Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / As-Saffat
37

As-Saffat — Wanaojipanga Safu

الصَّافَّاتِ
Za Makka Aya 182
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفًّۭا

Wassaaaffaati saffaa

Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.

Aya 2

فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًۭا

Fazzaajiraati zajraa

Na kwa wenye kukataza mabaya.

Aya 3

فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكْرًا

Fattaaliyaati Zikra

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

Aya 4

إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌۭ

Inna Illaahakum la Waahid

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

Aya 5

رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَٰرِقِ

Rabbus samaawaati wal ardi wa maa bainahumaa wa Rabbul mashaariq

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

Aya 6

إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ

Innaa zaiyannas samaaa 'ad dunyaa bizeenatinil kawaakib

Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.

Aya 7

وَحِفْظًۭا مِّن كُلِّ شَيْطَٰنٍۢ مَّارِدٍۢ

Wa hifzam min kulli Shaitaanim maarid

Na kulinda na kila shet'ani a'si.

Aya 8

لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍۢ

Laa yassamma 'oona ilal mala il a'alaa wa yuqzafoona min kulli jaanib

Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

Aya 9

دُحُورًۭا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌۭ وَاصِبٌ

Duhooranw wa lahum 'azaabunw waasib

Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

Aya 10

إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌۭ ثَاقِبٌۭ

Illaa man khatifal khatfata fa atba'ahoo shihaabun saaqib

Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.

Aya 11

فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّن طِينٍۢ لَّازِبٍۭ

Fastaftihim ahum ashaddu khalqan am man khalaqnaa; innaa khalaqnaahum min teenil laazib

Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.

Aya 12

بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ

Bal'ajibta wa yaskharoon

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

Aya 13

وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ

Wa izaa zukkiroo laa yazkuroon

Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.

Aya 14

وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةًۭ يَسْتَسْخِرُونَ

Wa izaa ra aw Aayatinw yastaskhiroon

Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.

Aya 15

وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَٰذَآ إِلَّا سِحْرٌۭ مُّبِينٌ

Wa qaalooo in haazaa illaa sihrum mubeen

Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.

Aya 16

أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًۭا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ

'A-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa 'izaaman 'ainnaa lamab'oosoon

Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

Aya 17

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ

Awa aabaa'unal awwaloon

Hata baba zetu wa zamani?

Aya 18

قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ

Qul na'am wa antum daakhiroon

Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.

Aya 19

فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ

Fa innamaa hiya zajra tunw waahidatun fa izaa hum yanzuroon

Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!

Aya 20

وَقَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ

Qa qaaloo yaa wailanaa haazaa Yawmud-Deen

Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

Aya 21

هَٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Haazaa Yawmul Faslil lazee kuntum bihee tukaziboon

Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.

Aya 22

۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ

Uhshurul lazeena zalamoo wa azwaajahum wa maa kaanoo ya'budoon

Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -

Aya 23

مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ

Min doonil laahi fahdoohum ilaa siraatil Jaheem

Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

Aya 24

وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ

Wa qifoohum innahum mas'ooloon

Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:

Aya 25

مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ

Maa lakum laa tanaasaroon

Mna nini? Mbona hamsaidiani?

Aya 26

بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ

Bal humul Yawma mustaslimoon

Bali hii leo, watasalimu amri.

Aya 27

وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَسَآءَلُونَ

Wa aqbala ba'duhum 'alaa ba'diny yatasaaa'aloon

Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.

Aya 28

قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ

Qaalooo innakum kuntum taatoonanaa 'anil yameen

Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.

Aya 29

قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ

Qaaloo bal lam takoonoo mu'mineen

Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.

Aya 30

وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًۭا طَٰغِينَ

Wa maa kaana lanaa 'alaikum min sultaanim bal kuntum qawman taagheen

Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.

Aya 31

فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ

Fahaqqa 'alainaa qawlu Rabbinaaa innaa lazaaa'iqoon

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

Aya 32

فَأَغْوَيْنَٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ

Fa aghwainaakum innaa kunnaa ghaaween

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

Aya 33

فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍۢ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ

Fa innahum Yawma'izin fil'azaabi mushtarikoon

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.

Aya 34

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ

Innaa kazaalika naf'alu bil mujrimeen

Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.

Aya 35

إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ

Innahum kaanooo izaa qeela lahum laaa ilaaha illal laahu yastakbiroon

Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.

Aya 36

وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍۢ مَّجْنُونٍۭ

Wa yaqooloona a'innaa lataarikooo aalihatinaa lishaa'irim majnoon

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?

Aya 37

بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ

bal jaaa'a bilhaqqi wa saddaqal mursaleen

Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.

Aya 38

إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ

Innakum lazaaa'iqul 'azaabil aleem

Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.

Aya 39

وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Wa maa tujzawna illaa maa kuntum ta'maloon

Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.

Aya 40

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ

Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

Aya 41

أُو۟لَٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌۭ مَّعْلُومٌۭ

Ulaaa'ika lahum rizqum ma'loom

Hao ndio watakao pata riziki maalumu,

Aya 42

فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ

Fa waakihu wa hum mukramoon

Matunda, nao watahishimiwa.

Aya 43

فِى جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Fee jannaatin Na'eem

Katika Bustani za neema.

Aya 44

عَلَىٰ سُرُرٍۢ مُّتَقَٰبِلِينَ

'Alaa sururim mutaqaa bileen

Wako juu ya viti wamekabiliana.

Aya 45

يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍۢ مِّن مَّعِينٍۭ

Yutaafu 'alaihim bikaasim mim ma'een

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem

Aya 46

بَيْضَآءَ لَذَّةٍۢ لِّلشَّٰرِبِينَ

Baidaaa'a laz zatil lish shaaribeen

Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.

Aya 47

لَا فِيهَا غَوْلٌۭ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ

Laa feehaa ghawlunw wa laa hum 'anhaa yunzafoon

Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

Aya 48

وَعِندَهُمْ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌۭ

Wa 'indahum qaasiraatut tarfi 'een

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.

Aya 49

كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌۭ مَّكْنُونٌۭ

Ka annahunna baidum maknoon

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.

Aya 50

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَسَآءَلُونَ

Fa aqbala ba'duhum 'alaa badiny yatasaaa 'aloon

Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.

Aya 51

قَالَ قَآئِلٌۭ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌۭ

Qaala qaaa'ilum minhum innee kaana lee qareen

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki

Aya 52

يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ

Yaqoolu a'innnaka laminal musaddiqeen

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki

Aya 53

أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًۭا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ

'A-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa 'izaaman 'ainnaa lamadeenoon

Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?

Aya 54

قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ

Qaala hal antum muttali'oon

Atasema: Je! Nyie mnawaona?

Aya 55

فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ

Fattala'a fara aahu fee sawaaa'il Jaheem

Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.

Aya 56

قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ

Qaala tallaahi in kitta laturdeen

Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.

Aya 57

وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ

Wa law laa ni'matu Rabbee lakuntu minal muhdareen

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.

Aya 58

أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ

Afamaa nahnu bimaiyiteen

Je! Sisi hatutakufa,

Aya 59

إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ

Illa mawtatanal oola wa maa nahnu bimu'azzabeen

Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.

Aya 60

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ

Inna haazaa falya'ma lil'aamiloon

Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.

Aya 61

لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَٰمِلُونَ

Limisli haaza falya'ma lil 'aamiloon

Kwa mfano wa haya nawatende watendao.

Aya 62

أَذَٰلِكَ خَيْرٌۭ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ

Azaalika khairun nuzulan am shajaratuz Zaqqom

Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?

Aya 63

إِنَّا جَعَلْنَٰهَا فِتْنَةًۭ لِّلظَّٰلِمِينَ

Innaa ja'alnaahaa fitnatal lizzaalimeen

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.

Aya 64

إِنَّهَا شَجَرَةٌۭ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ

Innahaa shajaratun takhruju feee aslil Jaheem

Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.

Aya 65

طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ

Tal'uhaa ka annahoo ru'oosush Shayaateen

Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.

Aya 66

فَإِنَّهُمْ لَءَاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ

Fa innahum la aakiloona minhaa famaali'oona minhal butoon

Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.

Aya 67

ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًۭا مِّنْ حَمِيمٍۢ

Summa inna lahum 'alaihaa lashawbam min hameem

Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.

Aya 68

ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ

Summa inna marji'ahum la ilal Jaheem

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.

Aya 69

إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ

Innahum alfaw aabaaa'ahum daaalleen

Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.

Aya 70

فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ

Fahum 'alaa aasaarihim yuhra'oon

Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.

Aya 71

وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ

Wa laqad dalla qablahum aksarul awwaleen

Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.

Aya 72

وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ

Wa laqad arsalnaa feehim munzireen

Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.

Aya 73

فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ

Fanzur kaifa kaana 'aaqibatul munzareen

Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.

Aya 74

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ

Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

Aya 75

وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌۭ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ

Wa laqad naadaanaa Noohun falani'mal mujeeboon

Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.

Aya 76

وَنَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ

Wa jajainaahu wa ahlahoo minal karbil 'azeem

Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.

Aya 77

وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ

Wa ja'alnaa zurriyyatahoo hummul baaqeen

Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.

Aya 78

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْءَاخِرِينَ

Wa taraknaa 'alaihi fil aakhireen

Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.

Aya 79

سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍۢ فِى ٱلْعَٰلَمِينَ

Salaamun 'alaa Noohin fil 'aalameen

Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!

Aya 80

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ

Innaa kazaalika najzil muhsineen

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

Aya 81

إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ

Innahoo min 'ibaadinal mu'mineen

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

Aya 82

ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْءَاخَرِينَ

Summa aghraqnal aakhareen

Kisha tukawazamisha wale wengine.

Aya 83

۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ

Wa ina min shee'atihee la Ibraaheem

Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,

Aya 84

إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍۢ سَلِيمٍ

Iz jaaa'a Rabbahoo bi qalbin saleem

Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.

Aya 85

إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ

Iz qaala li abeehi wa qawmihee maazaa ta'budoon

Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?

Aya 86

أَئِفْكًا ءَالِهَةًۭ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ

A'ifkan aalihatan doonal laahi tureedoon

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?

Aya 87

فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Famaa zannukum bi Rabbil'aalameen

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Aya 88

فَنَظَرَ نَظْرَةًۭ فِى ٱلنُّجُومِ

Fanazara nazratan finnujoom

Kisha akapiga jicho kutazama nyota.

Aya 89

فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌۭ

Faqaala inee saqeem

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!

Aya 90

فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ

Fatawallaw 'anhu mudbireen

Nao wakamwacha, wakampa kisogo.

Aya 91

فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ

Faraagha ilaaa aalihatihim faqaala alaa taakuloon

Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?

Aya 92

مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ

Maa lakum laa tantiqoon

Mna nini hata hamsemi?

Aya 93

فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ

Faraagha 'alaihim darbam bilyameen

Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.

Aya 94

فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ

Fa aqbalooo ilaihi yaziffoon

Basi wakamjia upesi upesi.

Aya 95

قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ

Qaala ata'budoona maa tanhitoon

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?

Aya 96

وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ

Wallaahu khalaqakum wa maa ta'maloon

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!

Aya 97

قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَٰنًۭا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ

Qaalub noo lahoo bun yaanan fa alqoohu fil jaheem

Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!

Aya 98

فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًۭا فَجَعَلْنَٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ

Fa araadoo bihee kaidan faja 'alnaahumul asfaleen

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.

Aya 99

وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ

Wa qaala innee zaahibun ilaa Rabbee sa yahdeen

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

Aya 100

رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Rabbi hab lee minas saaliheen

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

Aya 101

فَبَشَّرْنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٍۢ

Fabashsharnaahu bighulaamin haleem

Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

Aya 102

فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ

Falamma balagha ma'a hus sa'ya qaala yaa buniya inneee araa fil manaami anneee azbahuka fanzur maazaa taraa; qaala yaaa abatif 'al maa tu'maru satajidunee in shaaa'allaahu minas saabireen

Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.

Aya 103

فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ

Falammaaa aslamaa wa tallahoo liljabeen

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

Aya 104

وَنَٰدَيْنَٰهُ أَن يَٰٓإِبْرَٰهِيمُ

Wa naadainaahu ai yaaaa Ibraheem

Tulimwita: Ewe Ibrahim!

Aya 105

قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ

Qad saddaqtar ru'yaa; innaa kazaalika najzil muhsineen

Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.

Aya 106

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ

Inna haazaa lahuwal balaaa'ul mubeen

Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.

Aya 107

وَفَدَيْنَٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍۢ

Wa fadainaahu bizibhin 'azeem

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.

Aya 108

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْءَاخِرِينَ

Wa taraknaa 'alaihi fil aakhireen

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.

Aya 109

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ

Salaamun 'alaaa Ibraaheem

Iwe salama kwa Ibrahim!

Aya 110

كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ

Kazaalika najzil muhsineen

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

Aya 111

إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ

Innahoo min 'ibaadinal mu'mineen

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

Aya 112

وَبَشَّرْنَٰهُ بِإِسْحَٰقَ نَبِيًّۭا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Wa bashsharnaahu bi Ishaaqa Nabiyayam minas saaliheen

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.

Aya 113

وَبَٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَٰقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌۭ وَظَالِمٌۭ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌۭ

Wa baaraknaa 'alaihi wa 'alaaa Ishaaq; wa min zurriyya tihimaa muhsinunw wa zaalimul linafshihee mubeen

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.

Aya 114

وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Wa laqad mananna alaa Moosaa wa Haaroon

Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.

Aya 115

وَنَجَّيْنَٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ

Wa najjainaahumaa wa qawmahumaa minal karbil 'azeem

Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.

Aya 116

وَنَصَرْنَٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَٰلِبِينَ

Wa nasarnaahum fakaanoo humul ghaalibeen

Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.

Aya 117

وَءَاتَيْنَٰهُمَا ٱلْكِتَٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ

Wa aatainaahumal Kitaabal mustabeen

Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.

Aya 118

وَهَدَيْنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ

Wa hadainaahumus Siraatal Mustaqeem

Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.

Aya 119

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْءَاخِرِينَ

Wa taraknaa 'alaihimaa fil aakhireen

Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.

Aya 120

سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Salaamun 'alaa Moosaa wa Haaroon

Iwe salama kwa Musa na Haruni!

Aya 121

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ

Innaa kazaalika najzil muhsineen

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.

Aya 122

إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ

Innahumaa min 'ibaadinal mu'mineen

Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.

Aya 123

وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ

Wa inna Ilyaasa laminal mursaleen

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

Aya 124

إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ

Iz qaala liqawmiheee alaa tattaqoon

Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?

Aya 125

أَتَدْعُونَ بَعْلًۭا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَٰلِقِينَ

Atad'oona Ba'lanw wa tazaroona ahsanal khaaliqeen

Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,

Aya 126

ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ

Allaaha Rabbakum wa Rabba aabaaa'ikumul awwaleen

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?

Aya 127

فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ

Fakazzaboohu fa inna hum lamuhdaroon

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;

Aya 128

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ

Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.

Aya 129

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْءَاخِرِينَ

Wa taraknaa 'alaihi fil aakhireen

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.

Aya 130

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ

Salaamun 'alaaa Ilyaaseen

Iwe salama kwa Ilyas.

Aya 131

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ

Innaa kazaalika najzil muhsineen

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.

Aya 132

إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ

Innahoo min 'ibaadinal mu'mineen

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

Aya 133

وَإِنَّ لُوطًۭا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ

Wa inna Lootal laminal mursaleen

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

Aya 134

إِذْ نَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ

Iz najjainaahu wa ahlahooo ajma'een

Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,

Aya 135

إِلَّا عَجُوزًۭا فِى ٱلْغَٰبِرِينَ

Illaa 'ajoozan fil ghaabireen

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.

Aya 136

ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْءَاخَرِينَ

Summa dammarnal aakhareen

Kisha tukawaangamiza wale wengineo.

Aya 137

وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ

Wa innakum latamurroona 'alaihim musbiheen

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,

Aya 138

وَبِٱلَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ

Wa billail; afalaa ta'qiloon

Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?

Aya 139

وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ

Wa inna Yoonusa laminal mursaleen

Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.

Aya 140

إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ

Iz abaqa ilal fulkil mash hoon

Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.

Aya 141

فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ

Fasaahama fakaana minal mudhadeen

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.

Aya 142

فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌۭ

Faltaqamahul hootu wa huwa muleem

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.

Aya 143

فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ

Falaw laaa annahoo kaana minal musabbiheen

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,

Aya 144

لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ

Lalabisa fee batniheee ilaa Yawmi yub'asoon

Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.

Aya 145

۞ فَنَبَذْنَٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌۭ

Fanabaznaahu bil'araaa'i wa huwa saqeem

Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.

Aya 146

وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةًۭ مِّن يَقْطِينٍۢ

Wa ambatnaa 'alaihi shajaratam mai yaqteen

Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.

Aya 147

وَأَرْسَلْنَٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ

Wa arsalnaahu ilaa mi'ati alfin aw yazeedoon

Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.

Aya 148

فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍۢ

Fa aamanoo famatta' naahum ilaa heen

Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

Aya 149

فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ

Fastaftihim ali Rabbikal banaatu wa lahumul banoon

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?

Aya 150

أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثًۭا وَهُمْ شَٰهِدُونَ

Am khalaqnal malaaa'i kata inaasanw wa hm shaahidoon

Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

Aya 151

أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ

Alaaa innahum min ifkihim la yaqooloon

Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:

Aya 152

وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَٰذِبُونَ

Waladal laahu wa innhum lakaaziboon

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!

Aya 153

أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ

Astafal banaati 'alal baneen

Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?

Aya 154

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ

Maa lakum kaifa tahkumoon

Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?

Aya 155

أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Afalaa tazakkaroon

Hamkumbuki?

Aya 156

أَمْ لَكُمْ سُلْطَٰنٌۭ مُّبِينٌۭ

Am lakum sultaanum mubeen

Au mnayo hoja iliyo wazi?

Aya 157

فَأْتُوا۟ بِكِتَٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ

Faatoo bi Kitaabikum in kuntum saadiqeen

Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.

Aya 158

وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًۭا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ

Wa ja'aloo bainahoo wa bainal jinnati nasabaa; wa laqad 'alimatil jinnatu innahum lamuhdaroon

Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

Aya 159

سُبْحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ

Subhaanal laahi 'ammaa yasifoon

Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.

Aya 160

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ

Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.

Aya 161

فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ

Fa innakum wa maa ta'ubdoon

Basi hakika nyinyi na mnao waabudu

Aya 162

مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَٰتِنِينَ

Maaa antum 'alaihi befaaatineen

Hamwezi kuwapoteza

Aya 163

إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ

Illaa man huwa saalil jaheem

Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.

Aya 164

وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌۭ مَّعْلُومٌۭ

Wa maa minnasa illaa lahoo maqaamum ma'loom

Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.

Aya 165

وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ

Wa innaa llanah nus saaffoon

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

Aya 166

وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ

Wa innaa lanah nul musabbihoon

Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.

Aya 167

وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ

Wa in kaanoo la yaqooloon

Na walikuwapo walio kuwa wakisema:

Aya 168

لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًۭا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ

Law anna 'indana zikram minal awwaleen

Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,

Aya 169

لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ

Lakunna 'ibaadal laahil mukhlaseen

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.

Aya 170

فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ

Fakafaroo bihee fasawfa ya'lamoon

Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.

Aya 171

وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ

Wa laqad sabaqat Kalimatunaa li'ibaadinal mursa leen

Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.

Aya 172

إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ

Innaa hum lahumul mansooroon

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.

Aya 173

وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَٰلِبُونَ

Wa inna jundana lahumul ghaaliboon

Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.

Aya 174

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍۢ

Fatawalla 'anhum hatta heen

Basi waachilie mbali kwa muda.

Aya 175

وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ

Wa absirhum fasawfa yubsiroon

Na watazame, nao wataona.

Aya 176

أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ

Afabi'azaabinaa yasta'jiloon

Je! Wanaihimiza adhabu yetu?

Aya 177

فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ

Fa izaa nazala bisaahatihim fasaaa'a sabaahul munzareen

Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.

Aya 178

وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍۢ

Wa tawalla 'anhum hattaa heen

Na waache kwa muda.

Aya 179

وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ

Wa absir fasawfa yubsiroon

Na tazama, na wao wataona.

Aya 180

سُبْحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ

Subhaana Rabbika Rabbil 'izzati 'amma yasifoon

Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.

Aya 181

وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ

Wa salaamun 'alalmursaleen

Na Salamu juu ya Mitume.

Aya 182

وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Walhamdu lillaahi Rabbil 'aalameen

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.