Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Mutaffifin
83

Al-Mutaffifin — Wapunjaji

المُطَفِّفِينَ
Za Makka Aya 36
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَيْلٌۭ لِّلْمُطَفِّفِينَ

Wailul lil mutaffifeen

Ole wao hao wapunjao!

Aya 2

ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ

Allazeena izak taaloo 'alan naasi yastawfoon

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

Aya 3

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ

Wa izaa kaaloohum aw wazanoohum yukhsiroon

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

Aya 4

أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ

Alaa yazunnu ulaaa'ika annahum mab'oosoon

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

Aya 5

لِيَوْمٍ عَظِيمٍۢ

Li Yawmin 'Azeem

Katika Siku iliyo kuu,

Aya 6

يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Yawma yaqoomun naasu li Rabbil 'aalameen

Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Aya 7

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍۢ

Kallaaa inna kitaabal fujjaari lafee Sijjeen

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

Aya 8

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌۭ

Wa maa adraaka maa Sijjeen

Unajua nini Sijjin?

Aya 9

كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ

Kitaabum marqoom

Kitabu kilicho andikwa.

Aya 10

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma'izil lil mukazzibeen

Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

Aya 11

ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

Allazeena yukazziboona bi yawmid deen

Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

Aya 12

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ

Wa maa yukazzibu biheee illaa kullu mu'tadin aseem

Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

Aya 13

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ

Izaa tutlaa'alaihi aayaatunaa qaala asaateerul awwaleen

Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

Aya 14

كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ

Kallaa bal raana 'alaa quloobihim maa kaanoo yaksiboon

Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

Aya 15

كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّمَحْجُوبُونَ

Kallaaa innahum 'ar Rabbihim yawma'izil lamah jooboon

Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

Aya 16

ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ

Summa innahum lasaa lul jaheem

Kisha wataingia Motoni!

Aya 17

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Summa yuqaalu haazal lazee kuntum bihee tukazziboon

Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

Aya 18

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ

Kallaaa inna kitaabal abraari lafee'Illiyyeen

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

Aya 19

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ

Wa maaa adraaka maa 'Illiyyoon

Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

Aya 20

كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ

Kitaabum marqoom

Kitabu kilicho andikwa.

Aya 21

يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ

Yashhadu hul muqarra boon

Wanakishuhudia walio karibishwa.

Aya 22

إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ

Innal abraara lafee Na'eem

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

Aya 23

عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

'Alal araaa'iki yanzuroon

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Aya 24

تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ

Ta'rifu fee wujoohihim nadratan na'eem

Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

Aya 25

يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍۢ مَّخْتُومٍ

Yusqawna mir raheeqim makhtoom

Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

Aya 26

خِتَٰمُهُۥ مِسْكٌۭ ۚ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَٰفِسُونَ

Khitaamuhoo misk; wa fee zaalika falyatanaafasil Mutanaafisoon

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

Aya 27

وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ

Wa mizaajuhoo min Tasneem

Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

Aya 28

عَيْنًۭا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ

'Ainaiy yashrabu bihal muqarraboon

Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

Aya 29

إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ

Innal lazeena ajramoo kaanoo minal lazeena aamanoo yadhakoon

Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

Aya 30

وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ

Wa izaa marroo bihim yataghaamazoon

Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

Aya 31

وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ

Wa izan qalabooo ilaaa ahlihimun qalaboo fakiheen

Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

Aya 32

وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ

Wa izaa ra awhum qaalooo inna haaa'ulaaa'i ladaaal loon

Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

Aya 33

وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَٰفِظِينَ

Wa maaa ursiloo 'alaihim haafizeen

Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

Aya 34

فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ

Fal yawmal lazeena aamanoo minal kuffaari yadhakoon

Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

Aya 35

عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

'Alal araaa'iki yanzuroon

Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Aya 36

هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ

Hal suwwibal kuffaaru maa kaanoo yaf'aloon

Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?