Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Waqi'a
56

Al-Waqi'a — Tukio

الوَاقِعَةِ
Za Makka Aya 96
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ

Izaa waqa'atil waaqi'ah

Litakapo tukia hilo Tukio

Aya 2

لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Laisa liwaq'atihaa kaazibah

Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

Aya 3

خَافِضَةٌۭ رَّافِعَةٌ

Khafidatur raafi'ah

Literemshalo linyanyualo,

Aya 4

إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّۭا

Izaa rujjatil ardu rajjaa

Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

Aya 5

وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّۭا

Wa bussatil jibaalu bassaa

Na milima itapo sagwasagwa,

Aya 6

فَكَانَتْ هَبَآءًۭ مُّنۢبَثًّۭا

Fakaanat habaaa'am mumbassaa

Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

Aya 7

وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًۭا ثَلَٰثَةًۭ

Wa kuntum azwaajan salaasah

Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

Aya 8

فَأَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ

Fa as haabul maimanati maaa as haabul maimanah

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

Aya 9

وَأَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ

Wa as haabul mash'amati maaa as haabul mash'amah

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

Aya 10

وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ

Wassaabiqoonas saabiqoon

Na wa mbele watakuwa mbele.

Aya 11

أُو۟لَٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ

Ulaaa'ikal muqarraboon

Hao ndio watakao karibishwa

Aya 12

فِى جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Fee Jannaatin Na'eem

Katika Bustani zenye neema.

Aya 13

ثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ

Sullatum minal awwaleen

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

Aya 14

وَقَلِيلٌۭ مِّنَ ٱلْءَاخِرِينَ

Wa qaleelum minal aa khireen

Na wachache katika wa mwisho.

Aya 15

عَلَىٰ سُرُرٍۢ مَّوْضُونَةٍۢ

'Alaa sururim mawdoonah

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

Aya 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَٰبِلِينَ

Muttaki'eena 'alaihaa mutaqabileen

Wakiviegemea wakielekeana.

Aya 17

يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌۭ مُّخَلَّدُونَ

Yatoofu 'alaihim wildaa num mukkhalladoon

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

Aya 18

بِأَكْوَابٍۢ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍۢ مِّن مَّعِينٍۢ

Bi akwaabinw wa abaareeq, wa kaasim mim ma'een

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

Aya 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Laa yusadda'oona 'anhaa wa laa yunzifoon

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

Aya 20

وَفَٰكِهَةٍۢ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Wa faakihatim mimmaa yatakhaiyaroon

Na matunda wayapendayo,

Aya 21

وَلَحْمِ طَيْرٍۢ مِّمَّا يَشْتَهُونَ

Wa lahmi tairim mimmaa yashtahoon

Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

Aya 22

وَحُورٌ عِينٌۭ

Wa hoorun'een

Na Mahurulaini,

Aya 23

كَأَمْثَٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ

Ka amsaalil lu'lu'il maknoon

Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

Aya 24

جَزَآءًۢ بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ

Jazaaa'am bimaa kaanoo ya'maloon

Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

Aya 25

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًۭا وَلَا تَأْثِيمًا

Laa yasma'oona feehaa laghwanw wa laa taaseemaa

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

Aya 26

إِلَّا قِيلًۭا سَلَٰمًۭا سَلَٰمًۭا

Illaa qeelan salaaman salaamaa

Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

Aya 27

وَأَصْحَٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْيَمِينِ

Wa as haabul yameeni maaa as haabul Yameen

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

Aya 28

فِى سِدْرٍۢ مَّخْضُودٍۢ

Fee sidrim makhdood

Katika mikunazi isiyo na miba,

Aya 29

وَطَلْحٍۢ مَّنضُودٍۢ

Wa talhim mandood

Na migomba iliyo pangiliwa,

Aya 30

وَظِلٍّۢ مَّمْدُودٍۢ

Wa zillim mamdood

Na kivuli kilicho tanda,

Aya 31

وَمَآءٍۢ مَّسْكُوبٍۢ

Wa maaa'im maskoob

Na maji yanayo miminika,

Aya 32

وَفَٰكِهَةٍۢ كَثِيرَةٍۢ

Wa faakihatin kaseerah

Na matunda mengi,

Aya 33

لَّا مَقْطُوعَةٍۢ وَلَا مَمْنُوعَةٍۢ

Laa maqtoo'atinw wa laa mamnoo'ah

Hayatindikii wala hayakatazwi,

Aya 34

وَفُرُشٍۢ مَّرْفُوعَةٍ

Wa furushim marfoo'ah

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

Aya 35

إِنَّآ أَنشَأْنَٰهُنَّ إِنشَآءًۭ

Innaaa anshaanaahunna inshaaa'aa

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

Aya 36

فَجَعَلْنَٰهُنَّ أَبْكَارًا

Faja'alnaahunna abkaaraa

Na tutawafanya vijana,

Aya 37

عُرُبًا أَتْرَابًۭا

'Uruban atraabaa

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

Aya 38

لِّأَصْحَٰبِ ٱلْيَمِينِ

Li as haabil yameen

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

Aya 39

ثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ

Sullatum minal awwa leen

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

Aya 40

وَثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْءَاخِرِينَ

Wa sullatum minal aakhireen

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

Aya 41

وَأَصْحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Wa as haabush shimaali maaa as haabush shimaal

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

Aya 42

فِى سَمُومٍۢ وَحَمِيمٍۢ

Fee samoominw wa hameem

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

Aya 43

وَظِلٍّۢ مِّن يَحْمُومٍۢ

Wa zillim miny yahmoom

Na kivuli cha moshi mweusi,

Aya 44

لَّا بَارِدٍۢ وَلَا كَرِيمٍ

Laa baaridinw wa laa kareem

Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

Aya 45

إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ

Innaahum kaanoo qabla zaalika mutrafeen

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

Aya 46

وَكَانُوا۟ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ

Wa kaanoo yusirroona 'alal hinsil 'azeem

Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

Aya 47

وَكَانُوا۟ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًۭا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ

Wa kaanoo yaqooloona a'izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa izaaman'ainnaa lamab'oosoon

Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

Aya 48

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ

Awa aabaaa'unal awwaloon

Au baba zetu wa zamani?

Aya 49

قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْءَاخِرِينَ

Qul innal awwaleena wal aakhireen

Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

Aya 50

لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوْمٍۢ مَّعْلُومٍۢ

Lamajmoo'oona ilaa meeqaati yawmim ma'loon

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

Aya 51

ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلْمُكَذِّبُونَ

summa innakum ayyuhad daaalloonal mukazziboon

Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

Aya 52

لَءَاكِلُونَ مِن شَجَرٍۢ مِّن زَقُّومٍۢ

La aakiloona min shaja rim min zaqqoom

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

Aya 53

فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ

Famaali'oona minhal butoon

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

Aya 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ ٱلْحَمِيمِ

Fashaariboona 'alaihi minal hameem

Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

Aya 55

فَشَٰرِبُونَ شُرْبَ ٱلْهِيمِ

Fashaariboona shurbal heem

Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

Aya 56

هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ ٱلدِّينِ

Haazaa nuzuluhum yawmad deen

Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

Aya 57

نَحْنُ خَلَقْنَٰكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ

Nahnu khalaqnaakum falaw laa tusaddiqoon

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

Aya 58

أَفَرَءَيْتُم مَّا تُمْنُونَ

Afara'aytum maa tumnoon

Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

Aya 59

ءَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلْخَٰلِقُونَ

'A-antum takhluqoo nahooo am nahnul khaaliqoon

Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

Aya 60

نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ ٱلْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ

Nahnu qaddarnaa baina kumul mawta wa maa nahnu bimasbooqeen

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

Aya 61

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَٰلَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِى مَا لَا تَعْلَمُونَ

'Alaaa an nubaddila amsaalakum wa nunshi'akum fee maa laa ta'lamoon

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

Aya 62

وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ

Wa laqad 'alimtumun nash atal oolaa falaw laa tazakkaroon

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

Aya 63

أَفَرَءَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ

Afara'aytum maa tahrusoon

Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

Aya 64

ءَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلزَّٰرِعُونَ

'A-antum tazra'oonahooo am nahnuz zaari'ooon

Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

Aya 65

لَوْ نَشَآءُ لَجَعَلْنَٰهُ حُطَٰمًۭا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ

Law nashaaa'u laja'al naahu hutaaman fazaltum tafakkahoon

Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

Aya 66

إِنَّا لَمُغْرَمُونَ

Innaa lamughramoon

Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

Aya 67

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ

Bal nahnu mahroomoon

Bali sisi tumenyimwa.

Aya 68

أَفَرَءَيْتُمُ ٱلْمَآءَ ٱلَّذِى تَشْرَبُونَ

Afara'aytumul maaa'allazee tashraboon

Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

Aya 69

ءَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ ٱلْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنزِلُونَ

'A-antum anzaltumoohu minal muzni am nahnul munziloon

Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

Aya 70

لَوْ نَشَآءُ جَعَلْنَٰهُ أُجَاجًۭا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ

Law nashaaa'u ja'alnaahu ujaajan falaw laa tashkuroon

Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

Aya 71

أَفَرَءَيْتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِى تُورُونَ

Afara'aytumun naaral latee tooroon

Je! Mnauona moto mnao uwasha?

Aya 72

ءَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَآ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنشِـُٔونَ

'A-antum anshaatum shajaratahaaa am nahnul munshi'oon

Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

Aya 73

نَحْنُ جَعَلْنَٰهَا تَذْكِرَةًۭ وَمَتَٰعًۭا لِّلْمُقْوِينَ

Nahnu ja'alnaahaa tazkira tanw wa mataa'al lilmuqween

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

Aya 74

فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ

Fasabbih bismi Rabbikal 'azeem

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

Aya 75

۞ فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Falaa uqsimu bimaawaa qi'innujoom

Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

Aya 76

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٌۭ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ

Wa innahoo laqasamul lawta'lamoona'azeem

Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

Aya 77

إِنَّهُۥ لَقُرْءَانٌۭ كَرِيمٌۭ

Innahoo la quraanun kareem

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

Aya 78

فِى كِتَٰبٍۢ مَّكْنُونٍۢ

Fee kitaabim maknoon

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

Aya 79

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلْمُطَهَّرُونَ

Laa yamassuhooo illal mutahharoon

Hapana akigusaye ila walio takaswa.

Aya 80

تَنزِيلٌۭ مِّن رَّبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Tanzeelum mir Rabbil'aalameen

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Aya 81

أَفَبِهَٰذَا ٱلْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ

Afabihaazal hadeesi antum mudhinoon

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

Aya 82

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ

Wa taj'aloona rizqakum annakum tukazziboon

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

Aya 83

فَلَوْلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلْحُلْقُومَ

Falaw laaa izaa balaghatil hulqoom

Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

Aya 84

وَأَنتُمْ حِينَئِذٍۢ تَنظُرُونَ

Wa antum heena'izin tanzuroon

Na nyinyi wakati huo mnatazama!

Aya 85

وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ

Wa nahnu aqrabu ilaihi minkum wa laakil laa tubsiroon

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

Aya 86

فَلَوْلَآ إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ

Falaw laaa in kuntum ghira madeeneen

Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

Aya 87

تَرْجِعُونَهَآ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ

Tarji'oonahaaa in kuntum saadiqeen

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

Aya 88

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ

Fa ammaaa in kaana minal muqarrabeen

Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

Aya 89

فَرَوْحٌۭ وَرَيْحَانٌۭ وَجَنَّتُ نَعِيمٍۢ

Farawhunw wa raihaa nunw wa jannatu na'eem

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

Aya 90

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنْ أَصْحَٰبِ ٱلْيَمِينِ

Wa ammaaa in kaana min as haabil yameen

Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

Aya 91

فَسَلَٰمٌۭ لَّكَ مِنْ أَصْحَٰبِ ٱلْيَمِينِ

Fasalaamul laka min as haabil yameen

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

Aya 92

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ

Wa ammaaa in kaana minal mukazzibeenad daaalleen

Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

Aya 93

فَنُزُلٌۭ مِّنْ حَمِيمٍۢ

Fanuzulum min hameem

Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

Aya 94

وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ

Wa tasliyatu jaheem

Na kutiwa Motoni.

Aya 95

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلْيَقِينِ

Inna haaza lahuwa haqqul yaqeen

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

Aya 96

فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ

Fasabbih bismi rabbikal 'azeem

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.