إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ
Izas samaaa'un fatarat
Mbingu itapo chanika,
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ
Izas samaaa'un fatarat
Mbingu itapo chanika,
وَإِذَا ٱلْكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتْ
Wa izal kawaakibun tasarat
Na nyota zitapo tawanyika,
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ فُجِّرَتْ
Wa izal bihaaru fujjirat
Na bahari zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا ٱلْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
Wa izal qubooru bu'sirat
Na makaburi yatapo fukuliwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
'Alimat nafsum maa qaddamat wa akhkharat
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلْكَرِيمِ
Yaaa ayyuhal insaaanu maa gharraka bi Rabbikal kareem
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
ٱلَّذِى خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Allazee khalaqaka fasaw waaka fa'adalak
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
فِىٓ أَىِّ صُورَةٍۢ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Feee ayye sooratim maa shaaa'a rakkabak
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Kalla bal tukazziboona bid deen
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَٰفِظِينَ
Wa inna 'alaikum lahaa fizeen
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
كِرَامًۭا كَٰتِبِينَ
Kiraaman kaatibeen
Waandishi wenye hishima,
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
Ya'lamoona ma taf'aloon
Wanayajua mnayo yatenda.
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍۢ
Innal abraara lafee na'eem
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
وَإِنَّ ٱلْفُجَّارَ لَفِى جَحِيمٍۢ
Wa innal fujjaara lafee jaheem
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ ٱلدِّينِ
Yaslawnahaa Yawmad Deen
Wataingia humo Siku ya Malipo.
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَآئِبِينَ
Wa maa hum 'anhaa bighaaa 'ibeen
Na hawatoacha kuwamo humo.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Wa maaa adraaka maa Yawmud Deen
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ثُمَّ مَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Summa maaa adraaka maa Yawmud Deen
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌۭ لِّنَفْسٍۢ شَيْـًۭٔا ۖ وَٱلْأَمْرُ يَوْمَئِذٍۢ لِّلَّهِ
Yawma laa tamliku nafsul linafsin shai'anw walamru yawma'izil lillaah
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.