Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Muddathir
74

Al-Muddathir — Aliyejifunika

المُدَّثِّرِ
Za Makka Aya 56
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

يَٰٓأَيُّهَا ٱلْمُدَّثِّرُ

Yaaa ayyuhal muddassir

Ewe uliye jigubika!

Aya 2

قُمْ فَأَنذِرْ

Qum fa anzir

Simama uonye!

Aya 3

وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ

Wa rabbaka fakabbir

Na Mola wako Mlezi mtukuze!

Aya 4

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ

Wa siyaabaka fatahhir

Na nguo zako, zisafishe.

Aya 5

وَٱلرُّجْزَ فَٱهْجُرْ

Warrujza fahjur

Na yaliyo machafu yahame!

Aya 6

وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ

Wa laa tamnun tastaksir

Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.

Aya 7

وَلِرَبِّكَ فَٱصْبِرْ

Wa li Rabbika fasbir

Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!

Aya 8

فَإِذَا نُقِرَ فِى ٱلنَّاقُورِ

Fa izaa nuqira fin naaqoor

Basi litapo pulizwa barugumu,

Aya 9

فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍۢ يَوْمٌ عَسِيرٌ

Fazaalika yawma 'iziny yawmun 'aseer

Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.

Aya 10

عَلَى ٱلْكَٰفِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍۢ

'Alal kaafireena ghayru yaseer

Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

Aya 11

ذَرْنِى وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًۭا

Zamee wa man khalaqtu waheedaa

Niache peke yangu na niliye muumba;

Aya 12

وَجَعَلْتُ لَهُۥ مَالًۭا مَّمْدُودًۭا

Wa ja'altu lahoo maalam mamdoodaa

Na nikamjaalia awe na mali mengi,

Aya 13

وَبَنِينَ شُهُودًۭا

Wa baneena shuhoodaa

Na wana wanao onekana,

Aya 14

وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمْهِيدًۭا

Wa mahhattu lahoo tamheeda

Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.

Aya 15

ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ

Summa yat ma'u an azeed

Kisha anatumai nimzidishie!

Aya 16

كَلَّآ ۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِءَايَٰتِنَا عَنِيدًۭا

Kallaaa innahoo kaana li Aayaatinaa 'aneedaa

Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!

Aya 17

سَأُرْهِقُهُۥ صَعُودًا

Sa urhiquhoo sa'oodaa

Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.

Aya 18

إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ

Innahoo fakkara wa qaddar

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.

Aya 19

فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ

Faqutila kayfa qaddar

Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!

Aya 20

ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ

Summa qutila kaifa qaddar

Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!

Aya 21

ثُمَّ نَظَرَ

Summa nazar

Kisha akatazama,

Aya 22

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ

Summa 'abasa wa basar

Kisha akakunja kipaji, na akanuna.

Aya 23

ثُمَّ أَدْبَرَ وَٱسْتَكْبَرَ

Summaa adbara wastakbar

Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.

Aya 24

فَقَالَ إِنْ هَٰذَآ إِلَّا سِحْرٌۭ يُؤْثَرُ

Faqaala in haazaaa illaa sihruny yu'sar

Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.

Aya 25

إِنْ هَٰذَآ إِلَّا قَوْلُ ٱلْبَشَرِ

In haazaaa illaa qawlul bashar

Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.

Aya 26

سَأُصْلِيهِ سَقَرَ

Sa usleehi saqar

Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.

Aya 27

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Wa maaa adraaka maa saqar

Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?

Aya 28

لَا تُبْقِى وَلَا تَذَرُ

Laa tubqee wa laa tazar

Haubakishi wala hausazi.

Aya 29

لَوَّاحَةٌۭ لِّلْبَشَرِ

Lawwaahatul lilbashar

Unababua ngozi iwe nyeusi.

Aya 30

عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ

'Alaihaa tis'ata 'ashar

Juu yake wapo kumi na tisa.

Aya 31

وَمَا جَعَلْنَآ أَصْحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةًۭ ۙ وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةًۭ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لِيَسْتَيْقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَٰبَ وَيَزْدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓا۟ إِيمَٰنًۭا ۙ وَلَا يَرْتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَٰبَ وَٱلْمُؤْمِنُونَ ۙ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِى قُلُوبِهِم مَّرَضٌۭ وَٱلْكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلًۭا ۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهْدِى مَن يَشَآءُ ۚ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ۚ وَمَا هِىَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ

Wa maaja''alnaaa As haaban naari illaa malaaa 'ikatanw wa maa ja'alnaa 'iddatahum illaa fitnatal lillazeena kafaroo liyastayqinal lazeena ootul kitaaba wa yazdaadal lazeena aamanooo eemaananw wa laa yartaabal lazeena ootul kitaaba walmu'minoona wa liyaqoolal lazeena fee quloo bihim maradunw walkaafiroona maazaaa araadal laahu bihaazaa masalaa; kazaalika yudillul laahu many yashaaa'u wa yahdee many yashaaa'; wa maa ya'lamu junooda rabbika illaa hoo; wa maa hiya illaa zikraa lil bashar

Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.

Aya 32

كَلَّا وَٱلْقَمَرِ

Kallaa walqamar

Hasha! Naapa kwa mwezi!

Aya 33

وَٱلَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ

Wallaili adbar

Na kwa usiku unapo kucha!

Aya 34

وَٱلصُّبْحِ إِذَآ أَسْفَرَ

Wassub hi izaaa asfar

Na kwa asubuhi inapo pambazuka!

Aya 35

إِنَّهَا لَإِحْدَى ٱلْكُبَرِ

Innahaa la ihdal kubar

Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!

Aya 36

نَذِيرًۭا لِّلْبَشَرِ

Nazeeral lilbashar

Ni onyo kwa binaadamu,

Aya 37

لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ

Liman shaaa'a minkum any yataqaddama aw yata akhkhar

Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.

Aya 38

كُلُّ نَفْسٍۭ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ

Kullu nafsim bim kasabat raheenah

Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.

Aya 39

إِلَّآ أَصْحَٰبَ ٱلْيَمِينِ

Illaaa as haabal yameen

Isipo kuwa watu wa kuliani.

Aya 40

فِى جَنَّٰتٍۢ يَتَسَآءَلُونَ

Fee jannaatiny yata saaa'aloon

Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana

Aya 41

عَنِ ٱلْمُجْرِمِينَ

'Anil mujrimeen

Khabari za wakosefu:

Aya 42

مَا سَلَكَكُمْ فِى سَقَرَ

Maa salakakum fee saqar

Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?

Aya 43

قَالُوا۟ لَمْ نَكُ مِنَ ٱلْمُصَلِّينَ

Qaaloo lam naku minal musalleen

Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.

Aya 44

وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ ٱلْمِسْكِينَ

Wa lam naku nut'imul miskeen

Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

Aya 45

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلْخَآئِضِينَ

Wa kunnaa nakhoodu ma'al khaaa'ideen

Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.

Aya 46

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

Wa kunnaa nukazzibu bi yawmid Deen

Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.

Aya 47

حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلْيَقِينُ

Hattaaa ataanal yaqeen

Mpaka yakini ilipo tufikia.

Aya 48

فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ

Famaa tanfa'uhum shafaa'atush shaafi'een

Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.

Aya 49

فَمَا لَهُمْ عَنِ ٱلتَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ

Famaa lahum 'anittazkirati mu'rideen

Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?

Aya 50

كَأَنَّهُمْ حُمُرٌۭ مُّسْتَنفِرَةٌۭ

Ka annahum humurum mustanfirah

Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,

Aya 51

فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍۭ

Farrat min qaswarah

Wanao mkimbia simba!

Aya 52

بَلْ يُرِيدُ كُلُّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًۭا مُّنَشَّرَةًۭ

Bal yureedu kullum ri'im minhum any yu'taa suhufam munashsharah

Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.

Aya 53

كَلَّا ۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلْءَاخِرَةَ

Kallaa bal laa yakhaafoonal aakhirah

Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?

Aya 54

كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذْكِرَةٌۭ

Kallaaa innahoo tazkirah

Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!

Aya 55

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Fa man shaaa'a zakarah

Basi anaye taka atakumbuka.

Aya 56

وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ ۚ هُوَ أَهْلُ ٱلتَّقْوَىٰ وَأَهْلُ ٱلْمَغْفِرَةِ

Wa maa yazkuroona illaaa any yashaaa'al laah; Huwa ahlut taqwaa wa ahlul maghfirah

Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.