وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Wassamaaa'i wattaariq
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Wassamaaa'i wattaariq
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Wa maaa adraaka mattaariq
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
ٱلنَّجْمُ ٱلثَّاقِبُ
Annajmus saaqib
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
إِن كُلُّ نَفْسٍۢ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌۭ
In kullu nafsil lammaa 'alaihaa haafiz
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Fal yanzuril insaanu mimma khuliq
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
خُلِقَ مِن مَّآءٍۢ دَافِقٍۢ
Khuliqa mim maaa'in daafiq
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
يَخْرُجُ مِنۢ بَيْنِ ٱلصُّلْبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yakhruju mim bainissulbi wat taraaa'ib
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجْعِهِۦ لَقَادِرٌۭ
Innahoo 'alaa raj'ihee laqaadir
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
يَوْمَ تُبْلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Yawma tublas saraaa'ir
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٍۢ وَلَا نَاصِرٍۢ
Famaa lahoo min quwwatinw wa laa naasir
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجْعِ
Wassamaaa'i zaatir raj'
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
وَٱلْأَرْضِ ذَاتِ ٱلصَّدْعِ
Wal ardi zaatis sad'
Na kwa ardhi inayo pasuka!
إِنَّهُۥ لَقَوْلٌۭ فَصْلٌۭ
Innahoo laqawlun fasl
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
وَمَا هُوَ بِٱلْهَزْلِ
Wa maa huwa bil hazl
Wala si mzaha.
إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًۭا
Innahum yakeedoona kaidaa
Hakika wao wanapanga mpango.
وَأَكِيدُ كَيْدًۭا
Wa akeedu kaidaa
Na Mimi napanga mpango.
فَمَهِّلِ ٱلْكَٰفِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًۢا
Famahhilil kaafireena amhilhum ruwaidaa
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.