Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / At-Tariq
86

At-Tariq — Kinachokuja Usiku

الطَّارِقِ
Za Makka Aya 17
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ

Wassamaaa'i wattaariq

Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!

Aya 2

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ

Wa maaa adraaka mattaariq

Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?

Aya 3

ٱلنَّجْمُ ٱلثَّاقِبُ

Annajmus saaqib

Ni Nyota yenye mwanga mkali.

Aya 4

إِن كُلُّ نَفْسٍۢ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌۭ

In kullu nafsil lammaa 'alaihaa haafiz

Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.

Aya 5

فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Fal yanzuril insaanu mimma khuliq

Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?

Aya 6

خُلِقَ مِن مَّآءٍۢ دَافِقٍۢ

Khuliqa mim maaa'in daafiq

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,

Aya 7

يَخْرُجُ مِنۢ بَيْنِ ٱلصُّلْبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yakhruju mim bainissulbi wat taraaa'ib

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

Aya 8

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجْعِهِۦ لَقَادِرٌۭ

Innahoo 'alaa raj'ihee laqaadir

Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

Aya 9

يَوْمَ تُبْلَى ٱلسَّرَآئِرُ

Yawma tublas saraaa'ir

Siku zitakapo dhihirishwa siri.

Aya 10

فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٍۢ وَلَا نَاصِرٍۢ

Famaa lahoo min quwwatinw wa laa naasir

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

Aya 11

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجْعِ

Wassamaaa'i zaatir raj'

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!

Aya 12

وَٱلْأَرْضِ ذَاتِ ٱلصَّدْعِ

Wal ardi zaatis sad'

Na kwa ardhi inayo pasuka!

Aya 13

إِنَّهُۥ لَقَوْلٌۭ فَصْلٌۭ

Innahoo laqawlun fasl

Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

Aya 14

وَمَا هُوَ بِٱلْهَزْلِ

Wa maa huwa bil hazl

Wala si mzaha.

Aya 15

إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًۭا

Innahum yakeedoona kaidaa

Hakika wao wanapanga mpango.

Aya 16

وَأَكِيدُ كَيْدًۭا

Wa akeedu kaidaa

Na Mimi napanga mpango.

Aya 17

فَمَهِّلِ ٱلْكَٰفِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًۢا

Famahhilil kaafireena amhilhum ruwaidaa

Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.