Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Qamar
54

Al-Qamar — Mwezi

القَمَرِ
Za Makka Aya 55
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

ٱقْتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلْقَمَرُ

Iqtarabatis Saa'atu wsan shaqqal qamar

Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!

Aya 2

وَإِن يَرَوْا۟ ءَايَةًۭ يُعْرِضُوا۟ وَيَقُولُوا۟ سِحْرٌۭ مُّسْتَمِرٌّۭ

Wa iny yaraw aayatany yu'ridoo wa yaqooloo sihrum mustamirr

Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.

Aya 3

وَكَذَّبُوا۟ وَٱتَّبَعُوٓا۟ أَهْوَآءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍۢ مُّسْتَقِرٌّۭ

Wa kazzaboo wattaba'ooo ahwaaa'ahum; wa kullu amrim mustaqirr

Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.

Aya 4

وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّنَ ٱلْأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ

Wa laqad jaaa'ahum minal ambaaa'i maa feehi muzdajar

Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.

Aya 5

حِكْمَةٌۢ بَٰلِغَةٌۭ ۖ فَمَا تُغْنِ ٱلنُّذُرُ

Hikmatum baalighatun famaa tughnin nuzur

Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!

Aya 6

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَىْءٍۢ نُّكُرٍ

Fatawalla 'anhum; yawma yad'ud daa'i ilaa shai 'in nukur

Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;

Aya 7

خُشَّعًا أَبْصَٰرُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌۭ مُّنتَشِرٌۭ

khushsha'an absaaruhum yakrujoona minal ajdaasi ka annahum jaraadum muntashir

Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,

Aya 8

مُّهْطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِ ۖ يَقُولُ ٱلْكَٰفِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌۭ

Muhti'eena ilad daa'i yaqoolul kafiroona haazaa yawmun 'asir

Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.

Aya 9

۞ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍۢ فَكَذَّبُوا۟ عَبْدَنَا وَقَالُوا۟ مَجْنُونٌۭ وَٱزْدُجِرَ

Kazzabat qablahum qawmu Noohin fakazzaboo 'abdanaa wa qaaloo majnoo nunw wazdujir

Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.

Aya 10

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّى مَغْلُوبٌۭ فَٱنتَصِرْ

Fada'aa Rabbahooo annee maghloobun fantasir

Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!

Aya 11

فَفَتَحْنَآ أَبْوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٍۢ مُّنْهَمِرٍۢ

Fafatahnaaa abwaabas sa maaa'i bimaa'im munhamir

Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.

Aya 12

وَفَجَّرْنَا ٱلْأَرْضَ عُيُونًۭا فَٱلْتَقَى ٱلْمَآءُ عَلَىٰٓ أَمْرٍۢ قَدْ قُدِرَ

Wa fajjamal arda 'uyoonan faltaqal maaa'u 'alaaa amrin qad qudir

Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.

Aya 13

وَحَمَلْنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَٰحٍۢ وَدُسُرٍۢ

Wa hamalnaahu 'alaa zaati alwaahinw wa dusur

Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.

Aya 14

تَجْرِى بِأَعْيُنِنَا جَزَآءًۭ لِّمَن كَانَ كُفِرَ

Tajree bi a'yuninaa jazaaa 'al liman kaana kufir

Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.

Aya 15

وَلَقَد تَّرَكْنَٰهَآ ءَايَةًۭ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ

Wa laqat taraknaahaad aayatan fahal mim muddakir

Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?

Aya 16

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ

Fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur

Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.

Aya 17

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ

Wa laqad yassamal Quraana liz zikri fahal mimmuddakir

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?

Aya 18

كَذَّبَتْ عَادٌۭ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ

Kazzabat 'Aadun fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur

Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

Aya 19

إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًۭا صَرْصَرًۭا فِى يَوْمِ نَحْسٍۢ مُّسْتَمِرٍّۢ

Innaa arsalnaa 'alaihim reehan sarsaran fee Yawmi nahsim mustamirr

Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,

Aya 20

تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍۢ مُّنقَعِرٍۢ

Tanzi;un naasa ka anna huma'jaazu nakhlim munqa'ir

Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.

Aya 21

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ

'Fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

Aya 22

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ

Wa laqad yassamal Quraana liz zikri fahal mim muddakir

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?

Aya 23

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ

Kazzabat Samoodu binnuzur

Thamudi waliwakanusha Waonyaji.

Aya 24

فَقَالُوٓا۟ أَبَشَرًۭا مِّنَّا وَٰحِدًۭا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذًۭا لَّفِى ضَلَٰلٍۢ وَسُعُرٍ

Faqaalooo a-basharam minnaa waahidan nattabi'uhooo innaa izal lafee dalaalinw wa su'ur

Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!

Aya 25

أَءُلْقِىَ ٱلذِّكْرُ عَلَيْهِ مِنۢ بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌۭ

'A-ulqiyaz zikru 'alaihi mim baininaa bal huwa kazzaabun ashir

Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!

Aya 26

سَيَعْلَمُونَ غَدًۭا مَّنِ ٱلْكَذَّابُ ٱلْأَشِرُ

Sa-ya'lamoona ghadam manil kazzaabul ashir

Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.

Aya 27

إِنَّا مُرْسِلُوا۟ ٱلنَّاقَةِ فِتْنَةًۭ لَّهُمْ فَٱرْتَقِبْهُمْ وَٱصْطَبِرْ

Innaa mursilun naaqati fitnatal lahum fartaqibhum wastabir

Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.

Aya 28

وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ ٱلْمَآءَ قِسْمَةٌۢ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍۢ مُّحْتَضَرٌۭ

Wa nabbi'hum annal maaa'a qismatum bainahum kullu shirbim muhtadar

Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.

Aya 29

فَنَادَوْا۟ صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Fanaadaw saahibahum fata'aataa fa'aqar

Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.

Aya 30

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ

Fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!

Aya 31

إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةًۭ وَٰحِدَةًۭ فَكَانُوا۟ كَهَشِيمِ ٱلْمُحْتَظِرِ

Innaaa arsalnaa 'alaihim saihatanw waahidatan fakaano kahasheemil muhtazir

Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.

Aya 32

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ

Wa laqad yassarnal quraana liz zikri fahal mim muddakir

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?

Aya 33

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍۭ بِٱلنُّذُرِ

Kazzabat qawmu lootim binnuzur

Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.

Aya 34

إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٍۢ ۖ نَّجَّيْنَٰهُم بِسَحَرٍۢ

Innaa arsalnaa 'alaihim haasiban illaaa aala Loot najjainaahum bisahar

Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.

Aya 35

نِّعْمَةًۭ مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِى مَن شَكَرَ

Ni'matam min 'indinaa; kazaalika najzee man shakar

Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.

Aya 36

وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا۟ بِٱلنُّذُرِ

Wa laqad anzarahum batshatanaa fatamaaraw binnuzur

Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.

Aya 37

وَلَقَدْ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِۦ فَطَمَسْنَآ أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ

Wa laqad raawadoohu 'andaifee fatamasnaaa a'yunahum fazooqoo 'azaabee wa nuzur

Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!

Aya 38

وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌۭ مُّسْتَقِرٌّۭ

Wa laqad sabbahahum bukratan 'azaabum mustaqirr

Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.

Aya 39

فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ

Fazooqoo 'azaabee wa nuzur

Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!

Aya 40

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ

Wa laqad yassarnal Quraana liz zikri fahal mim muddakir

Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?

Aya 41

وَلَقَدْ جَآءَ ءَالَ فِرْعَوْنَ ٱلنُّذُرُ

Wa laqad jaaa'a Aala Fir'awnan nuzur

Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.

Aya 42

كَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَٰهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍۢ مُّقْتَدِرٍ

Kazzaboo bi Aayaatinaa kullihaa fa akhaznaahum akhza 'azeezim muqtadir

Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.

Aya 43

أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌۭ مِّنْ أُو۟لَٰٓئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَآءَةٌۭ فِى ٱلزُّبُرِ

Akuffaarukum khairum min ulaaa'ikum am lakum baraaa'atun fiz Zubur

Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?

Aya 44

أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌۭ مُّنتَصِرٌۭ

Am yaqooloona nahnu jamee'um muntasir

Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.

Aya 45

سَيُهْزَمُ ٱلْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ

Sa yuhzamul jam'u wa yuwalloonad dubur

Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.

Aya 46

بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَٱلسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ

Balis Saa'atu maw'iduhum was Saa'atu adhaa wa amarr

Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.

Aya 47

إِنَّ ٱلْمُجْرِمِينَ فِى ضَلَٰلٍۢ وَسُعُرٍۢ

Innal mujrimeena fee dalaalinw wa su'ur

Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.

Aya 48

يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِى ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا۟ مَسَّ سَقَرَ

Yawma yushaboona fin Naari'alaa wujoohimim zooqoo massa saqar

Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!

Aya 49

إِنَّا كُلَّ شَىْءٍ خَلَقْنَٰهُ بِقَدَرٍۢ

Innaa kulla shai'in khalaqnaahu biqadar

Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.

Aya 50

وَمَآ أَمْرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٌۭ كَلَمْحٍۭ بِٱلْبَصَرِ

Wa maaa amrunaaa illaa waahidatun kalamhim bilbasar

Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.

Aya 51

وَلَقَدْ أَهْلَكْنَآ أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ

Wa laqad ahlaknaaa ashyaa'akum fahal mim muddakir

Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?

Aya 52

وَكُلُّ شَىْءٍۢ فَعَلُوهُ فِى ٱلزُّبُرِ

Wa kullu shai'in fa'aloohu fiz Zubur

Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.

Aya 53

وَكُلُّ صَغِيرٍۢ وَكَبِيرٍۢ مُّسْتَطَرٌ

Wa kullu sagheerinw wa kabeerim mustatar

Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.

Aya 54

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍۢ وَنَهَرٍۢ

Innal muttaqeena fee jannaatinw wa nahar

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.

Aya 55

فِى مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍۢ مُّقْتَدِرٍۭ

Fee maq'adi sidqin 'inda Maleekim Muqtadir

Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.