Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Buruj
85

Al-Buruj — Buruji

البُرُوجِ
Za Makka Aya 22
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ

Wassamaaa'i zaatil burooj

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

Aya 2

وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ

Wal yawmil maw'ood

Na kwa siku iliyo ahidiwa!

Aya 3

وَشَاهِدٍۢ وَمَشْهُودٍۢ

Wa shaahidinw wa mashhood

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

Aya 4

قُتِلَ أَصْحَٰبُ ٱلْأُخْدُودِ

Qutila as haabul ukhdood

Wameangamizwa watu wa makhandaki

Aya 5

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ

Annaari zaatil waqood

Yenye moto wenye kuni nyingi,

Aya 6

إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌۭ

Iz hum 'alaihaa qu'ood

Walipo kuwa wamekaa hapo,

Aya 7

وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌۭ

Wa hum 'alaa maa yaf'aloona bilmu 'mineena shuhood

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

Aya 8

وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ

Wa maa naqamoo minhum illaaa aiyu'minoo billaahil 'azeezil Hameed

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

Aya 9

ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍۢ شَهِيدٌ

Allazee lahoo mulkus samaawaati wal ard; wallaahu 'alaa kulli shai 'in Shaheed

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

Aya 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ

Innal lazeena fatanul mu'mineena wal mu'minaati summa lam yatooboo falahum 'azaabu Jahannama wa lahum 'azaabul hareeq

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

Aya 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ جَنَّٰتٌۭ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ

Innal lazeena aamanoo wa 'amilus saalihaati lahum Jannaatun tajree min tahtihal anhaar; zaalikal fawzul kabeer

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

Aya 12

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Inna batsha Rabbika lashadeed

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

Aya 13

إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ

Innahoo Huwa yubdi'u wa yu'eed

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

Aya 14

وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ

Wa Huwal Ghafoorul Wadood

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

Aya 15

ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ

Zul 'Arshil Majeed

Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

Aya 16

فَعَّالٌۭ لِّمَا يُرِيدُ

Fa' 'aalul limaa yureed

Atendaye ayatakayo.

Aya 17

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ

Hal ataaka hadeesul junood

Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

Aya 18

فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ

Fir'awna wa Samood

Ya Firauni na Thamudi?

Aya 19

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍۢ

Balil lazeena kafaroo fee takzeeb

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

Aya 20

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ

Wallaahu minw waraaa'ihim muheet

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

Aya 21

بَلْ هُوَ قُرْءَانٌۭ مَّجِيدٌۭ

Bal huwa Quraanum Majeed

Bali hii ni Qur'ani tukufu

Aya 22

فِى لَوْحٍۢ مَّحْفُوظٍۭ

Fee Lawhim Mahfooz

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.