Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Ash-Shu'araa
26

Ash-Shu'araa — Washairi

الشُّعَرَاءِ
Za Makka Aya 227
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

طسٓمٓ

Taa-Seeen-Meeem

T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)

Aya 2

تِلْكَ ءَايَٰتُ ٱلْكِتَٰبِ ٱلْمُبِينِ

Tilka Aayaatul Kitaabil Mubeen

Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

Aya 3

لَعَلَّكَ بَٰخِعٌۭ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ

La'allaka baakhi'un nafsaka allaa yakoonoo mu'mineen

Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

Aya 4

إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةًۭ فَظَلَّتْ أَعْنَٰقُهُمْ لَهَا خَٰضِعِينَ

In nashaa nunazzil 'alaihim minas samaaa'i Aayatan fazallat a'naaquhum lahaa khaadi'een

Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.

Aya 5

وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍۢ مِّنَ ٱلرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ

Wa maa yaateehim min zikrim minar Rahmaani muhdasin illaa kaanoo 'anhu mu'rideen

Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.

Aya 6

فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ

Faqad kazzaboo fasa yaateehim ambaaa'u maa kaanoo bihee yastahzi'oon

Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.

Aya 7

أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍۢ كَرِيمٍ

Awa lam yaraw ilal ardi kam ambatnaa feehaa min kulli zawjin kareem

Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

Aya 8

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Inn fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Aya 9

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 10

وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّٰلِمِينَ

Wa iz naadaa Rabbuka Moosaaa ani'-til qawmaz zaalimeen

Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,

Aya 11

قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ

Qawma Fir'awn; alaa yattaqoon

Watu wa Firauni. Hawaogopi?

Aya 12

قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ

Qaala Rabbi inneee akhaafu ai yukazziboon

Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.

Aya 13

وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَٰرُونَ

Wa yadeequ sadree wa laa yantaliqu lisaanee fa arsil ilaa Haaroon

Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

Aya 14

وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌۭ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ

Wa lahum 'alaiya zambun fa akhaafu ai yaqtuloon

Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.

Aya 15

قَالَ كَلَّا ۖ فَٱذْهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآ ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ

Qaala kallaa fazhabaa bi Aayaatinaaa innaa ma'akum mustami'oon

Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

Aya 16

فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Faatiyaa Fir'awna faqoolaaa innaa Rasoolu Rabbil 'aalameen

Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 17

أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

An arsil ma'anaa Baneee Israaa'eel

Waachilie Wana wa Israili wende nasi.

Aya 18

قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًۭا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ

Qaala alam nurabbika feenaa waleedanw wa labista feenaa min 'umurika sineen

(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?

Aya 19

وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَٰفِرِينَ

Wa fa'alta fa'latakal latee fa'alta wa anta minal kaafireen

Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?

Aya 20

قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًۭا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Qaala fa'altuhaaa izanw wa ana minad daaaleen

(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.

Aya 21

فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًۭا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ

Fafarartu minkum lam maa khiftukum fawahaba lee Rabbee hukmanw wa ja'alanee minal mursaleen

Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

Aya 22

وَتِلْكَ نِعْمَةٌۭ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

Wa tilka ni'matun tamun nuhaa 'alaiya an 'abbatta Baneee Israaa'eel

Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

Aya 23

قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Qaala Fir'awnu wa maa Rabbul 'aalameen

Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Aya 24

قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Qaala Rabbus samaawaati wal ardi wa maa bainahumaa in kuntum mooqineen

Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

Aya 25

قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ

Qaala liman hawlahooo alaa tastami'oon

(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?

Aya 26

قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ

Qaala Rabbukum wa Rabbu aabaaa'ikumul awwaleen

(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

Aya 27

قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌۭ

Qaala inna Rasoolakumul lazee ursila ilaikum lamajnoon

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.

Aya 28

قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ

Qaala Rabbul mashriqi wal maghribi wa maa baina humaa in kuntum ta'qiloon

(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

Aya 29

قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ

Qaala la'init takhazta ilaahan ghairee la aj'alannaka minal masjooneen

(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

Aya 30

قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍۢ مُّبِينٍۢ

Qaala awalw ji'tuka bishai'im mubeen

Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

Aya 31

قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Qaala faati biheee in kunta minas saadiqeen

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.

Aya 32

فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌۭ مُّبِينٌۭ

Fa alqaa 'asaahu fa izaaa hiya su'baanum mubeen

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.

Aya 33

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ

Wa naza'a yadahoo faizaa hiya baidaaa'u linnaa zireen

Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.

Aya 34

قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٌۭ

Qaala lilmala-i hawlahooo inna haazaa lasaahirun 'aleem

(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

Aya 35

يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ

Yureedu ai yukhrijakum min ardikum bisihrihee famaazaa taamuroon

Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

Aya 36

قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Qaalooo arjih wa akhaahu wab'as filmadaaa'ini haashireen

Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.

Aya 37

يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍۢ

Yaatooka bikulli sah haarin 'aleem

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

Aya 38

فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوْمٍۢ مَّعْلُومٍۢ

Fa jumi'as saharatu limeeqaati Yawmim ma'loom

Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.

Aya 39

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ

Wa qeela linnaasi hal antum mujtami'oon

Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?

Aya 40

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَٰلِبِينَ

La'allanaa nattabi'us saharata in kaanoo humul ghaalibeen

Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.

Aya 41

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَٰلِبِينَ

Falammaa jaaa'as saharatu qaaloo li Fir'awna a'inna lanaa la ajjran in kunnaa nahnul ghaalibeen

Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?

Aya 42

قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًۭا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ

Qaala na'am wa innakum izal laminal muqarrabeen

Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

Aya 43

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ

Qaala lahum Moosaaa alqoo maaa antum mulqoon

Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.

Aya 44

فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَٰلِبُونَ

Fa alqaw hibaalahum wa 'isiyyahum wa qaaloo bi'izzati Fir'awna innaa lanahnul ghaaliboon

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

Aya 45

فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ

Fa alqaa Moosaa 'asaahu fa izaa hiya talqafu maa yaafikoon

Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.

Aya 46

فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Fa ulqiyas saharatu saajideen

Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.

Aya 47

قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Qaalooo aamannaa bi Rabbil 'aalameen

Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 48

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Rabbi Moosaa wa Haaroon

Mola Mlezi wa Musa na Harun.

Aya 49

قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَٰفٍۢ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ

Qaala aamantum lahoo qabla an aazana lakum innahoo lakabeerukumul lazee 'alla makumus sihra falasawfa ta'lamoon; la uqatti'anna aidiyakum wa arjulakum min khilaafinw wa la usallibanna kum ajma'een

(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.

Aya 50

قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

Qaaloo la daira innaaa ilaa Rabbinaa munqalliboon

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Aya 51

إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Innaa natma'u ai yaghfira lanaa Rabbunna khataa yaanaaa an kunnaaa awwalal mu'mineen

Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.

Aya 52

۞ وَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِىٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Wa awhainaaa ilaa Moosaaa an asri bi'ibaadeee innakum muttaba'oon

Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

Aya 53

فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Fa arsala Fir'awnu filmadaaa'ini haashireen

Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.

Aya 54

إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرْذِمَةٌۭ قَلِيلُونَ

Inna haaa'ulaaa'i lashir zimatun qaleeloon

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

Aya 55

وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَآئِظُونَ

Wa innahum lanaa laghaaa'izoon

Nao wanatuudhi.

Aya 56

وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

Wa innaa lajamee'un haaziroon

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.

Aya 57

فَأَخْرَجْنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍۢ

Fa akhrajnaahum min Jannaatinw wa 'uyoon

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,

Aya 58

وَكُنُوزٍۢ وَمَقَامٍۢ كَرِيمٍۢ

Wa kunoozinw wa ma qaamin kareem

Na makhazina, na vyeo vya hishima,

Aya 59

كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَٰهَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

Kazaalika wa awrasnaahaa Baneee Israaa'eel

Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

Aya 60

فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ

Fa atba'oohum mushriqeen

Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.

Aya 61

فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ

Falammaa taraaa'al jam'aani qaala as haabu Moosaaa innaa lamudrakoon

Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!

Aya 62

قَالَ كَلَّآ ۖ إِنَّ مَعِىَ رَبِّى سَيَهْدِينِ

Qaala kallaaa inna ma'iya Rabbee sa yahdeen

(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

Aya 63

فَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضْرِب بِّعَصَاكَ ٱلْبَحْرَ ۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍۢ كَٱلطَّوْدِ ٱلْعَظِيمِ

Fa awhainaaa ilaa Moosaaa anidrib bi'asaakal bahra fanfalaqa fakaana kullu firqin kattawdil 'azeem

Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

Aya 64

وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ ٱلْءَاخَرِينَ

Wa azlafnaa sammal aakhareen

Na tukawajongeza hapo wale wengine.

Aya 65

وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجْمَعِينَ

Wa anjainaa Moosaa wa mam ma'ahooo ajma'een

Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.

Aya 66

ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْءَاخَرِينَ

Summa aghraqnal aakhareen

Kisha tukawazamisha hao wengine.

Aya 67

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Inna fee zaalika la Aayaah; wa maa kaana aksaru hu mu'mineen

Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.

Aya 68

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 69

وَٱتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَٰهِيمَ

Watlu 'alaihim naba-a Ibraaheem

Na wasomee khabari za Ibrahim.

Aya 70

إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَا تَعْبُدُونَ

Iz qaala li abeehi wa qawmihee maa ta'budoon

Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

Aya 71

قَالُوا۟ نَعْبُدُ أَصْنَامًۭا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ

Qaaloo na'budu asnaaman fanazallu lahaa 'aakifeen

Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

Aya 72

قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ

Qaala hal yasma'oona kum iz tad'oon

Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?

Aya 73

أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ

Aw yanfa'oonakum aw yadurroon

Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?

Aya 74

قَالُوا۟ بَلْ وَجَدْنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ

Qaaloo bal wajadnaaa aabaaa 'anaa kazaalika yaf'aloon

Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

Aya 75

قَالَ أَفَرَءَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ

Qaala afara 'aitum maa kuntum ta'budoon

Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-

Aya 76

أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلْأَقْدَمُونَ

Antum wa aabaaa'ukumul aqdamoon

Nyinyi na baba zenu wa zamani?

Aya 77

فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّۭ لِّىٓ إِلَّا رَبَّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Fa innahum 'aduwwwul leee illaa Rabbal 'aalameen

Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 78

ٱلَّذِى خَلَقَنِى فَهُوَ يَهْدِينِ

Allazee khalaqanee fa Huwa yahdeen

Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,

Aya 79

وَٱلَّذِى هُوَ يُطْعِمُنِى وَيَسْقِينِ

Wallazee Huwa yut'imunee wa yasqeen

Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

Aya 80

وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ

Wa izaa mardtu fahuwa yashfeen

Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.

Aya 81

وَٱلَّذِى يُمِيتُنِى ثُمَّ يُحْيِينِ

Wallazee yumeetunee summa yuhyeen

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

Aya 82

وَٱلَّذِىٓ أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِى خَطِيٓـَٔتِى يَوْمَ ٱلدِّينِ

Wallazeee atma'u ai yaghfira lee khateee' atee Yawmad Deen

Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

Aya 83

رَبِّ هَبْ لِى حُكْمًۭا وَأَلْحِقْنِى بِٱلصَّٰلِحِينَ

Rabbi hab lee hukmanw wa alhiqnee bis saaliheen

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.

Aya 84

وَٱجْعَل لِّى لِسَانَ صِدْقٍۢ فِى ٱلْءَاخِرِينَ

Waj'al lee lisaana sidqin fil aakhireen

Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.

Aya 85

وَٱجْعَلْنِى مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

Waj'alnee minw warasati Jannnatin Na'eem

Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

Aya 86

وَٱغْفِرْ لِأَبِىٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Waghfir li abeee innahoo kaana mind daalleen

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

Aya 87

وَلَا تُخْزِنِى يَوْمَ يُبْعَثُونَ

Wa laa tukhzinee Yawma yub'asoon

Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.

Aya 88

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌۭ وَلَا بَنُونَ

Yawma laa yanfa'u maalunw wa laa banoon

Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.

Aya 89

إِلَّا مَنْ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلْبٍۢ سَلِيمٍۢ

Illaa man atal laaha biqalbin saleem

Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.

Aya 90

وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ

Wa uzlifatil Jannatu lilmuttaqeen

Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.

Aya 91

وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ

Wa burrizatil Jaheemu lilghaaween

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

Aya 92

وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ

Wa qeela lahum aina maa kuntum ta'budoon

Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu

Aya 93

مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ

Min doonil laahi hal yansuroonakum aw yantasiroon

Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?

Aya 94

فَكُبْكِبُوا۟ فِيهَا هُمْ وَٱلْغَاوُۥنَ

Fakubkiboo feehaa hum walghaawoon

Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,

Aya 95

وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ

Wa junoodu Ibleesa ajma'oon

Na majeshi ya Ibilisi yote.

Aya 96

قَالُوا۟ وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ

Qaaloo wa hum feehaa yakkhtasimoon

Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

Aya 97

تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِى ضَلَٰلٍۢ مُّبِينٍ

Tallaahi in kunnaa lafee dalaalim mubeen

Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,

Aya 98

إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Iz nusawweekum bi Rabbil 'aalameen

Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 99

وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلْمُجْرِمُونَ

Wa maaa adallanaaa illal mujrimoon

Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.

Aya 100

فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ

Famaa lanaa min shaa fi'een

Basi hatuna waombezi.

Aya 101

وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍۢ

Wa laa sadeeqin hameem

Wala rafiki wa dhati.

Aya 102

فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةًۭ فَنَكُونَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Falaw anna lanaa karratan fanakoona minal mu'mineen

Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.

Aya 103

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Inna fee zaalika la Aayatanw wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Aya 104

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 105

كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ ٱلْمُرْسَلِينَ

Kazzabat qawmu Noohinil Mursaleen

Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

Aya 106

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Iz qaala lahum akhoohum Noohun alaa tattaqoon

Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?

Aya 107

إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

Innee lakum Rasoolun ameen

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Aya 108

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqullaaha wa atee'oon

Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Aya 109

وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 110

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqul laaha wa atee'oon

Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Aya 111

۞ قَالُوٓا۟ أَنُؤْمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلْأَرْذَلُونَ

Qaalooo anu'minu laka wattaba 'akal arzaloon

Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?

Aya 112

قَالَ وَمَا عِلْمِى بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ

Qaala wa maa 'ilmee bimaa kaanoo ya'maloon

Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?

Aya 113

إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّى ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ

In hisaabuhum illaa 'alaa Rabbee law tash'uroon

Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!

Aya 114

وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Wa maaa ana bitaaridil mu'mineen

Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

Aya 115

إِنْ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٌۭ مُّبِينٌۭ

In ana illaa nazeerum mubeen

Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.

Aya 116

قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمَرْجُومِينَ

Qaaloo la'il lam tantahi yaa Noohu latakoonanna minal marjoomeen

Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

Aya 117

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِى كَذَّبُونِ

Qaala Rabbi inna qawmee kazzaboon

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.

Aya 118

فَٱفْتَحْ بَيْنِى وَبَيْنَهُمْ فَتْحًۭا وَنَجِّنِى وَمَن مَّعِىَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Faftab bainee wa bai nahum fat hanw wa najjinee wa mam ma'iya minal mu'mineen

Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

Aya 119

فَأَنجَيْنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ

Fa anjainaahu wa mamma'ahoo fil fulkil mashhoon

Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.

Aya 120

ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ ٱلْبَاقِينَ

Summa aghraqnaa ba'dul baaqeen

Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

Aya 121

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Inna fee zaalika la Aayaah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.

Aya 122

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 123

كَذَّبَتْ عَادٌ ٱلْمُرْسَلِينَ

Kazzabat 'Aadunil mursaleen

Kina A'd waliwakanusha Mitume.

Aya 124

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Iz qaala lahum akhoohum Hoodun alaa tattaqoon

Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?

Aya 125

إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

Innee lakum Rasoolun ameen

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Aya 126

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqullaaha wa atee'oon

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Aya 127

وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa maa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 128

أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةًۭ تَعْبَثُونَ

Atabnoona bikulli ree'in aayatan ta'basoon

Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

Aya 129

وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ

Wa tattakhizoona masaani'a la'allakum takhludoon

Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!

Aya 130

وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ

Wa izaa batashtum batashtum jabbaareen

Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.

Aya 131

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqul laaha wa atee'oon

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

Aya 132

وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِىٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ

Wattaqul lazeee amad dakum bimaa ta'lamoon

Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

Aya 133

أَمَدَّكُم بِأَنْعَٰمٍۢ وَبَنِينَ

Amaddakum bi an'aa minw wa baneen

Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.

Aya 134

وَجَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍ

Wa jannaatinw wa 'uyoon

Na mabustani na chemchem.

Aya 135

إِنِّىٓ أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍۢ

Innee akhaafu 'alaikum 'azaaba Yawmin 'azeem

Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.

Aya 136

قَالُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْنَآ أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ ٱلْوَٰعِظِينَ

Qaaloo sawaaa'un 'alainaaa awa 'azta am lam takum minal waa'izeen

Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

Aya 137

إِنْ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلْأَوَّلِينَ

In haazaaa illaa khuluqul awwaleen

Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

Aya 138

وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ

Wa maa nahnu bimu 'azzabeen

Wala sisi hatutaadhibiwa.

Aya 139

فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَٰهُمْ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Fakazzaboohu fa ahlaknaahum; inna fee zaalika la aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Aya 140

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 141

كَذَّبَتْ ثَمُودُ ٱلْمُرْسَلِينَ

Kazzabat Samoodul mursaleen

Kina Thamud waliwakanusha Mitume.

Aya 142

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Iz qaala lahum akhoohum Saalihun alaa tattaqoon

Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?

Aya 143

إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

Innee lakum Rasoolun ameen

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Aya 144

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqul laaha wa atee'oon

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

Aya 145

وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 146

أَتُتْرَكُونَ فِى مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ

Atutrakoona fee maa haahunnaaa aamineen

Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?

Aya 147

فِى جَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍۢ

Fee jannaatinw wa 'uyoon

Katika mabustani, na chemchem?

Aya 148

وَزُرُوعٍۢ وَنَخْلٍۢ طَلْعُهَا هَضِيمٌۭ

Wa zuroo inw wa nakhlin tal 'uhaa hadeem

Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.

Aya 149

وَتَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًۭا فَٰرِهِينَ

Wa tanhitoona minal jibaali buyootan faariheen

Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

Aya 150

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqul laaha wa atee'oon

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Aya 151

وَلَا تُطِيعُوٓا۟ أَمْرَ ٱلْمُسْرِفِينَ

Wa laa tutee'ooo amral musrifeen

Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,

Aya 152

ٱلَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ

Allazeena yufsidoona fil ardi wa laa yuslihoon

Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.

Aya 153

قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ

Qaalooo innamaa anta minal musahhareen

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.

Aya 154

مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌۭ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Maaa anta illaa basharum mislunaa faati bi Aayatin in kunta minas saadiqeen

Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Aya 155

قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٌۭ لَّهَا شِرْبٌۭ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍۢ مَّعْلُومٍۢ

Qaala haazihee naaqatul lahaa shirbunw w alakum shirbu yawmim ma'loom

Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

Aya 156

وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٍۢ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍۢ

Wa laa tamassoohaa bisooo'in fa yaakhuzakum 'azaabu Yawmin 'Azeem

Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.

Aya 157

فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا۟ نَٰدِمِينَ

Fa'aqaroohaa fa asbahoo naadimeen

Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.

Aya 158

فَأَخَذَهُمُ ٱلْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Fa akhazahumul 'azaab; inna fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum m'mineen

Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Aya 159

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 160

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلِينَ

kazzabat qawmu Lootinil mursaleen

Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.

Aya 161

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Iz qaala lahum akhoohum Lootun alaa tattaqoon

Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?

Aya 162

إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

Innee lakum rasoolun ameen

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.

Aya 163

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqul laaha wa atee'oon

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

Aya 164

وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 165

أَتَأْتُونَ ٱلذُّكْرَانَ مِنَ ٱلْعَٰلَمِينَ

Ataatoonaz zukraana minal 'aalameen

Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

Aya 166

وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَٰجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ

Wa tazaroona maa khalaqa lakum Rabbukum min azwaajikum; bal antum qawmun 'aadoon

Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!

Aya 167

قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمُخْرَجِينَ

Qaloo la'il lam tantahi yaa Lootu latakoonanna minal mukhrajeen

Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!

Aya 168

قَالَ إِنِّى لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلْقَالِينَ

Qaala innee li'amalikum minal qaaleen

Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.

Aya 169

رَبِّ نَجِّنِى وَأَهْلِى مِمَّا يَعْمَلُونَ

Rabbi najjjinee wa ahlee mimmmaa ya'maloon

Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

Aya 170

فَنَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ

Fanajjainaahu wa ahlahooo ajma'een

Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,

Aya 171

إِلَّا عَجُوزًۭا فِى ٱلْغَٰبِرِينَ

Illaa 'ajoozan filghaabireen

Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.

Aya 172

ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْءَاخَرِينَ

Summa dammarnal aa khareen

Kisha tukawaangamiza wale wengine.

Aya 173

وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًۭا ۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلْمُنذَرِينَ

Wa amtarnaa 'alaihim mataran fasaaa'a matarul munzareen

Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.

Aya 174

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Inna fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Aya 175

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Aya 176

كَذَّبَ أَصْحَٰبُ لْـَٔيْكَةِ ٱلْمُرْسَلِينَ

Kazzaba As haabul Aykatil mursaleen

Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

Aya 177

إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Iz qaala lahum Shu'aybun alaa tattaqoon

Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?

Aya 178

إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

Innee lakum Rasoolun ameen

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Aya 179

فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Fattaqul laaha wa atee'oon

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Aya 180

وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 181

۞ أَوْفُوا۟ ٱلْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا۟ مِنَ ٱلْمُخْسِرِينَ

Awful kaila wa laa takoonoo minal mukhsireen

Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.

Aya 182

وَزِنُوا۟ بِٱلْقِسْطَاسِ ٱلْمُسْتَقِيمِ

Wa zinoo bilqistaasil mustaqeem

Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;

Aya 183

وَلَا تَبْخَسُوا۟ ٱلنَّاسَ أَشْيَآءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا۟ فِى ٱلْأَرْضِ مُفْسِدِينَ

Wa laa tabkhasun naasa ashyaaa 'ahum wa laa ta'saw fil ardi mufsideen

Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.

Aya 184

وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِى خَلَقَكُمْ وَٱلْجِبِلَّةَ ٱلْأَوَّلِينَ

Wattaqul lazee khalaqakum waljibillatal awwaleen

Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.

Aya 185

قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ

Qaalooo innamaa anta minal musahhareen

Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.

Aya 186

وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌۭ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلْكَٰذِبِينَ

Wa maaa anta illaa basharum mislunaa wa innazunnuka laminal kaazibeen

Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

Aya 187

فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًۭا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Fa asqit 'alainaa kisafam minas samaaa'i in kunta minas saadiqeen

Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Aya 188

قَالَ رَبِّىٓ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ

Qaala Rabbeee a'lamu bimaa ta'maloon

Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.

Aya 189

فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ ٱلظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ

Fakazzaboohu fa akhazahum 'azaabu Yawmiz zullah; innahoo kaana 'azaaba Yawmin 'Azeem

Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

Aya 190

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

Inna fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Aya 191

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Wa inna Rabbaka la huwal 'Azeezur Raheem

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 192

وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa innahoo latanzeelu Rabbil 'aalameen

Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 193

نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلْأَمِينُ

Nazala bihir Roohul Ameen

Ameuteremsha Roho muaminifu,

Aya 194

عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُنذِرِينَ

'Alaa qalbika litakoona minal munzireen

Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,

Aya 195

بِلِسَانٍ عَرَبِىٍّۢ مُّبِينٍۢ

Bilisaanin 'Arabiyyim mubeen

Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.

Aya 196

وَإِنَّهُۥ لَفِى زُبُرِ ٱلْأَوَّلِينَ

Wa innahoo lafee Zuburil awwaleen

Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

Aya 197

أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ ءَايَةً أَن يَعْلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُا۟ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

Awalam yakul lahum Aayatan ai ya'lamahoo 'ulamaaa'u Baneee Israaa'eel

Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?

Aya 198

وَلَوْ نَزَّلْنَٰهُ عَلَىٰ بَعْضِ ٱلْأَعْجَمِينَ

Wa law nazzalnaahu 'alaa ba'dil a'jameen

Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,

Aya 199

فَقَرَأَهُۥ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا۟ بِهِۦ مُؤْمِنِينَ

Faqara ahoo 'alaihim maa kaanoo bihee mu'mineen

Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.

Aya 200

كَذَٰلِكَ سَلَكْنَٰهُ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ

Kazaalika salaknaahu fee quloobil mujrimeen

Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

Aya 201

لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُا۟ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ

Laa yu'minoona bihee hattaa yarawul 'azaabal aleem

Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

Aya 202

فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةًۭ وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ

Fayaatiyahum baghtatanw wa hum laa yash'uroon

Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.

Aya 203

فَيَقُولُوا۟ هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ

Fa yaqooloo hal nahnu munzaroon

Na watasema: Je, tutapewa muhula?

Aya 204

أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ

Aafabi 'azaabinaa yasta'jiloon

Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?

Aya 205

أَفَرَءَيْتَ إِن مَّتَّعْنَٰهُمْ سِنِينَ

Aara'aita im matta'naahum sineen

Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,

Aya 206

ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُوا۟ يُوعَدُونَ

Summa jaaa'ahum maa kaanoo yoo'adoon

Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,

Aya 207

مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يُمَتَّعُونَ

Maaa aghnaaa 'anhum maa kaanoo yumaatoo'oon

Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?

Aya 208

وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ

Wa maaa ahlaknaa min qaryatin illaa lahaa munziroon

Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -

Aya 209

ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Zikraa wa maa kunnaa zaalimeen

Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

Aya 210

وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ

Wa maa tanazzalat bihish Shayaateen

Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,

Aya 211

وَمَا يَنۢبَغِى لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ

Wa maa yambaghee lahum wa maa yastatee'oon

Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

Aya 212

إِنَّهُمْ عَنِ ٱلسَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ

Innahum 'anis sam'i lama'zooloon

Hakika hao wametengwa na kusikia.

Aya 213

فَلَا تَدْعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلْمُعَذَّبِينَ

Falaa tad'u ma'al laahi ilaahan aakhara fatakoona minal mu'azzabeen

Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.

Aya 214

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ ٱلْأَقْرَبِينَ

Wa anzir 'asheeratakal aqrabeen

Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

Aya 215

وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Wakhfid janaahaka limanit taba 'aka minal mu'mineen

Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.

Aya 216

فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّى بَرِىٓءٌۭ مِّمَّا تَعْمَلُونَ

Fa in asawka faqul innee bareee'um mimmmaa ta'maloon

Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.

Aya 217

وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

Wa tawakkal alal 'Azeezir Raheem

Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Aya 218

ٱلَّذِى يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ

Allazee yaraaka heena taqoom

Ambaye anakuona unapo simama,

Aya 219

وَتَقَلُّبَكَ فِى ٱلسَّٰجِدِينَ

Wa taqallubaka fis saajideen

Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.

Aya 220

إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ

Innahoo Huwas Samee'ul 'Aleem

Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.

Aya 221

هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ

Hal unabbi'ukum 'alaa man tanazzalush Shayaateen

Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?

Aya 222

تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍۢ

Tanazzalu 'alaa kulli affaakin aseem

Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

Aya 223

يُلْقُونَ ٱلسَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَٰذِبُونَ

Yulqoonas sam'a wa aksaruhum aaziboon

Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.

Aya 224

وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلْغَاوُۥنَ

Washshu 'araaa'u yattabi 'uhumul ghaawoon

Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.

Aya 225

أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِى كُلِّ وَادٍۢ يَهِيمُونَ

Alam tara annahum fee kulli waadiny yaheemoon

Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

Aya 226

وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ

Wa annahum yaqooloona ma laa yaf'aloon

Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?

Aya 227

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُوا۟ ٱللَّهَ كَثِيرًۭا وَٱنتَصَرُوا۟ مِنۢ بَعْدِ مَا ظُلِمُوا۟ ۗ وَسَيَعْلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓا۟ أَىَّ مُنقَلَبٍۢ يَنقَلِبُونَ

Illal lazeena aamanoo w a'amilus saalihaati wa zakarul laaha kaseeranw wantasaroo mim ba'di maa zulimoo; wa saya'lamul lazeena zalamooo aiya munqalbiny yanqaliboon

Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.