إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Izash shamsu kuwwirat
Jua litakapo kunjwa,
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Izash shamsu kuwwirat
Jua litakapo kunjwa,
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ
Wa izan nujoomun kadarat
Na nyota zikazimwa,
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Wa izal jibaalu suyyirat
Na milima ikaondolewa,
وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Wa izal 'ishaaru 'uttilat
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Wa izal wuhooshu hushirat
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Wa izal bihaaru sujjirat
Na bahari zikawaka moto,
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Wa izan nufoosu zuwwijat
Na nafsi zikaunganishwa,
وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ
Wa izal maw'oodatu su'ilat
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
بِأَىِّ ذَنۢبٍۢ قُتِلَتْ
Bi ayyi zambin qutilat
Kwa kosa gani aliuliwa?
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ
Wa izas suhufu nushirat
Na madaftari yatakapo enezwa,
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ
Wa izas samaaa'u kushitat
Na mbingu itapo tanduliwa,
وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Wa izal jaheemu su'-'irat
Na Jahannamu itapo chochewa,
وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Wa izal jannatu uzlifat
Na Pepo ikasogezwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّآ أَحْضَرَتْ
'Alimat nafsum maaa ahdarat
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ
Falaaa uqsimu bil khunnas
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ
Al jawaaril kunnas
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Wallaili izaa 'as'as
Na kwa usiku unapo pungua,
وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Wassubhi izaa tanaffas
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍۢ كَرِيمٍۢ
Innahoo laqawlu rasoolin kareem
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍۢ
Zee quwwatin 'inda zil 'arshi makeen
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
مُّطَاعٍۢ ثَمَّ أَمِينٍۢ
Mutaa'in samma ameen
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍۢ
Wa maa saahibukum bimajnoon
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ
Wa laqad ra aahu bilufuqil mubeen
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍۢ
Wa maa huwa 'alal ghaibi bidaneen
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَٰنٍۢ رَّجِيمٍۢ
Wa maa huwa biqawli shaitaanir rajeem
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Fa ayna tazhaboon
Basi mnakwenda wapi?
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ
In huwa illaa zikrul lil'aalameen
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Liman shaaa'a minkum ai yastaqeem
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Wa maa tashaaa'oona illaaa ai yashaaa 'al laahu Rabbul 'Aalameen
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.