Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / An-Najm
53

An-Najm — Nyota

النَّجۡمِ
Za Makka Aya 62
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلنَّجْمِ إِذَا هَوَىٰ

Wannajmi izaa hawaa

Naapa kwa nyota inapo tua,

Aya 2

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمْ وَمَا غَوَىٰ

Maa dalla saahibukum wa maa ghawaa

Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.

Aya 3

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلْهَوَىٰٓ

Wa maa yyantiqu 'anilhawaaa

Wala hatamki kwa matamanio.

Aya 4

إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْىٌۭ يُوحَىٰ

In huwa illaa Wahyuny yoohaa

Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;

Aya 5

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلْقُوَىٰ

'Allamahoo shadeedul quwaa

Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,

Aya 6

ذُو مِرَّةٍۢ فَٱسْتَوَىٰ

Zoo mirratin fastawaa

Mwenye kutua, akatulia,

Aya 7

وَهُوَ بِٱلْأُفُقِ ٱلْأَعْلَىٰ

Wa huwa bil ufuqil a'laa

Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.

Aya 8

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Summa danaa fatadalla

Kisha akakaribia na akateremka.

Aya 9

فَكَانَ قَابَ قَوْسَيْنِ أَوْ أَدْنَىٰ

Fakaana qaaba qawsaini aw adnaa

Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.

Aya 10

فَأَوْحَىٰٓ إِلَىٰ عَبْدِهِۦ مَآ أَوْحَىٰ

Fa awhaaa ilaa 'abdihee maaa awhaa

Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.

Aya 11

مَا كَذَبَ ٱلْفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Maa kazabal fu'aadu maa ra aa

Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.

Aya 12

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Afatumaaroonahoo 'alaa maayaraa

Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?

Aya 13

وَلَقَدْ رَءَاهُ نَزْلَةً أُخْرَىٰ

Wa laqad ra aahu nazlatan ukhraa

Na akamwona mara nyingine,

Aya 14

عِندَ سِدْرَةِ ٱلْمُنتَهَىٰ

'Inda sidratil muntaha

Penye Mkunazi wa mwisho.

Aya 15

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلْمَأْوَىٰٓ

'Indahaa jannatul maawaa

Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.

Aya 16

إِذْ يَغْشَى ٱلسِّدْرَةَ مَا يَغْشَىٰ

Iz yaghshas sidrata maa yaghshaa

Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.

Aya 17

مَا زَاغَ ٱلْبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Maa zaaghal basaru wa maa taghaa

Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.

Aya 18

لَقَدْ رَأَىٰ مِنْ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلْكُبْرَىٰٓ

Laqad ra aa min aayaati Rabbihil kubraaa

Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.

Aya 19

أَفَرَءَيْتُمُ ٱللَّٰتَ وَٱلْعُزَّىٰ

Afara'aytumul laata wal 'uzzaa

Je! Mmemuona Lata na Uzza?

Aya 20

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلْأُخْرَىٰٓ

Wa manaatas saalisatal ukhraa

Na Manaat, mwingine wa tatu?

Aya 21

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلْأُنثَىٰ

A-lakumuz zakaru wa lahul unsaa

Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?

Aya 22

تِلْكَ إِذًۭا قِسْمَةٌۭ ضِيزَىٰٓ

Tilka izan qismatun deezaa

Huo ni mgawanyo wa dhulma!

Aya 23

إِنْ هِىَ إِلَّآ أَسْمَآءٌۭ سَمَّيْتُمُوهَآ أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلْطَٰنٍ ۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهْوَى ٱلْأَنفُسُ ۖ وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلْهُدَىٰٓ

In hiya illaaa asmaaa'un sammaitumoohaaa antum wa aabaaa'ukum maaa anzalal laahu bihaa min sultaan; inyyattabi'oona illaz zanna wa maa tahwal anfusu wa laqad jaaa'ahum mir Rabbihimul hudaa

Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.

Aya 24

أَمْ لِلْإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Am lil insaani maa taman naa

Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?

Aya 25

فَلِلَّهِ ٱلْءَاخِرَةُ وَٱلْأُولَىٰ

Falillaahil aakhiratu wal oolaa

Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.

Aya 26

۞ وَكَم مِّن مَّلَكٍۢ فِى ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغْنِى شَفَٰعَتُهُمْ شَيْـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعْدِ أَن يَأْذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرْضَىٰٓ

Wa kam mim malakin fissamaawaati laa tughnee shafaa'atuhum shai'an illaa mim ba'di anyyaazanal laahu limany yashaaa'u wa yardaa

Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.

Aya 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِٱلْءَاخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلْمَلَٰٓئِكَةَ تَسْمِيَةَ ٱلْأُنثَىٰ

innal lazeena laa yu'minoona bil aakhirati la yusammoonal malaaa'ikata tasmiyatal unsaa

Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.

Aya 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنْ عِلْمٍ ۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ ۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغْنِى مِنَ ٱلْحَقِّ شَيْـًۭٔا

Wa maa lahum bihee min 'ilmin iny yattabi'oona illaz zanna wa innaz zanna laa yughnee minal haqqi shai'aa

Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.

Aya 29

فَأَعْرِضْ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكْرِنَا وَلَمْ يُرِدْ إِلَّا ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا

Fa a'rid 'am man tawallaa 'an zikrinaa wa lam yurid illal hayaatad dunyaa

Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.

Aya 30

ذَٰلِكَ مَبْلَغُهُم مِّنَ ٱلْعِلْمِ ۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ ٱهْتَدَىٰ

Zalika mablaghuhum minal 'ilm; inna rabbaka huwa a'lamu biman dalla 'an sabee lihee wa huwa a'lamu bimanih tadaa

Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.

Aya 31

وَلِلَّهِ مَا فِى ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِى ٱلْأَرْضِ لِيَجْزِىَ ٱلَّذِينَ أَسَٰٓـُٔوا۟ بِمَا عَمِلُوا۟ وَيَجْزِىَ ٱلَّذِينَ أَحْسَنُوا۟ بِٱلْحُسْنَى

Wa lillaahi maa fis samaawaati wa maa fil ardi liyajziyal lazeena asaaa'oo bimaa 'amiloo wa yajziyal lazeena ahsanoo bilhusnaa

Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.

Aya 32

ٱلَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَٰٓئِرَ ٱلْإِثْمِ وَٱلْفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَ ۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلْمَغْفِرَةِ ۚ هُوَ أَعْلَمُ بِكُمْ إِذْ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلْأَرْضِ وَإِذْ أَنتُمْ أَجِنَّةٌۭ فِى بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمْ ۖ فَلَا تُزَكُّوٓا۟ أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ

Allazeena yajtaniboona kabaaa'iral ismi walfawaa hisha illal lamam; inna rabbaka waasi'ul maghfirah; huwa a'lamu bikum iz ansha akum minal ardi wa iz antum ajinnatun fee butooni umma haatikum falaa tuzakkooo anfusakum huwa a'lamu bimanit taqaa

Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.

Aya 33

أَفَرَءَيْتَ ٱلَّذِى تَوَلَّىٰ

Afara'ayatal lazee tawallaa

Je! Umemwona yule aliye geuka?

Aya 34

وَأَعْطَىٰ قَلِيلًۭا وَأَكْدَىٰٓ

Wa a'taa qaleelanw wa akdaa

Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?

Aya 35

أَعِندَهُۥ عِلْمُ ٱلْغَيْبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ

A'indahoo 'ilmul ghaibi fahuwa yaraa

Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?

Aya 36

أَمْ لَمْ يُنَبَّأْ بِمَا فِى صُحُفِ مُوسَىٰ

Am lam yunabbaa bimaa fee suhuhfi Moosa

Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?

Aya 37

وَإِبْرَٰهِيمَ ٱلَّذِى وَفَّىٰٓ

Wa Ibraaheemal lazee waffaaa

Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?

Aya 38

أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٌۭ وِزْرَ أُخْرَىٰ

Allaa taziru waaziratunw wizra ukhraa

Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?

Aya 39

وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ

Wa al laisa lil insaani illaa maa sa'aa

Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?

Aya 40

وَأَنَّ سَعْيَهُۥ سَوْفَ يُرَىٰ

Wa anna sa'yahoo sawfa yuraa

Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?

Aya 41

ثُمَّ يُجْزَىٰهُ ٱلْجَزَآءَ ٱلْأَوْفَىٰ

Summa yujzaahul jazaaa 'al awfaa

Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.

Aya 42

وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلْمُنتَهَىٰ

Wa anna ilaa rabbikal muntahaa

Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.

Aya 43

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضْحَكَ وَأَبْكَىٰ

Wa annahoo huwa adhaka wa abkaa

Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.

Aya 44

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحْيَا

Wa annahoo huwa amaata wa ahyaa

Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.

Aya 45

وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰ

Wa annahoo khalaqaz zawjainiz zakara wal unsaa

Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike

Aya 46

مِن نُّطْفَةٍ إِذَا تُمْنَىٰ

Min nutfatin izaa tumnaa

Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.

Aya 47

وَأَنَّ عَلَيْهِ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُخْرَىٰ

Wa anna 'alaihin nash atal ukhraa

Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.

Aya 48

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغْنَىٰ وَأَقْنَىٰ

Wa annahoo huwa aghnaa wa aqnaa

Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.

Aya 49

وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعْرَىٰ

Wa annahoo huwa rabbush shi'raa

Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.

Aya 50

وَأَنَّهُۥٓ أَهْلَكَ عَادًا ٱلْأُولَىٰ

Wa annahooo ahlak a 'Aadanil oolaa

Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,

Aya 51

وَثَمُودَا۟ فَمَآ أَبْقَىٰ

Wa samooda famaaa abqaa

Na Thamudi hakuwabakisha,

Aya 52

وَقَوْمَ نُوحٍۢ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ هُمْ أَظْلَمَ وَأَطْغَىٰ

Wa qawma Noohim min qablu innahum kaanoo hum azlama wa atghaa

Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;

Aya 53

وَٱلْمُؤْتَفِكَةَ أَهْوَىٰ

Wal mu'tafikata ahwaa

Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.

Aya 54

فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ

Faghashshaahaa maa ghashshaa

Vikaifunika vilivyo funika.

Aya 55

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ

Fabi ayyi aalaaa'i Rabbika tatamaaraa

Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?

Aya 56

هَٰذَا نَذِيرٌۭ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلْأُولَىٰٓ

Haazaa nazeerum minan nuzuril oolaa

Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.

Aya 57

أَزِفَتِ ٱلْءَازِفَةُ

Azifatil laazifah

Kiyama kimekaribia!

Aya 58

لَيْسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ

Laisa lahaa min doonil laahi kaashifah

Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.

Aya 59

أَفَمِنْ هَٰذَا ٱلْحَدِيثِ تَعْجَبُونَ

Afamin hazal hadeesi ta'jaboon

Je! Mnayastaajabia maneno haya?

Aya 60

وَتَضْحَكُونَ وَلَا تَبْكُونَ

Wa tadhakoona wa laa tabkoon

Na mnacheka, wala hamlii?

Aya 61

وَأَنتُمْ سَٰمِدُونَ

Wa antum saamidoon

Nanyi mmeghafilika?

Aya 62

فَٱسْجُدُوا۟ لِلَّهِ وَٱعْبُدُوا۟ ۩

Fasjudoo lillaahi wa'budoo

Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.