Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Mursalat
77

Al-Mursalat — Waliotumwa

المُرۡسَلَاتِ
Za Makka Aya 50
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلْمُرْسَلَٰتِ عُرْفًۭا

Wal mursalaati'urfaa

Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!

Aya 2

فَٱلْعَٰصِفَٰتِ عَصْفًۭا

Fal'aasifaati 'asfaa

Na zinazo vuma kwa kasi!

Aya 3

وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشْرًۭا

Wannaashiraati nashraa

Na zikaeneza maeneo yote!

Aya 4

فَٱلْفَٰرِقَٰتِ فَرْقًۭا

Falfaariqaati farqaa

Na zinazo farikisha zikatawanya!

Aya 5

فَٱلْمُلْقِيَٰتِ ذِكْرًا

Falmulqiyaati zikra

Na zinazo peleka mawaidha!

Aya 6

عُذْرًا أَوْ نُذْرًا

'Uzran aw nuzraa

Kwa kuudhuru au kuonya,

Aya 7

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٌۭ

Innamaa too'adoona lawaaqi'

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

Aya 8

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتْ

Fa izam nujoomu tumisat

Wakati nyota zitakapo futwa,

Aya 9

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتْ

Wa izas samaaa'u furijat

Na mbingu zitakapo pasuliwa,

Aya 10

وَإِذَا ٱلْجِبَالُ نُسِفَتْ

Wa izal jibaalu nusifat

Na milima itakapo peperushwa,

Aya 11

وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتْ

Wa izar Rusulu uqqitat

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

Aya 12

لِأَىِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ

Li ayyi yawmin ujjilat

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

Aya 13

لِيَوْمِ ٱلْفَصْلِ

Li yawmil Fasl

Kwa siku ya kupambanua!

Aya 14

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ

Wa maaa adraaka maa yawmul fasl

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

Aya 15

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma 'izillilmukazzibeen

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 16

أَلَمْ نُهْلِكِ ٱلْأَوَّلِينَ

Alam nuhlikil awwaleen

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

Aya 17

ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ ٱلْءَاخِرِينَ

Summa nutbi'uhumul aakhireen

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

Aya 18

كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ

Kazzlika naf'alu bilmujrimeen

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

Aya 19

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailunw yawma 'izil lil mukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 20

أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّآءٍۢ مَّهِينٍۢ

Alam nakhlukkum mimmaaa'im maheen

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

Aya 21

فَجَعَلْنَٰهُ فِى قَرَارٍۢ مَّكِينٍ

Faja'alnaahu fee qaraarim makeen

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

Aya 22

إِلَىٰ قَدَرٍۢ مَّعْلُومٍۢ

Illaa qadrim ma'loom

Mpaka muda maalumu?

Aya 23

فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ ٱلْقَٰدِرُونَ

Faqadarnaa fani'mal qaadiroon

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

Aya 24

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma 'izil lilmukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 25

أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ كِفَاتًا

Alam naj'alil arda kifaataa

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

Aya 26

أَحْيَآءًۭ وَأَمْوَٰتًۭا

Ahyaaa'anw wa amwaataa

Walio hai na maiti?

Aya 27

وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَٰسِىَ شَٰمِخَٰتٍۢ وَأَسْقَيْنَٰكُم مَّآءًۭ فُرَاتًۭا

Wa ja'alnaa feehaa rawaasiya shaamikhaatinw wa asqainaakum maaa'an furaataa

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

Aya 28

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma 'izil lilmukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 29

ٱنطَلِقُوٓا۟ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Intaliqooo ilaa maa kuntum bihee tukazziboon

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

Aya 30

ٱنطَلِقُوٓا۟ إِلَىٰ ظِلٍّۢ ذِى ثَلَٰثِ شُعَبٍۢ

Intaliqooo ilaa zillin zee salaasi shu'ab

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

Aya 31

لَّا ظَلِيلٍۢ وَلَا يُغْنِى مِنَ ٱللَّهَبِ

Laa zaleelinw wa laa yughnee minal lahab

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

Aya 32

إِنَّهَا تَرْمِى بِشَرَرٍۢ كَٱلْقَصْرِ

Innahaa tarmee bishararin kalqasr

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

Aya 33

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٌۭ صُفْرٌۭ

Ka annahoo jimaalatun sufr

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

Aya 34

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma 'izil lilmukazibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 35

هَٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ

Haazaa yawmu laa uantiqoon

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

Aya 36

وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ

Wa laa yu'zanu lahum fa ya'taziroon

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

Aya 37

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailunw yawma 'izil lilmukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

Aya 38

هَٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَٰكُمْ وَٱلْأَوَّلِينَ

Haaza yawmul fasli jama 'naakum wal awwaleen

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

Aya 39

فَإِن كَانَ لَكُمْ كَيْدٌۭ فَكِيدُونِ

Fa in kaana lakum kaidun fakeedoon

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

Aya 40

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma'izil lilmukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

Aya 41

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى ظِلَٰلٍۢ وَعُيُونٍۢ

Innal muttaqeena fee zilaalinw wa 'uyoon

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

Aya 42

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ

Wa fawaakiha mimmaa yastahoon

Na matunda wanayo yapenda,

Aya 43

كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Kuloo washraboo haneee 'am bimaa kuntum ta'maloon

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

Aya 44

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ

Innaa kazaalika najzil muhsineen

Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

Aya 45

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailuny yawma 'izil lilmuzkazzibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 46

كُلُوا۟ وَتَمَتَّعُوا۟ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجْرِمُونَ

Kuloo wa tamatta'oo qaleelan innakum mujrimoon

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

Aya 47

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailunny yawma 'izil lilmukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 48

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرْكَعُوا۟ لَا يَرْكَعُونَ

Wa izaa qeela lahumur ka'oo aa yarka'oon

Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

Aya 49

وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Wailunny yawma 'izil lilmukazzibeen

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Aya 50

فَبِأَىِّ حَدِيثٍۭ بَعْدَهُۥ يُؤْمِنُونَ

Fabi ayyi hadeesim ba'dahoo yu'minoon

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?