1
اللَّهُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ لاَ تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلاَ نَوْمٌ لَّهُ مَا فِي السَّمَوَاتِ وَمَا فِي الأَرْضِ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِنْدَهُ إِلاَّ بِإِذْنِهِ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلاَ يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلاَّ بِمَا شَاء وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلاَ يَؤُودُهُ حِفْظُهُمَا وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ
Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye Mkuu.
Chanzo: Al-Hakim 1 / 562, Sahih at-Targhib wa at-Tarhib 1/273, at-Tabarani.
2
بسم الله الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴿قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ* اللَّهُ الصَّمَدُ* لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ* وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُواً أَحَدٌ﴾.
بسم الله الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴿قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ* مِن شَرِّ مَا خَلَقَ* وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ* وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ* وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ﴾.
بسم الله الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴿قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ* مَلِكِ النَّاسِ* إِلَهِ النَّاسِ* مِن شَرِّ الْوَسْوَاسِ الْخَنَّاسِ* الَّذِي يُوَسْوِسُ فِي صُدُورِ النَّاسِ* مِنَ الْجِنَّةِ وَ النَّاسِ﴾
(ثلاث مرات )
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa. Hakuzaa wala hakuzaliwa. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja. Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko, Na shari ya alivyo viumba, Na shari ya giza la usiku liingiapo, Na shari ya wanao pulizia mafundoni, Na shari ya hasidi anapo husudu. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu, Mfalme wa wanaadamu, Mungu wa wanaadamu, Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas, Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu, Kutokana na majini na wanaadamu.
Chanzo: Al-Ikhlas:1-4. Al-Falaq:1-5. An-Nas:1-6, Abu Dawud 4/322, At-Tirmizi 5/567, Sahih At-Tirmizi 3/182.
3
أَصْبَحْنَا وَأَصْبَحَ الْمُلْكُ لِلَّهِ, وَالْحَمْدُ لِلَّهِ, لاَ إِلَهَ إلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ, لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ, رَبِّ أَسْأَلُكَ خَيْرَ مَا فِي هَذَا الْيَوْمِ وَخَيرَ مَا بَعْدَهُ, وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِي هَذَا الْيَوْمِ وَشَرِّ مَا بَعْدَهُ, رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنَ الْكَسَلِ وَسُوءِ الْكِبَرِ, رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابٍ فِي النَّارِ وَعَذَابٍ فِي الْقَبْرِ
Tumeingia wakati wa asubuhi na umekuwa Ufalme ni wa Mwenyezi Mungu, na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa ila ni Mwenyezi Mungu, hali ya kuwa peke yake hana mshirika, ni wake Ufalme na ni zake sifa njema, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza, Ewe Mola, nakuomba kheri ya siku ya leo, na kheri ya baada ya siku hii, na ninajilinda kwako kutokana na shari ya siku ya leo na shari ya baada ya siku hii, Ewe Mola, najilinda kwako kutokana na uvivu, na ubaya wa uzee (uzee mbaya), Ewe Mola, najilinda kwako kutokana na adhabu ya moto na adhabu ya kaburi. Na ikiingia jioni atasema: Tumeingia jioni na imefika jioni na Ufalme ni wa Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe vyote, Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba kheri ya usiku huu, na najilinda kwako kutokana na shari ya kilicho ndani ya usiku huu, na shari ya baada ya usiku huu.
Chanzo: Muslim 4/2088.
4
اللَّهُمَّ بِكَ أَصْبَحْنَا, وَبِكَ أَمْسَيْنَا, وَبِكَ نَحْيَا, وَبِكَ نَمُوتُ وَإِلَيْكَ النُّشُورُ
Ewe Mwenyezi Mungu kwa sababu yako tumeingia katika wakati wa asubuhi, na kwa ajili yako tumeingia jioni, na kwa ajili yako ndio tumekuwa hai, na kwa ajili yako tutakufa na kwako tutafufuliwa. Na ikifika jioni atasema: Ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili yako tumefika jioni, na kwa ajili yako tumefika asubuhi, na kwa ajili yako tuko hai, na kwa ajili yako tutakufa na ni kwako tu marejeo.
Chanzo: Sahih At-Tirmizi 3/142.
5
اللَّهُمَّ أَنْتَ رَبِّي لَا إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ, خَلَقْتَنِي وَأَنَا عَبْدُكَ, وَأَنَا عَلَى عَهْدِكَ وَوَعْدِكَ مَا اسْتَطَعْتُ, أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا صَنَعْتُ, أَبُوءُ لَكَ بِنِعْمَتِكَ عَلَيَّ, وَأَبُوءُ بِذَنْبِي فَاغْفِرْ لِي فَإِنَّهُ لاَ يَغْفِرُ الذُّنوبَ إِلاَّ أَنْتَ
Ewe mwenyezi Mungu Wewe ni Mola wangu, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja wako, nami niko juu ya ahadi yako, na agano lako, kiasi cha uwezo wangu, najilinda kwako kutokana na shari ya nilicho kifanya, nakiri kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unisamehe kwani hakuna mwenye kusamehe madhambi ila Wewe.
Chanzo: Al-Bukhari 7/150, An-Nasa'i, At-Tirmizi.
6
اللَّهُمَّ إِنِّي أَصْبَحْتُ أُشْهِدُكَ, وَأُشْهِدُ حَمَلَةَ عَرْشِكَ, وَمَلاَئِكَتَكَ, وَجَمِيعَ خَلْقِكَ, أَنَّكَ أَنْتَ اللَّهُ لَا إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ وَحْدَكَ لاَ شَرِيكَ لَكَ, وَأَنَّ مُحَمَّداً عَبْدُكَ وَرَسُولُكَ (أربع مرات)
Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nimefika asubuhi nakushuhudia na nina washuhudiza wabeba wa arshi yako, na Malaika wako, na viumbe wako wote, kwamba Wewe ndiye Mwenyezi Mungu, hapana apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, hali ya kuwa peke yako huna mshirika, na kwamba Muhammad ni mja wako na ni Mtume wako. (Atasema hivo mara nne asubuhi au jioni). Atakae yasema hayo asubuhi au jioni mara nne, Mwenyezi Mungu (S.W) atamuepusha na moto.
Chanzo: Abu Dawud 4/317, An-Nasa'i, Ibn As-Sunni.
7
اللَّهُمَّ مَا أَصْبَحَ بِي مِنْ نِعْمَةٍ أَوْ بِأَحَدٍ مِنْ خَلْقِكَ فَمِنْكَ وَحْدَكَ لاَ شَرِيكَ لَكَ, فَلَكَ الْحَمْدُ وَلَكَ الشُّكْرُ
Ewe Mweneyezi Mungu sikuamka na neema yoyote au kati ya kiumbe chako chochote, na neema ila inatoka kwako, hali ya kuwa peke yako huna mshirika wako, ni zako sifa njema na ni zako shukrani. Atakaesema maneno hayo kila asubuhi basi atakuwa ametekeleza shukrani za siku nzima, na atakae yasema jioni atakuwa ametekeleza shukrani za usiku mzima.
Chanzo: Abu Dawud 4/318, Ibn As-Sunni (Hadith no. 41), Ibn Hibban (Hadith no. 2361).
8
اللَّهُمَّ عَافِنِي فِي بَدَنِي, اللَّهُمَّ عَافِنِي فِي سَمْعِي, اللَّهُمَّ عَافِنِي فِي بَصَرِي, لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ. اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ الْكُفْرِ, وَالفَقْرِ, وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابِ القَبْرِ, لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ (ثلاث مرات)
Ewe Mwenyezi Mungu nipe afya ya mwili wangu, Ewe Mwenyezi Mungu nipe afya ya usikizi wangu, Ewe Mwenyezi Mungu nipe afya ya uoni wangu, hapana Mola asae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, (mara tatu). Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwako kutokana na ukafiri, na ufakiri, na najilinda kwako kutokana na adhabu ya kaburi, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe. (mara tatu).
Chanzo: Abu Dawud 4/324, Ahmad 5/42, An-Nasa'i, Ibn As-Sunni (Hadith no. 69), Ibn Hibban (Hadith no. 2361).
9
حَسْبِيَ اللَّهُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ عَلَيهِ تَوَكَّلتُ وَهُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ (سبع مرات)
Ananitosha Mwenyezi Mungu, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa hakiila Yeye, kwake Yeye nimetegemea, na Yeye ni Mola wa arshi tukufu. (mara saba asubuhi na jioni)
Chanzo: Ibn As-Sunni (no. 71), Abu Dawud 4/321, Ibn As-Sunni.
10
اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ الْعَفْوَ وَالْعَافِيَةَ فِي الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ, اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ الْعَفْوَ وَالْعَافِيَةَ: فِي دِينِي وَدُنْيَايَ وَأَهْلِي, وَمَالِي, اللَّهُمَّ اسْتُرْ عَوْرَاتِي, وَآمِنْ رَوْعَاتِي, اللَّهُمَّ احْفَظْنِي مِنْ بَينِ يَدَيَّ, وَمِنْ خَلْفِي, وَعَنْ يَمِينِي, وَعَنْ شِمَالِي, وَمِنْ فَوْقِي, وَأَعُوذُ بِعَظَمَتِكَ أَنْ أُغْتَالَ مِنْ تَحْتِي
Ewe Mwenyezi Mungu nakuomba msamaha na afya duniani na akhera. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba msamaha na afya katika dini yangu na dunia yangu na jamaa zangu, na mali zangu, Ewe Mwenyezi Mungu nisitiri uchi wangu, na unitulize khofu yangu, Ewe Mwenyezi Mungu nihifadhi mbele yangu, na nyuma yangu, na kulia kwangu, na kushoto kwangu, na juu yangu, na najilinda kwa utukufu wako kwa kutekwa chini yangu.
Chanzo: Sahih Ibn Majah 2/332, Abu Dawud.
11
اللَّهُمَّ عَالِمَ الغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ فَاطِرَ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضِ, رَبَّ كُلِّ شَيْءٍ وَمَلِيكَهُ, أَشْهَدُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ, أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ نَفْسِي, وَمِنْ شَرِّ الشَّيْطانِ وَشَرَكِهِ, وَأَنْ أَقْتَرِفَ عَلَى نَفْسِي سُوءاً, أَوْ أَجُرَّهُ إِلَى مُسْلِمٍ
Ewe Mwenyezi Mungu, mjuzi wa yaliyojificha na yaliyowazi, Muumba wa mbingu na ardhi, Mola wa kila kitu, na Mfalme wake (wa vitu vyote), nakiri kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, najilinda kwako kutokana na shari ya nafsi yangu, na shari ya shetani na shirki yake, na kujichumia uovu kwa nafsi yangu au kumletea muislamu.
Chanzo: Sahih At-Tirmizi 3/142, Abu Dawud.
12
بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لاَ يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلاَ فِي السّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ (ثلاث مرات)
Kwa jina la Mwenyezi Mungu ambae hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kilichopo ardhini wala mbinguni, nae ni Msikivu na Mjuzi. (mara tatu).
Chanzo: Abu Dawud 4/323, At-Tirmizi 5/465, Ibn Majah 2/332, Ahmad.
13
رَضِيتُ بِاللَّهِ رَبَّاً, وَبِالْإِسْلاَمِ دِيناً, وَبِمُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم نَبِيّاً (ثلاث مرات)
Nimeridhia kuwa Ewe Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu, na uislamu ndiyo dini yangu, na Muhammad (s.a.w) kuwa ndiye Mtume wangu. (mara tatu).
Chanzo: Ahmad 4/ 337, An-Nasa'i, Ibn As-Sunni (no. 68), At-Tirmizi 5/465.
14
يَا حَيُّ يَا قَيُّومُ بِرَحْمَتِكَ أَسْتَغيثُ أَصْلِحْ لِي شَأْنِيَ كُلَّهُ وَلاَ تَكِلْنِي إِلَى نَفْسِي طَرْفَةَ عَيْنٍ
Ewe Uliyehai, Uliyesimama kwa dhati yako, kwa rehema zako ninakuomba uniokoe, nitengenezee mambo yangu yote, wala usiniachie mambo yangu mwenyewe (pasina kunisaidia), hata kwa muda (mdogo, kama muda) wa kupepesa jicho.
Chanzo: Al-Hakim 1/545.
15 AI
أَصْبَحْنَا وَأَصْبَحَ الْمُلْكُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ, اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَ هَذَا الْيَوْمِ:فَتْحَهُ, وَنَصْرَهُ, وَنورَهُ, وَبَرَكَتَهُ, وَهُدَاهُ, وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِيهِ وَشَرِّ مَا بَعْدَهُ
Tumeingia asubuhi na ufalme wote ni wa Allah, Mola wa walimwengu. Ee Allah! Nakuomba heri ya siku hii: ushindi wake, nusura yake, nuru yake, baraka zake na uongofu wake; na najilinda kwako kutokana na shari yake na shari ya yanayokuja baada yake. (Jioni: "Tumeingia jioni..." ukitaja usiku.)
Chanzo: Abu Dawud 4/322.
16
أَصْبَحْنا عَلَى فِطْرَةِ الْإِسْلاَمِ, وَعَلَى كَلِمَةِ الْإِخْلاَصِ, وَعَلَى دِينِ نَبِيِّنَا مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم, وَعَلَى مِلَّةِ أَبِينَا إِبْرَاهِيمَ, حَنِيفاً مُسْلِماً وَمَا كَانَ مِنَ الْمُشرِكِينَ
Tumeingia asubuhi na maumbile ya kiislamu, na neno la ikhlasi, na dini ya Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na mila (dini) ya Baba yetu Ibrahim iliyo sawa hali ya kuwa muislamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu. Na ikiingia jioni atasema: Tumeingia jioni na maumbile ya kiislamu, na neno la ikhlasi, na dini ya Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na mila (dini) ya Baba yetu Ibrahim iliyo sawa hali ya kuwa muislamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu
Chanzo: Ahmad 3/406-7, 5/123, An-Nasa'i, At-Tirmizi 4/209.
17
سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ (مائة مرة)
Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni zake. (mara mia moja).
Chanzo: Muslim 4/2071.
18
لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ, لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ, وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ (عشر مرات أو مرة واحدة عند الكسل)
Hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu peke yake, hana mshirika wake, niwake Ufalme, na ni zake sifa njema zote, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. (Mara kumi, au mara moja ukisikia uvivu).
Chanzo: An-Nasa'i, Abu Dawud 4/319, Ibn Majah, Ahmad 4/60.
19
لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ, وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ, لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ (مائة مرة)
Amesema Mtume (s.a.w): Mwenye kusema inapoingia asubuhi: Hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu peke yake, hana mshirika wake, niwake Ufalme, na ni zake sifa njema zote, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. ......kwa siku mara mia moja, basi yeye ana thawabu za kuwaacha huru watumwa kumi, na ataandikiwa thawabu mia moja, na atafutiwa madhambi mia moja, na atakuwa na kinga ya shetani kwa siku hiyo mpaka jioni, na hapatakuwa na mtu bora kumshinda, ila yule aliyefanya zaidi yake.
Chanzo: Al-Bukhari 4/95, Muslim 4/2071.
20
سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ: عَدَدَ خَلْقِهِ, وَرِضَا نَفْسِهِ, وَزِنَةَ عَرْشِهِ, وَمِدَادَ كَلِمَاتِهِ (ثلاث مرات)
Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni zake, kwa hesabu ya viumbe wake, na radhi yake, na uzito wa arshi yake, na wino wa maneno yake, (mara tatu kila asubuhi)
Chanzo: Muslim 4/2090.
21 AI
اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ عِلْماً نَافِعاً, وَرِزْقاً طَيِّباً, وَعَمَلاً مُتَقَبَّلاً
Ee Allah! Nakuomba elimu yenye manufaa, riziki nzuri na amali iliyokubaliwa.
Chanzo: Ibn As-Sunni (Hadith no. 54), Ibn Majah (Hadith no. 925).
22
أَسْتَغْفِرُ اللَّهَ وَأَتُوبُ إِلَيْهِ (مائة مرة في اليوم)
Nakuomba msamaha Mwenyezi Mungu, na ninarejea kwake. (mara mia moja kwa siku).
Chanzo: Al-Bukhari, Muslim 4/2075.
23
اللَّهُمَّ صَلِّ وَسَلِّمْ عَلَى نَبَيِّنَا مُحَمَّدٍ (عشر مرات)
Ewe Mwenyezi Mungu mfikishie rehema na amani Mtume wetu Muhammad. ....Mwenye kuniombea rehema asubuhi mara kumi, na jioni mara kumi, nitamuombea shifaa (msamaha) siku ya kiayama.
Chanzo: At-Tabrani, Sahih at-Targhib wa at-Tarhib 1/273.