Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / At-Takwir
81

At-Takwir — Kukunjwa

التَّكۡوِيرِ
Za Makka Aya 29
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ

Izash shamsu kuwwirat

Jua litakapo kunjwa,

Aya 2

وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ

Wa izan nujoomun kadarat

Na nyota zikazimwa,

Aya 3

وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ

Wa izal jibaalu suyyirat

Na milima ikaondolewa,

Aya 4

وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ

Wa izal 'ishaaru 'uttilat

Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,

Aya 5

وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ

Wa izal wuhooshu hushirat

Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

Aya 6

وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ

Wa izal bihaaru sujjirat

Na bahari zikawaka moto,

Aya 7

وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ

Wa izan nufoosu zuwwijat

Na nafsi zikaunganishwa,

Aya 8

وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ

Wa izal maw'oodatu su'ilat

Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,

Aya 9

بِأَىِّ ذَنۢبٍۢ قُتِلَتْ

Bi ayyi zambin qutilat

Kwa kosa gani aliuliwa?

Aya 10

وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ

Wa izas suhufu nushirat

Na madaftari yatakapo enezwa,

Aya 11

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ

Wa izas samaaa'u kushitat

Na mbingu itapo tanduliwa,

Aya 12

وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ

Wa izal jaheemu su'-'irat

Na Jahannamu itapo chochewa,

Aya 13

وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ

Wa izal jannatu uzlifat

Na Pepo ikasogezwa,

Aya 14

عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّآ أَحْضَرَتْ

'Alimat nafsum maaa ahdarat

Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.

Aya 15

فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ

Falaaa uqsimu bil khunnas

Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,

Aya 16

ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ

Al jawaaril kunnas

Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

Aya 17

وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ

Wallaili izaa 'as'as

Na kwa usiku unapo pungua,

Aya 18

وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ

Wassubhi izaa tanaffas

Na kwa asubuhi inapo pambazuka,

Aya 19

إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍۢ كَرِيمٍۢ

Innahoo laqawlu rasoolin kareem

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,

Aya 20

ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍۢ

Zee quwwatin 'inda zil 'arshi makeen

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,

Aya 21

مُّطَاعٍۢ ثَمَّ أَمِينٍۢ

Mutaa'in samma ameen

Anaye t'iiwa, tena muaminifu.

Aya 22

وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍۢ

Wa maa saahibukum bimajnoon

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

Aya 23

وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ

Wa laqad ra aahu bilufuqil mubeen

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

Aya 24

وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍۢ

Wa maa huwa 'alal ghaibi bidaneen

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

Aya 25

وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَٰنٍۢ رَّجِيمٍۢ

Wa maa huwa biqawli shaitaanir rajeem

Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.

Aya 26

فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ

Fa ayna tazhaboon

Basi mnakwenda wapi?

Aya 27

إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ

In huwa illaa zikrul lil'aalameen

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Aya 28

لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ

Liman shaaa'a minkum ai yastaqeem

Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.

Aya 29

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Wa maa tashaaa'oona illaaa ai yashaaa 'al laahu Rabbul 'Aalameen

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.