Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Abasa
80

Abasa — Alikunja Uso

عَبَسَ
Za Makka Aya 42
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

'Abasa wa tawallaa.

Alikunja kipaji na akageuka,

Aya 2

أَن جَآءَهُ ٱلْأَعْمَىٰ

An jaa-ahul 'a-maa

Kwa sababu alimjia kipofu!

Aya 3

وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

Wa maa yudreeka la'allahu yaz zakkaa.

Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?

Aya 4

أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكْرَىٰٓ

Au yaz zak karu fatanfa 'ahuz zikraa.

Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?

Aya 5

أَمَّا مَنِ ٱسْتَغْنَىٰ

Amma manis taghnaa

Ama ajionaye hana haja,

Aya 6

فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ

Fa-anta lahu tasaddaa

Wewe ndio unamshughulikia?

Aya 7

وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ

Wa ma 'alaika allaa yaz zakka.

Na si juu yako kama hakutakasika.

Aya 8

وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسْعَىٰ

Wa amma man jaa-aka yas'a

Ama anaye kujia kwa juhudi,

Aya 9

وَهُوَ يَخْشَىٰ

Wahuwa yakhshaa,

Naye anaogopa,

Aya 10

فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ

Fa-anta 'anhu talah haa.

Ndio wewe unampuuza?

Aya 11

كَلَّآ إِنَّهَا تَذْكِرَةٌۭ

Kalla innaha tazkirah

Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.

Aya 12

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Faman shaa a zakarah

Basi anaye penda akumbuke.

Aya 13

فِى صُحُفٍۢ مُّكَرَّمَةٍۢ

Fi suhufim mukar rama,

Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,

Aya 14

مَّرْفُوعَةٍۢ مُّطَهَّرَةٍۭ

Marfoo'atim mutah hara,

Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.

Aya 15

بِأَيْدِى سَفَرَةٍۢ

Bi'aidee safara

Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,

Aya 16

كِرَامٍۭ بَرَرَةٍۢ

Kiraamim bararah.

Watukufu, wema.

Aya 17

قُتِلَ ٱلْإِنسَٰنُ مَآ أَكْفَرَهُۥ

Qutilal-insanu maa akfarah.

Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?

Aya 18

مِنْ أَىِّ شَىْءٍ خَلَقَهُۥ

Min aiyyi shai-in Khalaq

Kwa kitu gani amemuumba?

Aya 19

مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

Min nutfah; khalaqahu faqad-darah.

Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.

Aya 20

ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ

Thummas sabeela yas-sarah

Kisha akamsahilishia njia.

Aya 21

ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقْبَرَهُۥ

Thumma amatahu fa-aqbarah

Kisha akamfisha, akamtia kaburini.

Aya 22

ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ

Thumma iza shaa-a ansharah

Kisha apendapo atamfufua.

Aya 23

كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَآ أَمَرَهُۥ

Kalla lamma yaqdi maa amarah.

La! Hajamaliza aliyo muamuru.

Aya 24

فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ

Falyanzuril insanu ilaa ta-amih

Hebu mtu na atazame chakula chake.

Aya 25

أَنَّا صَبَبْنَا ٱلْمَآءَ صَبًّۭا

Anna sabab nalmaa-a sabba.

Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,

Aya 26

ثُمَّ شَقَقْنَا ٱلْأَرْضَ شَقًّۭا

Thumma sha qaqnal-arda shaqqa.

Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,

Aya 27

فَأَنۢبَتْنَا فِيهَا حَبًّۭا

Fa ambatna feeha habba

Kisha tukaotesha humo nafaka,

Aya 28

وَعِنَبًۭا وَقَضْبًۭا

Wa 'inabaw-wa qadba

Na zabibu, na mimea ya majani,

Aya 29

وَزَيْتُونًۭا وَنَخْلًۭا

Wa zaitoonaw wanakh la'

Na mizaituni, na mitende,

Aya 30

وَحَدَآئِقَ غُلْبًۭا

Wa hadaa-iqa ghulba

Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,

Aya 31

وَفَٰكِهَةًۭ وَأَبًّۭا

Wa faki hataw-wa abba.

Na matunda, na malisho ya wanyama;

Aya 32

مَّتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ

Mata'al-lakum wa li-an'amikum.

Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

Aya 33

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ

Faiza jaa-atis saakhah.

Basi utakapo kuja ukelele,

Aya 34

يَوْمَ يَفِرُّ ٱلْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ

Yauma yafir-rul mar-u min akheeh

Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,

Aya 35

وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ

Wa ummihee wa abeeh

Na mamaye na babaye,

Aya 36

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ

Wa sahi batihee wa baneeh.

Na mkewe na wanawe -

Aya 37

لِكُلِّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍۢ شَأْنٌۭ يُغْنِيهِ

Likul limri-im-minuhm yaumaa-izin shaa nuy-yughneeh

Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.

Aya 38

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ مُّسْفِرَةٌۭ

Wujoo huny-yauma-izim-musfira;

Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,

Aya 39

ضَاحِكَةٌۭ مُّسْتَبْشِرَةٌۭ

Dahi katum mustab shirah

Zitacheka, zitachangamka;

Aya 40

وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌۭ

Wa wujoohuy yauma-izin 'alaiha ghabar a

Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,

Aya 41

تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ

Tarhaquha qatarah.

Giza totoro litazifunika,

Aya 42

أُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْكَفَرَةُ ٱلْفَجَرَةُ

Ulaa-ika humul-kafa ratul-fajarah.

Hao ndio makafiri watenda maovu.