Noor
Kiswahili
Noor / Dua / Maradhi na Kifo / Dua kwa maiti katika swala ya jeneza

Dua kwa maiti katika swala ya jeneza

Maradhi na Kifo · 4 dua

Dua kwa maiti katika swala ya jeneza 0:00
Sikiliza
1

اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ وَارْحَمْهُ, وَعَافِهِ, وَاعْفُ عَنْهُ, وَأَكْرِمْ نُزُلَهُ, وَوَسِّعْ مُدْخَلَهُ, وَاغْسِلْهُ بِالْمَاءِ وَالثَّلْجِ وَالْبَرَدِ, وَنَقِّهِ مِنَ الْخَطَايَا كَمَا نَقَّيْتَ الثَّوْبَ الأَبْيَضَ مِنَ الدَّنَسِ, وَأَبْدِلْهُ دَاراً خَيْراً مِنْ دَارِهِ, وَأَهْلاً خَيْراً مِنْ أَهْلِهِ, وَزَوْجَاً خَيْراً مِنْ زَوْجِهِ, وَأَدْخِلْهُ الْجَنَّةَ, وَأَعِذْهُ مِنْ عَذَابِ القَبْرِ [وَعَذَابِ النَّارِ

Ewe Mwenyezi Mungu msamehe na umrehemu, na umuafu na msamehe, na mtukuze kushuka kwake (kaburini), na upanue kuingia kwake, na muoshe na maji, na kwa theluji, na barafu, na mtakase na makosa, kama unavyo takasa nguo nyeupe kutokana na uchafu, na mbadilishie nyumba bora kuliko nyumba yake, na jamaa bora kuliko jamaa zake, na mke bora kuliko mke wake, na muingize peponi, na mkinge na adhabu ya kaburi (na adhabu ya moto).

Chanzo: Muslim 2/663.

2

اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِحَيِّنَا وَمَيِّتِنَا, وَشَاهِدِنَا وَغَائِبِنَا, وَصَغِيرِنَا وَكَبيرِنَا, وَذَكَرِنَا وَأُنْثَانَا. اللَّهُمَّ مَنْ أَحْيَيْتَهُ مِنَّا فَأَحْيِهِ عَلَى الْإِسْلاَمِ, وَمَنْ تَوَفَّيْتَهُ مِنَّا فَتَوَفَّهُ عَلَى الإِيمَانِ, اللَّهُمَّ لاَ تَحْرِمْنَا أَجْرَهُ, وَلاَ تُضِلَّنَا بَعْدَهُ

Ewe Mwenyezi Mungu msamehe aliyehai katika sisi na aliyekufa, na aliyepo na asiyekuwepo, na mdogo katika yetu na mkubwa, na mwanamume kati yetu na mwanamke, Ewe Mwenyezi Mungu unayemuweka hai kati yetu basi muweke katika uislamu, na uliyemfisha basi mfishe juu ya imani, Ewe Mwenyezi Mungu muweke katika uislamu, na unayemfisha usitupoteze baada yake.

Chanzo: Ibn Majah 1/480, Ahmad 2/368.

3

اللَّهُمَّ إِنَّ فُلاَنَ بْنَ فُلاَنٍ فِي ذِمَّتِكَ, وَحَبْلِ جِوَارِكَ, فَقِهِ مِنْ فِتْنَةِ الْقَبْرِ, وَعَذَابِ النَّارِ, وَأَنْتَ أَهْلُ الْوَفَاءِ وَالْحَقِّ, فَاغْفِرْ لَهُ وَارْحَمْهُ إِنَّكَ أَنْتَ الغَفُورُ الرَّحيمُ

Ewe Mwenyezi Mungu hakika fulani bin fulani yuko katika dhima yako, na kamba ya ujirani wako, basi mkinge na fitna ya kaburi na adhabu ya moto, nawe ndiwe mstahiki wa utekelezaji na ukweli, basi msamehe na umrehemu hakika Wewe ni mwingi wa kusamehe, mwingi wa kurehemu.

Chanzo: Ibn Majah, Abu Dawud 3/211.

4

اللَّهُمَّ عَبْدُكَ وَابْنُ أَمَتِكَ احْتَاجَ إِلَى رَحْمَتِكَ, وَأَنْتَ غَنِيٌّ عَنْ عَذَابِهِ, إِنْ كَانَ مُحْسِناً فَزِدْ فِي حَسَنَاتِهِ, وَإِنْ كَانَ مُسِيئاً فَتَجَاوَزْ عَنْهُ

Ewe Mwenyezi Mungu mja wako na mtoto wa kijakazi chako, ni muhitaji wa rehema yako, nawe huhitaji na kumuadhibu, kwahiyo akiwa ni mwema mzidishie katika mema yake, na akiwa ni muovu msamehe madhambi yake.

Chanzo: Al-Hakim 1/359.