Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Inshiqaq
84

Al-Inshiqaq — Kupasuka

الانشِقَاقِ
Za Makka Aya 25
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتْ

Izas samaaa'un shaqqat

Itapo chanika mbingu,

Aya 2

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

Wa azinat li Rabbihaa wa huqqat

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

Aya 3

وَإِذَا ٱلْأَرْضُ مُدَّتْ

Wa izal ardu muddat

Na ardhi itakapo tanuliwa,

Aya 4

وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ

Wa alqat maa feehaa wa takhallat

Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

Aya 5

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

Wa azinat li Rabbihaa wa huqqat

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

Aya 6

يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًۭا فَمُلَٰقِيهِ

Yaaa ayyuhal insaanu innaka kaadihun ilaa Rabbika kad han famulaaqeeh

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

Aya 7

فَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ

Fa ammaa man ootiya kitaabahoo biyameenih

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

Aya 8

فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًۭا يَسِيرًۭا

Fasawfa yuhaasabu hi saabai yaseeraa

Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

Aya 9

وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًۭا

Wa yanqalibu ilaaa ahlihee masrooraa

Na arudi kwa ahali zake na furaha.

Aya 10

وَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهْرِهِۦ

Wa ammaa man ootiya kitaabahoo waraaa'a zahrih

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

Aya 11

فَسَوْفَ يَدْعُوا۟ ثُبُورًۭا

Fasawfa yad'oo subooraa

Basi huyo ataomba kuteketea.

Aya 12

وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا

Wa yaslaa sa'eeraa

Na ataingia Motoni.

Aya 13

إِنَّهُۥ كَانَ فِىٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًا

Innahoo kaana feee ahlihee masrooraa

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

Aya 14

إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ

Innahoo zanna al lai yahoor

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

Aya 15

بَلَىٰٓ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرًۭا

Balaaa inna Rabbahoo kaana bihee baseeraa

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

Aya 16

فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلشَّفَقِ

Falaaa uqsimu bishshafaq

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

Aya 17

وَٱلَّيْلِ وَمَا وَسَقَ

Wallaili wa maa wasaq

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

Aya 18

وَٱلْقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ

Walqamari izat tasaq

Na kwa mwezi unapo pevuka,

Aya 19

لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍۢ

Latarkabunna tabaqan 'an tabaq

Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!

Aya 20

فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ

Famaa lahum laa yu'minoon

Basi wana nini hawaamini?

Aya 21

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ ٱلْقُرْءَانُ لَا يَسْجُدُونَ ۩

Wa izaa quri'a 'alaihimul Quraanu laa yasjudoon

Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?

Aya 22

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ يُكَذِّبُونَ

Balil lazeena kafaroo yukazziboon

Bali walio kufuru wanakanusha tu.

Aya 23

وَٱللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ

Wallaahu a'lamu bimaa yoo'oon

Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

Aya 24

فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

Fabashshirhum bi'azaabin aleem

Basi wabashirie adhabu chungu!

Aya 25

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۭ

Illal lazeena aamanoo wa 'amilus saalihaati lahum ajrun ghairu mamnoon

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.