Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Qiyama
75

Al-Qiyama — Kiyama

القِيَامَةِ
Za Makka Aya 40
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ

Laaa uqsimu bi yawmil qiyaamah

Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

Aya 2

وَلَآ أُقْسِمُ بِٱلنَّفْسِ ٱللَّوَّامَةِ

Wa laaa uqsimu bin nafsil lawwaamah

Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

Aya 3

أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُۥ

Ayahsabul insaanu al lan najm'a 'izaamah

Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

Aya 4

بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّىَ بَنَانَهُۥ

Balaa qaadireena 'alaaa an nusawwiya banaanah

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

Aya 5

بَلْ يُرِيدُ ٱلْإِنسَٰنُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُۥ

Bal yureedul insaanu liyafjura amaamah

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

Aya 6

يَسْـَٔلُ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلْقِيَٰمَةِ

Yas'alu ayyyaana yawmul qiyaamah

Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

Aya 7

فَإِذَا بَرِقَ ٱلْبَصَرُ

Fa izaa bariqal basar

Basi jicho litapo dawaa,

Aya 8

وَخَسَفَ ٱلْقَمَرُ

We khasafal qamar

Na mwezi utapo patwa,

Aya 9

وَجُمِعَ ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ

Wa jumi'ash shamusu wal qamar

Na likakusanywa jua na mwezi,

Aya 10

يَقُولُ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ ٱلْمَفَرُّ

Yaqoolul insaanu yaw ma 'izin aynal mafarr

Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

Aya 11

كَلَّا لَا وَزَرَ

Kallaa laa wazar

La! Hapana pa kukimbilia!

Aya 12

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمُسْتَقَرُّ

Ilaa rabbika yawma 'izinil mustaqarr

Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

Aya 13

يُنَبَّؤُا۟ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ

Yunabba 'ul insaanu yawma 'izim bimaa qaddama wa akhkhar

Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

Aya 14

بَلِ ٱلْإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفْسِهِۦ بَصِيرَةٌۭ

Balil insaanu 'alaa nafsihee baseerah

Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

Aya 15

وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ

Wa law alqaa ma'aazeerah

Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

Aya 16

لَا تُحَرِّكْ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِۦٓ

Laa tuharrik bihee lisaa naka lita'jala bih

Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

Aya 17

إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُۥ وَقُرْءَانَهُۥ

Inna 'alainaa jam'ahoo wa qur aanah

Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

Aya 18

فَإِذَا قَرَأْنَٰهُ فَٱتَّبِعْ قُرْءَانَهُۥ

Fa izaa qaraanaahu fattabi' qur aanah

Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

Aya 19

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُۥ

Summa inna 'alainaa bayaanah

Kisha ni juu yetu kuubainisha.

Aya 20

كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ

Kallaa bal tuhibboonal 'aajilah

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

Aya 21

وَتَذَرُونَ ٱلْءَاخِرَةَ

Wa tazaroonal Aakhirah

Na mnaacha maisha ya Akhera.

Aya 22

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاضِرَةٌ

Wujoohuny yawma 'izin naadirah

Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

Aya 23

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌۭ

Ilaa rabbihaa naazirah

Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

Aya 24

وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۭ بَاسِرَةٌۭ

Wa wujoohuny yawma 'izim baasirah

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

Aya 25

تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌۭ

Tazunnu any yuf'ala bihaa faaqirah

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

Aya 26

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ

Kallaaa izaa balaghatit taraaqee

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

Aya 27

وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍۢ

Wa qeela man raaq

Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

Aya 28

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلْفِرَاقُ

Wa zanna annahul firaaq

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

Aya 29

وَٱلْتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

Waltaffatis saaqu bissaaq

Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

Aya 30

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمَسَاقُ

Ilaa rabbika yawma'izinil masaaq

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

Aya 31

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Falaa saddaqa wa laa sallaa

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

Aya 32

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Wa laakin kazzaba wa tawalla

Bali alikanusha, na akageuka.

Aya 33

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

Summa zahaba ilaaa ahlihee yatamatta

Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

Aya 34

أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ

Awlaa laka fa awlaa

Ole wako, ole wako!

Aya 35

ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰٓ

Summa awlaa laka fa awla

Kisha Ole wako, ole wako!

Aya 36

أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَن يُتْرَكَ سُدًى

Ayahsabul insaanu anyytraka sudaa

Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

Aya 37

أَلَمْ يَكُ نُطْفَةًۭ مِّن مَّنِىٍّۢ يُمْنَىٰ

Alam yaku nutfatam mim maniyyiny yumnaa

Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

Aya 38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةًۭ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Summa kaana 'alaqata fakhalaq fasawwaa

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

Aya 39

فَجَعَلَ مِنْهُ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ

Faja'ala minhuz zawjayniz zakara wal unsaa

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

Aya 40

أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحْۦِىَ ٱلْمَوْتَىٰ

Alaisa zaalika biqaadirin 'alaaa any yuhyiyal mawtaa

Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?