

Aya 23

فَٱنطَلَقُوا۟ وَهُمْ يَتَخَٰفَتُونَ

Fantalaqoo wa hum yatakhaafatoon

Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,

Aya 24

أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا ٱلْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌۭ

Al laa yadkhulannahal yawma 'alaikum miskeen

Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.

Aya 25

وَغَدَوْا۟ عَلَىٰ حَرْدٍۢ قَٰدِرِينَ

Wa ghadaw 'alaa hardin qaadireen

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Aya 26

فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوٓا۟ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Falammaa ra awhaa qaalooo innaa ladaaalloon

Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!

Aya 27

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ

Bal nahnu mahroomoon

Bali tumenyimwa!

Aya 28

قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ

Qaala awsatuhum alam aqul lakum law laa tusabbihoon

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

Aya 29

قَالُوا۟ سُبْحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Qaaloo subhaana rabbinaaa innaa kunnaa zaalimeen

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

Aya 30

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَلَٰوَمُونَ

Fa aqbala ba'duhum 'alaa ba'diny yatalaawamoon

Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

Aya 31

قَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ

Qaaloo yaa wailanaaa innaa kunnaa taagheen

Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Aya 32

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًۭا مِّنْهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

'Asaa rabbunaaa any yubdilanaa khairam minhaaa innaaa ilaa rabbinaa raaghiboon

Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Aya 33

كَذَٰلِكَ ٱلْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ ٱلْءَاخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا۟ يَعْلَمُونَ

Kazaalikal azaab, wa la'azaabul aakhirati akbar; law kaanoo ya'lamoon

Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!

Aya 34

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Inna lilmuttaqeena 'inda rabbihim jannaatin na'eem

Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

Aya 35

أَفَنَجْعَلُ ٱلْمُسْلِمِينَ كَٱلْمُجْرِمِينَ

Afanaj'alul muslimeena kalmujrimeen

Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

Aya 36

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ

Maa lakum kaifa tahhkumoon

Mna nini? Mnahukumu vipi?

Aya 37

أَمْ لَكُمْ كِتَٰبٌۭ فِيهِ تَدْرُسُونَ

Am lakum kitaabun feehi tadrusoon

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

Aya 38

إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ

Inna lakum feehi lamaa takhaiyaroon

Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?

Aya 39

أَمْ لَكُمْ أَيْمَٰنٌ عَلَيْنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ

Am lakum aymaanun 'alainaa baalighatun ilaa yawmil qiyaamati inna lakum lamaa tahkumoon

Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?

Aya 40

سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ

Salhum ayyuhum bizaa lika za'eem

Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?

Aya 41

أَمْ لَهُمْ شُرَكَآءُ فَلْيَأْتُوا۟ بِشُرَكَآئِهِمْ إِن كَانُوا۟ صَٰدِقِينَ

Am lahum shurakaaa'u falyaatoo bishurakaaa 'ihim in kaanoo saadiqeen

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

Aya 42

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍۢ وَيُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ

Yawma yukshafu 'am saaqinw wa yud'awna ilas sujoodi falaa yastatee'oon

Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,

Aya 43

خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌۭ ۖ وَقَدْ كَانُوا۟ يُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمْ سَٰلِمُونَ

Khaashi'atan absaaruhum tarhaquhum zillatunw wa qad kaanoo yud'awna ilassujoodi wa hum saalimoon

Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -

Aya 44

فَذَرْنِى وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ

Fazarnee wa many yukazzibu bihaazal hadeesi sanastad rijuhum min haisu laa ya'lamoon

Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.

Aya 45

وَأُمْلِى لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِى مَتِينٌ

Wa umlee lahum; inna kaidee mateen

Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

Aya 46

أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًۭا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍۢ مُّثْقَلُونَ

Am tas'aluhum ajran fahum mim maghramim musqaloon

Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

Aya 47

أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ

Am 'indahumul ghaibu fahum yaktuboon

Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

Aya 48

فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌۭ

Fasbir lihkmi rabbika wa laa takun kasaahibil boot; iz naadaa wa huwa makzoom

Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.

Aya 49

لَّوْلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعْمَةٌۭ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ مَذْمُومٌۭ

Law laaa an tadaara kahoo ni'matum mir rabbihee lanubiza bil'araaa'i wa huwa mazmoom

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Aya 50

فَٱجْتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Fajtabaahu rabbuhoo faja'alahoo minas saaliheen

Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Aya 51

وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَٰرِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا۟ ٱلذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجْنُونٌۭ

Wa iny-yakaadul lazeena kafaroo la-yuzliqoonaka biabsaarihim lammaa saml'uz-Zikra wa yaqooloona innahoo lamajnoon

Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Aya 52

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ

Wa maa huwa illaa zikrul lil'aalameen

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.