Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / An-Naba
78

An-Naba — Habari

النَّبَإِ
Za Makka Aya 40
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ

'Amma Yatasaa-aloon

WANAULIZANA nini?

Aya 2

عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلْعَظِيمِ

'Anin-nabaa-il 'azeem

Ile khabari kuu,

Aya 3

ٱلَّذِى هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ

Allazi hum feehi mukh talifoon

Ambayo kwayo wanakhitalifiana.

Aya 4

كَلَّا سَيَعْلَمُونَ

Kallaa sa y'alamoon

La! Karibu watakuja jua.

Aya 5

ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ

Thumma kallaa sa y'alamoon

Tena la! Karibu watakuja jua.

Aya 6

أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ مِهَٰدًۭا

Alam naj'alil arda mihaa da

Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?

Aya 7

وَٱلْجِبَالَ أَوْتَادًۭا

Wal jibaala au taada

Na milima kama vigingi?

Aya 8

وَخَلَقْنَٰكُمْ أَزْوَٰجًۭا

Wa khalaq naakum azwaaja

Na tukakuumbeni kwa jozi?

Aya 9

وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًۭا

Waja'alnan naumakum subata

Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?

Aya 10

وَجَعَلْنَا ٱلَّيْلَ لِبَاسًۭا

Waja'alnal laila libasa

Na tukaufanya usiku ni nguo?

Aya 11

وَجَعَلْنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشًۭا

Waja'alnan nahara ma 'aasha

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?

Aya 12

وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًۭا شِدَادًۭا

Wa banaina fauqakum sab 'an shi daada

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

Aya 13

وَجَعَلْنَا سِرَاجًۭا وَهَّاجًۭا

Waja'alna siraajaw wah haaja

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;

Aya 14

وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلْمُعْصِرَٰتِ مَآءًۭ ثَجَّاجًۭا

Wa anzalna minal m'usiraati maa-an saj-jaaja

Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,

Aya 15

لِّنُخْرِجَ بِهِۦ حَبًّۭا وَنَبَاتًۭا

Linukh rija bihee habbaw wana baata

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,

Aya 16

وَجَنَّٰتٍ أَلْفَافًا

Wa jan naatin alfafa

Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.

Aya 17

إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ كَانَ مِيقَٰتًۭا

Inna yaumal-fasli kana miqaata

Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,

Aya 18

يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًۭا

Yauma yun fakhu fis-soori fataa toona afwaaja

Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,

Aya 19

وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ أَبْوَٰبًۭا

Wa futiha tis samaa-u fakaanat abwaaba

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,

Aya 20

وَسُيِّرَتِ ٱلْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا

Wa suyyi raatil jibaalu fa kaanat saraaba

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.

Aya 21

إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًۭا

Inna jahan nama kaanat mirsaada

Hakika Jahannamu inangojea!

Aya 22

لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابًۭا

Lit taa gheena ma aaba

Kwa walio asi ndio makaazi yao,

Aya 23

لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحْقَابًۭا

Laa bitheena feehaa ahqaaba

Wakae humo karne baada ya karne,

Aya 24

لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًۭا وَلَا شَرَابًا

Laa ya zooqoona feeha bar daw walaa sharaaba

Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,

Aya 25

إِلَّا حَمِيمًۭا وَغَسَّاقًۭا

Illa hamee maw-wa ghas saaqa

Ila maji yamoto sana na usaha,

Aya 26

جَزَآءًۭ وِفَاقًا

Jazaa-aw wi faaqa

Ndio jaza muwafaka.

Aya 27

إِنَّهُمْ كَانُوا۟ لَا يَرْجُونَ حِسَابًۭا

Innahum kaanu laa yarjoona hisaaba

Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.

Aya 28

وَكَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابًۭا

Wa kazzabu bi aayaa tina kizzaba

Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.

Aya 29

وَكُلَّ شَىْءٍ أَحْصَيْنَٰهُ كِتَٰبًۭا

Wa kulla shai-in ahsai naahu kitaa ba

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.

Aya 30

فَذُوقُوا۟ فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا

Fa zooqoo falan-nazee dakum ill-laa azaaba

Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!

Aya 31

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا

Inna lil mutta qeena mafaaza

Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,

Aya 32

حَدَآئِقَ وَأَعْنَٰبًۭا

Hadaa-iqa wa a'anaa ba

Mabustani na mizabibu,

Aya 33

وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًۭا

Wa kaawa 'iba at raaba

Na wake walio lingana nao,

Aya 34

وَكَأْسًۭا دِهَاقًۭا

Wa ka'san di haaqa

Na bilauri zilizo jaa,

Aya 35

لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًۭا وَلَا كِذَّٰبًۭا

Laa yasma'oona fiha lagh waw walaa kizzaba

Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -

Aya 36

جَزَآءًۭ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابًۭا

Jazaa-am mir-rabbika ataa-an hisaaba

Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.

Aya 37

رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ٱلرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًۭا

Rabbis samaa waati wal ardi wa maa baina humar rahmaani laa yam likoona minhu khi taaba

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!

Aya 38

يَوْمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلْمَلَٰٓئِكَةُ صَفًّۭا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًۭا

Yauma yaqoo mur roohu wal malaa-ikatu saf-fal laa yata kalla moona illa man azina lahur rahmaanu wa qaala sawaaba

Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.

Aya 39

ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلْحَقُّ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا

Zaalikal yaumul haqqu faman shaa-at ta khaaza ill-laa rabbihi ma-aaba

Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.

Aya 40

إِنَّآ أَنذَرْنَٰكُمْ عَذَابًۭا قَرِيبًۭا يَوْمَ يَنظُرُ ٱلْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلْكَافِرُ يَٰلَيْتَنِى كُنتُ تُرَٰبًۢا

In naa anzar naakum azaaban qareebaiy-yauma yan zurul marr-u maa qaddamat yadaahu wa ya qoolul-kaafiru yaa lai tanee kuntu turaaba

Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!