Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Alaq
96

Al-Alaq — Pande la Damu

العَلَقِ
Za Makka Aya 19
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ

Iqra bismi rab bikal lazee khalaq

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

Aya 2

خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ مِنْ عَلَقٍ

Khalaqal insaana min 'alaq

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

Aya 3

ٱقْرَأْ وَرَبُّكَ ٱلْأَكْرَمُ

Iqra wa rab bukal akram

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

Aya 4

ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلْقَلَمِ

Al lazee 'allama bil qalam

Ambaye amefundisha kwa kalamu.

Aya 5

عَلَّمَ ٱلْإِنسَٰنَ مَا لَمْ يَعْلَمْ

'Al lamal insaana ma lam y'alam

Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

Aya 6

كَلَّآ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَيَطْغَىٰٓ

Kallaa innal insaana layatghaa

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri

Aya 7

أَن رَّءَاهُ ٱسْتَغْنَىٰٓ

Ar-ra aahus taghnaa

Akijiona katajirika.

Aya 8

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجْعَىٰٓ

Innna ilaa rabbikar ruj'aa

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

Aya 9

أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ

Ara-aital lazee yanhaa

Umemwona yule anaye mkataza

Aya 10

عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰٓ

'Abdan iza sallaa

Mja anapo sali?

Aya 11

أَرَءَيْتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلْهُدَىٰٓ

Ara-aita in kana 'alal hudaa

Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

Aya 12

أَوْ أَمَرَ بِٱلتَّقْوَىٰٓ

Au amara bit taqwaa

Au anaamrisha uchamngu?

Aya 13

أَرَءَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ

Ara-aita in kaz zaba wa ta walla

Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

Aya 14

أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ

Alam y'alam bi-an nal lahaa yaraa

Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

Aya 15

كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًۢا بِٱلنَّاصِيَةِ

Kalla la illam yantahi la nasfa'am bin nasiyah

Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

Aya 16

نَاصِيَةٍۢ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٍۢ

Nasiyatin kazi batin khaatiyah

Shungi la uwongo, lenye makosa!

Aya 17

فَلْيَدْعُ نَادِيَهُۥ

Fal yad'u naadiyah

Basi na awaite wenzake!

Aya 18

سَنَدْعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

Sanad 'uz zabaaniyah

Nasi tutawaita Mazabania!

Aya 19

كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَٱسْجُدْ وَٱقْتَرِب ۩

Kalla; la tuti'hu wasjud waqtarib

Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!