سَبِّحِ ٱسْمَ رَبِّكَ ٱلْأَعْلَى
Sabbihisma Rabbikal A'laa
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
سَبِّحِ ٱسْمَ رَبِّكَ ٱلْأَعْلَى
Sabbihisma Rabbikal A'laa
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
ٱلَّذِى خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Allazee khalaqa fasawwaa
Aliye umba, na akaweka sawa,
وَٱلَّذِى قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Wallazee qaddara fahadaa
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
وَٱلَّذِىٓ أَخْرَجَ ٱلْمَرْعَىٰ
Wallazeee akhrajal mar'aa
Na aliye otesha malisho,
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحْوَىٰ
Faja'alahoo ghusaaa'an ahwaa
Kisha akayafanya makavu, meusi.
سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Sanuqri'uka falaa tansaaa
Tutakusomesha wala hutasahau,
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ يَعْلَمُ ٱلْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ
Illaa maa shaaa'al laah; innahoo ya'lamul jahra wa maa yakhfaa
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ
Wa nu-yassiruka lilyusraa
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكْرَىٰ
Fazakkir in nafa'atizzikraa
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ
Sa yazzakkaru maiyakhshaa
Atakumbuka mwenye kuogopa.
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلْأَشْقَى
Wa yatajannabuhal ashqaa
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
ٱلَّذِى يَصْلَى ٱلنَّارَ ٱلْكُبْرَىٰ
Allazee yaslan Naaral kubraa
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ
Summa laa yamootu feehaa wa laa yahyaa
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Qad aflaha man tazakkaa
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
وَذَكَرَ ٱسْمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
Wa zakaras ma Rabbihee fasallaa
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
بَلْ تُؤْثِرُونَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Bal tu'siroonal hayaatad dunyaa
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
وَٱلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ وَأَبْقَىٰٓ
Wal Aakhiratu khairunw wa abqaa
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
إِنَّ هَٰذَا لَفِى ٱلصُّحُفِ ٱلْأُولَىٰ
Inna haazaa lafis suhu fil oolaa
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
صُحُفِ إِبْرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Suhufi Ibraaheema wa Moosaa
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.