Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / An-Nazi'at
79

An-Nazi'at — Wanaochomoa

النَّازِعَاتِ
Za Makka Aya 46
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرْقًۭا

Wan naazi 'aati gharqa

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,

Aya 2

وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشْطًۭا

Wan naa shi taati nashta

Na kwa wanao toa kwa upole,

Aya 3

وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبْحًۭا

Wass saabi-haati sabha

Na wanao ogelea,

Aya 4

فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبْقًۭا

Fass saabi qaati sabqa

Wakishindana mbio,

Aya 5

فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًۭا

Fal mu dab-bi raati amra

Wakidabiri mambo.

Aya 6

يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ

Yawma tarjufur raajifa

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,

Aya 7

تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ

Tatba'u har raadifa

Kifuate cha kufuatia.

Aya 8

قُلُوبٌۭ يَوْمَئِذٍۢ وَاجِفَةٌ

Quloobuny-yau maaiziw-waaji-fa

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,

Aya 9

أَبْصَٰرُهَا خَٰشِعَةٌۭ

Absaa ruhaa khashi'ah

Macho yatainama chini.

Aya 10

يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ

Ya qoo loona a-inna lamar doo doona fil haafirah

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

Aya 11

أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمًۭا نَّخِرَةًۭ

Aizaa kunna 'izaa man-nakhirah

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

Aya 12

قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًۭا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌۭ

Qaalu tilka izan karratun khaasirah.

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

Aya 13

فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ

Fa inna ma hiya zajratuw-waahida

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

Aya 14

فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ

Faizaa hum biss saahirah

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

Aya 15

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Hal ataaka hadeethu Musaa

Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

Aya 16

إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى

Iz nadaahu rabbuhu bil waadil-muqad dasi tuwa

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

Aya 17

ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Izhab ilaa fir'auna innahu taghaa.

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.

Aya 18

فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

Faqul hal laka ilaa-an tazakka.

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

Aya 19

وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ

Wa ahdi yaka ila rabbika fatakh sha

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

Aya 20

فَأَرَىٰهُ ٱلْءَايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ

Fa araahul-aayatal kubra.

Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

Aya 21

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Fa kazzaba wa asaa.

Lakini aliikadhibisha na akaasi.

Aya 22

ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ

Thumma adbara yas'aa.

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

Aya 23

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Fa hashara fanada.

Akakusanya watu akanadi.

Aya 24

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ

Faqala ana rabbu kumul-a'laa.

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

Aya 25

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْءَاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ

Fa-akha zahul laahu nakalal aakhirati wal-oola.

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

Aya 26

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةًۭ لِّمَن يَخْشَىٰٓ

Inna fee zaalika la'ibratal limaiy-yaksha

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

Aya 27

ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا

A-antum a shaddu khalqan amis samaa-u banaaha.

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

Aya 28

رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Raf'a sam kaha fasaw waaha

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

Aya 29

وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا

Wa aghtasha lailaha wa akhraja duhaaha.

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.

Aya 30

وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Wal arda b'ada zaalika dahaaha.

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

Aya 31

أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا

Akhraja minha maa-aha wa mar 'aaha.

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

Aya 32

وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا

Wal jibala arsaaha.

Na milima akaisimamisha,

Aya 33

مَتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ

Mataa'al lakum wali an 'aamikum.

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

Aya 34

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ

Fa-izaa jaaa'atit taaam matul kubraa.

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

Aya 35

يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

Yauma Yata zakkarul insaanu ma sa'aa.

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

Aya 36

وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

Wa burrizatil-jaheemu limany-yaraa.

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

Aya 37

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Fa ammaa man taghaa.

Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

Aya 38

وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا

Wa aasaral hayaatad dunyaa

Na akakhiari maisha ya dunia,

Aya 39

فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ

Fa innal jaheema hiyal maawaa.

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

Aya 40

وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ

Wa ammaa man khaafa maqaama Rabbihee wa nahan nafsa 'anil hawaa

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

Aya 41

فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ

Fa innal jannata hiyal maawaa

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

Aya 42

يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا

Yas'aloonaka 'anis saa'ati ayyaana mursaahaa

Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

Aya 43

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ

Feema anta min zikraahaa

Una nini wewe hata uitaje?

Aya 44

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ

Ilaa Rabbika muntahaa haa

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

Aya 45

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا

Innamaaa anta munziru maiy yakshaahaa

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

Aya 46

كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓا۟ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا

Ka annahum Yawma yarawnahaa lam yalbasooo illaa 'ashiyyatan aw duhaahaa

Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.