Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / At-Tur
52

At-Tur — Mlima

الطُّورِ
Za Makka Aya 49
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلطُّورِ

Wat-Toor

Naapa kwa mlima wa T'ur,

Aya 2

وَكِتَٰبٍۢ مَّسْطُورٍۢ

Wa kitaabim mastoor

Na Kitabu kilicho andikwa

Aya 3

فِى رَقٍّۢ مَّنشُورٍۢ

Fee raqqim manshoor

Katika ngozi iliyo kunjuliwa,

Aya 4

وَٱلْبَيْتِ ٱلْمَعْمُورِ

Wal baitil ma'moor

Na kwa Nyumba iliyo jengwa,

Aya 5

وَٱلسَّقْفِ ٱلْمَرْفُوعِ

Wassaqfil marfoo'

Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,

Aya 6

وَٱلْبَحْرِ ٱلْمَسْجُورِ

Wal bahril masjoor

Na kwa bahari iliyo jazwa,

Aya 7

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٌۭ

Inna 'azaaba Rabbika lawaaqi'

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.

Aya 8

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٍۢ

Maa lahoo min daafi'

Hapana wa kuizuia.

Aya 9

يَوْمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوْرًۭا

Yawma tamoorus samaaa'u mawraa

Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,

Aya 10

وَتَسِيرُ ٱلْجِبَالُ سَيْرًۭا

Wa taseerul jibaalu sairaa

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.

Aya 11

فَوَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Fawailuny yawma 'izil lil mukaazzibeen

Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,

Aya 12

ٱلَّذِينَ هُمْ فِى خَوْضٍۢ يَلْعَبُونَ

Allazeena hum fee khawdiny yal'aboon

Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.

Aya 13

يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Yawma yuda'-'oona ilaa naari jahannama da'-'aa

Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,

Aya 14

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِى كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Haazihin naarul latee kuntum bihaa tukazziboon

(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!

Aya 15

أَفَسِحْرٌ هَٰذَآ أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ

Afasihrun haazaaaa am antum laa tubsiroon

Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?

Aya 16

ٱصْلَوْهَا فَٱصْبِرُوٓا۟ أَوْ لَا تَصْبِرُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Islawhaa fasbirooo aw laa tasbiroo sawaaa'un 'alaikum innamaa tujzawna maa kuntum ta'maloon

Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.

Aya 17

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍۢ وَنَعِيمٍۢ

Innal muttaqeena fee jannaatinw wa na'eem

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,

Aya 18

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَىٰهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ ٱلْجَحِيمِ

Faakiheena bimaaa aataahum rabbuhum wa waqaahum rabbuhum 'azaabal jaheem

Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.

Aya 19

كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Kuloo washraboo haneee 'am bimaa kuntum ta'maloon

Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.

Aya 20

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٍۢ مَّصْفُوفَةٍۢ ۖ وَزَوَّجْنَٰهُم بِحُورٍ عِينٍۢ

Muttaki'eena 'alaa sururim masfoofatinw wa zawwaj naahum bihoorin 'een

Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.

Aya 21

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَٱتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَآ أَلَتْنَٰهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَىْءٍۢ ۚ كُلُّ ٱمْرِئٍۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌۭ

Wallazeena aamanoo wattaba'at hum zurriyyatuhum bieemaanin alhaqnaa bihim zurriyyatahum wa maaa alatnaahum min 'amalihim min shai'; kullum ri'im bimaa kasaba raheen

Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.

Aya 22

وَأَمْدَدْنَٰهُم بِفَٰكِهَةٍۢ وَلَحْمٍۢ مِّمَّا يَشْتَهُونَ

Wa amdadnaahum bifaa kihatinw wa lahmim mimmaa yashtahoon

Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.

Aya 23

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأْسًۭا لَّا لَغْوٌۭ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌۭ

Yatanaaza'oona feehaa kaasal laa laghwun feehaa wa laa taaseem

Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.

Aya 24

۞ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌۭ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌۭ مَّكْنُونٌۭ

Wa yatoofu 'alaihim ghilmaanul lahum ka annahum lu'lu'um maknoon

Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.

Aya 25

وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَسَآءَلُونَ

Wa aqbala ba'duhum 'alaa ba'diny yatasaaa'aloon

Wataelekeana wakiulizana.

Aya 26

قَالُوٓا۟ إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِىٓ أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ

Qaalooo innaa kunnaa qablu feee ahlinaa mushfiqeen

Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;

Aya 27

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Famannnal laahu 'alainaa wa waqaanaa 'azaabas samoom

Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.

Aya 28

إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Innaa kunnaa min qablu nad'oohu innahoo huwal barrur raheem

Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.

Aya 29

فَذَكِّرْ فَمَآ أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍۢ وَلَا مَجْنُونٍ

Fazakkir famaaa anta bini'mati rabbika bikaahininw wa laa majnoon

Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.

Aya 30

أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌۭ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيْبَ ٱلْمَنُونِ

Am yaqooloona shaa'irun natarabbasu bihee raibal manoon

Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.

Aya 31

قُلْ تَرَبَّصُوا۟ فَإِنِّى مَعَكُم مِّنَ ٱلْمُتَرَبِّصِينَ

Qul tarabbasoo fa innee ma'akum minal mutarabbiseen

Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.

Aya 32

أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَٰمُهُم بِهَٰذَآ ۚ أَمْ هُمْ قَوْمٌۭ طَاغُونَ

Am taamuruhum ahlaamuhum bihaazaaa am hum qawmun taaghoon

Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?

Aya 33

أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥ ۚ بَل لَّا يُؤْمِنُونَ

Am yaqooloona taqawwalah; bal laa yu'minoon

Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!

Aya 34

فَلْيَأْتُوا۟ بِحَدِيثٍۢ مِّثْلِهِۦٓ إِن كَانُوا۟ صَٰدِقِينَ

Falyaatoo bihadeesim misliheee in kaanoo saadiqeen

Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.

Aya 35

أَمْ خُلِقُوا۟ مِنْ غَيْرِ شَىْءٍ أَمْ هُمُ ٱلْخَٰلِقُونَ

Am khuliqoo min ghairi shai'in am humul khaaliqoon

Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

Aya 36

أَمْ خَلَقُوا۟ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ ۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ

Am khalaqus samaawaati wal ard; bal laa yooqinoon

Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.

Aya 37

أَمْ عِندَهُمْ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ ٱلْمُصَۣيْطِرُونَ

Am'indahum khazaaa'inu rabbika am humul musaitiroon

Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

Aya 38

أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌۭ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ ۖ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُم بِسُلْطَٰنٍۢ مُّبِينٍ

Am lahum sullamuny yastami'oona feehi falyaati mustami'uhum bisultaanim mubeen

Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!

Aya 39

أَمْ لَهُ ٱلْبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلْبَنُونَ

Am lahul banaatu wa lakumul banoon

Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?

Aya 40

أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًۭا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍۢ مُّثْقَلُونَ

Am tas'aluhum ajran fahum mim maghramim musqaloon

Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?

Aya 41

أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ

Am 'indahumul ghaibu fahum yaktuboon

Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?

Aya 42

أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًۭا ۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ هُمُ ٱلْمَكِيدُونَ

Am yureedoona kaidan fallazeena kafaroo humul makeedoon

Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.

Aya 43

أَمْ لَهُمْ إِلَٰهٌ غَيْرُ ٱللَّهِ ۚ سُبْحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ

Am lahum ilaahun ghairul laa; subhaanal laahi 'ammaa yushrikoon

Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.

Aya 44

وَإِن يَرَوْا۟ كِسْفًۭا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطًۭا يَقُولُوا۟ سَحَابٌۭ مَّرْكُومٌۭ

Wa iny yaraw kisfam minas samaaa'i saaqitany yaqooloo sahaabum markoom

Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.

Aya 45

فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى فِيهِ يُصْعَقُونَ

Fazarhum hatta yulaaqoo yawmahumul lazee feehi yus'aqoon

Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.

Aya 46

يَوْمَ لَا يُغْنِى عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْـًۭٔا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ

Yawma laa yughnee 'anhum kaidumhum shai'anw wa laa hum yunsaroon

Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.

Aya 47

وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ عَذَابًۭا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ

Wa inna lillazeena zalamoo 'azaaban doona zalika wa laakinna aksarahum laa ya'lamoon

Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.

Aya 48

وَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا ۖ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ

Wasbir lihukmi rabbika fa innaka bi-a'yuninaa wa sabbih bihamdi rabbika heena taqoom

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,

Aya 49

وَمِنَ ٱلَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَٰرَ ٱلنُّجُومِ

Wa minal laili fasabbihhu wa idbaaran nujoom

Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.