Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Adh-Dhariyat
51

Adh-Dhariyat — Zinazotawanya

الذَّارِيَاتِ
Za Makka Aya 60
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلذَّٰرِيَٰتِ ذَرْوًۭا

Waz-zaariyaati zarwaa

Naapa kwa pepo zinazo tawanya,

Aya 2

فَٱلْحَٰمِلَٰتِ وِقْرًۭا

Falhaamilaati wiqraa

Na zinazo beba mizigo,

Aya 3

فَٱلْجَٰرِيَٰتِ يُسْرًۭا

Faljaariyaati yusraa

Na zinazo kwenda kwa wepesi.

Aya 4

فَٱلْمُقَسِّمَٰتِ أَمْرًا

Falmuqassimaati amraa

Na zinazo gawanya kwa amri,

Aya 5

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌۭ

Innamaa too'adoona la-saadiq

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,

Aya 6

وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٌۭ

Wa innad deena la waaqi'

Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.

Aya 7

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْحُبُكِ

Wassamaaa'i zaatil hubuk

Naapa kwa mbingu zenye njia,

Aya 8

إِنَّكُمْ لَفِى قَوْلٍۢ مُّخْتَلِفٍۢ

Innakum lafee qawlim mukhtalif

Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.

Aya 9

يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ

Yu'faku 'anhu man ufik

Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.

Aya 10

قُتِلَ ٱلْخَرَّٰصُونَ

Qutilal kharraasoon

Wazushi wameangamizwa.

Aya 11

ٱلَّذِينَ هُمْ فِى غَمْرَةٍۢ سَاهُونَ

Allazeena hum fee ghamratin saahoon

Ambao wameghafilika katika ujinga.

Aya 12

يَسْـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلدِّينِ

Yas'aloona ayyaana yawmud Deen

Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?

Aya 13

يَوْمَ هُمْ عَلَى ٱلنَّارِ يُفْتَنُونَ

Yawma hum 'alan naari yuftanoon

Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.

Aya 14

ذُوقُوا۟ فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تَسْتَعْجِلُونَ

Zooqoo fitnatakum haa zal lazee kuntum bihee tas ta'jiloon

Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.

Aya 15

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍ

Innal muttaqeena fee jannaatinw wa 'uyoon

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

Aya 16

ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ

Aakhizeena maaa aataahum Rabbuhum; innahum kaanoo qabla zaalika muhsineen

Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

Aya 17

كَانُوا۟ قَلِيلًۭا مِّنَ ٱلَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ

kaanoo qaleelam minal laili maa yahja'oon

Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.

Aya 18

وَبِٱلْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ

Wa bilashaari hum yastaghfiroon

Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

Aya 19

وَفِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّۭ لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ

Wa feee amwaalihim haqqul lissaaa'ili walmahroom

Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.

Aya 20

وَفِى ٱلْأَرْضِ ءَايَٰتٌۭ لِّلْمُوقِنِينَ

Wa fil ardi aayaatul lilmooqineen

Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

Aya 21

وَفِىٓ أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ

Wa feee anfusikum; afalaa tubsiroon

Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?

Aya 22

وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ

Wa fissamaaa'i rizqukum wa maa too'adoon

Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.

Aya 23

فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ لَحَقٌّۭ مِّثْلَ مَآ أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ

Fawa Rabbis samaaa'i wal ardi innahoo lahaqqum misla maa annakum tantiqoon

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

Aya 24

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ ٱلْمُكْرَمِينَ

Hal ataaka hadeesu daifi Ibraaheemal mukrameen

Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?

Aya 25

إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَٰمًۭا ۖ قَالَ سَلَٰمٌۭ قَوْمٌۭ مُّنكَرُونَ

Iz dakhaloo 'alaihi faqaaloo salaaman qaala salaamun qawmum munkaroon

Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.

Aya 26

فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجْلٍۢ سَمِينٍۢ

Faraagha ilaaa ahlihee fajaaa'a bi'ijlin sameen

Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.

Aya 27

فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ

Faqarrabahooo ilaihim qaala alaa taakuloon

Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?

Aya 28

فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةًۭ ۖ قَالُوا۟ لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٍۢ

Fa awjasa minhm khee fatan qaaloo laa takhaf wa bashsharoohu bighulaamin 'aleem

Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.

Aya 29

فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُۥ فِى صَرَّةٍۢ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌۭ

Fa aqbalatim ra-atuhoo fee sarratin fasakkat wajhahaa wa qaalat 'ajoozun 'aqeem

Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!

Aya 30

قَالُوا۟ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْحَكِيمُ ٱلْعَلِيمُ

Qaaloo kazaaliki qaala Rabbuki innahoo huwal hakeemul 'aleem

Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.

Aya 31

۞ قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ

Qaala famaa khatbukum ayyuhal mursaloon

AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?

Aya 32

قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍۢ مُّجْرِمِينَ

Qaalooo innaaa ursilnaaa ilaa qawmim mujrimeen

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,

Aya 33

لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةًۭ مِّن طِينٍۢ

Linursila 'alaihim hijaa ratam min teen

Tuwatupie mawe ya udongo,

Aya 34

مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ

Musawwamatan 'inda rabbika lilmusrifeen

Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.

Aya 35

فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Fa akhrajnaa man kaana feehaa minal mu'mineen

Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.

Aya 36

فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍۢ مِّنَ ٱلْمُسْلِمِينَ

Famaa wajadnaa feehaa ghaira baitim minal muslimeen

Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

Aya 37

وَتَرَكْنَا فِيهَآ ءَايَةًۭ لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ

Wa taraknaa feehaaa aayatal lillazeena yakhaafoonal 'azaabal aleem

Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.

Aya 38

وَفِى مُوسَىٰٓ إِذْ أَرْسَلْنَٰهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَٰنٍۢ مُّبِينٍۢ

Wa fee Moosaaa iz arsalnaahu ilaa Fir'wna bisultaa nim mubeen

Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.

Aya 39

فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِۦ وَقَالَ سَٰحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌۭ

Fatawalla biruknihee wa qaala saahirun aw majnoon

Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!

Aya 40

فَأَخَذْنَٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذْنَٰهُمْ فِى ٱلْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌۭ

Fa akhaznaahu wa junoo dahoo fanabaznaahum fil yammi wa huwa muleem

Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.

Aya 41

وَفِى عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلْعَقِيمَ

Wa fee 'Aadin iz arsalnaa 'alaihimur reehal'aqeem

Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.

Aya 42

مَا تَذَرُ مِن شَىْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَٱلرَّمِيمِ

Maa tazaru min shai'in atat 'alaihi illaa ja'alat hu karrameem

Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.

Aya 43

وَفِى ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا۟ حَتَّىٰ حِينٍۢ

Wa fee Samooda iz qeela lahum tamatta''oo hattaa heen

Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.

Aya 44

فَعَتَوْا۟ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّٰعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ

Fa'ataw 'an amri Rabbihim fa akhazal humus saa'iqatu wa hum yanzuroon

Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.

Aya 45

فَمَا ٱسْتَطَٰعُوا۟ مِن قِيَامٍۢ وَمَا كَانُوا۟ مُنتَصِرِينَ

Famas tataa'oo min qiyaaminw wa maa kaanoo muntasireen

Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

Aya 46

وَقَوْمَ نُوحٍۢ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَوْمًۭا فَٰسِقِينَ

Wa qawma Noohim min qablu innahum kaano qawman faasiqeen

Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

Aya 47

وَٱلسَّمَآءَ بَنَيْنَٰهَا بِأَيْي۟دٍۢ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ

Wassamaaa'a banainaa haa bi aydinw wa innaa lamoosi'oon

Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.

Aya 48

وَٱلْأَرْضَ فَرَشْنَٰهَا فَنِعْمَ ٱلْمَٰهِدُونَ

Wal arda farashnaahaa fani'mal maahidoon

Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

Aya 49

وَمِن كُلِّ شَىْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ

Wa min kulli shai'in khalaqnaa zawjaini la'allakum tazakkaroon

Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

Aya 50

فَفِرُّوٓا۟ إِلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌۭ مُّبِينٌۭ

Fafirrooo ilal laahi innee lakum minhu nazeerum mubeen

Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Aya 51

وَلَا تَجْعَلُوا۟ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌۭ مُّبِينٌۭ

Wa laa taj'aloo ma'al laahi ilaahan aakhara innee lakum minhu nazeerum mubeen

Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Aya 52

كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا۟ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ

Kazaalika maaa atal lazeena min qablihim mir Rasoolin illaa qaaloo saahirun aw majnoon

Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.

Aya 53

أَتَوَاصَوْا۟ بِهِۦ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌۭ طَاغُونَ

Atawaasaw bih; bal hum qawmun taaghoon

Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.

Aya 54

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٍۢ

Fatawalla 'anhum famaaa anta bimaloom

Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.

Aya 55

وَذَكِّرْ فَإِنَّ ٱلذِّكْرَىٰ تَنفَعُ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Wa zakkir fa innaz zikraa tanfa'ul mu'mineen

Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

Aya 56

وَمَا خَلَقْتُ ٱلْجِنَّ وَٱلْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ

Wa maa khalaqtul jinna wal insa illaa liya'budoon

Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.

Aya 57

مَآ أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍۢ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ

Maaa ureedu minhum mir rizqinw wa maaa ureedu anyyut'imoon

Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.

Aya 58

إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلْقُوَّةِ ٱلْمَتِينُ

Innal laaha Huwar Razzaaqu Zul Quwwatil Mateen

Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.

Aya 59

فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ ذَنُوبًۭا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَٰبِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ

Fa inna lillazeena zalamoo zanoobam misla zanoobi ashaabihim falaa yasta'jiloon

Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.

Aya 60

فَوَيْلٌۭ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِن يَوْمِهِمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ

Fawailul lillazeena kafaroo miny yawmihimul lazee yoo'adoon

Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.