هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ
Hal ataaka hadeesul ghaashiyah
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ
Hal ataaka hadeesul ghaashiyah
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Wujoohuny yawma 'izin khaashi'ah
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٌۭ نَّاصِبَةٌۭ
'Aamilatun naasibah
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةًۭ
Taslaa naaran haamiyah
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍۢ
Tusqaa min 'aynin aaniyah
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍۢ
Laisa lahum ta'aamun illaa min daree'
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍۢ
Laa yusminu wa laa yughnee min joo'
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاعِمَةٌۭ
Wujoohuny yawma 'izin naa'imah
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌۭ
Lisa'yihaa raadiyah
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍۢ
Fee jannatin 'aaliyah
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةًۭ
Laa tasma'u feehaa laaghiyah
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيْنٌۭ جَارِيَةٌۭ
Feehaa 'aynun jaariyah
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٌۭ مَّرْفُوعَةٌۭ
Feehaa sururum marfoo'ah
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكْوَابٌۭ مَّوْضُوعَةٌۭ
Wa akwaabum mawdoo 'ah
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌۭ
Wa namaariqu masfoofah
Na matakia safu safu,
وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ
Wa zaraabiyyu mabsoosah
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
Afalaa yanzuroona ilalibili kaifa khuliqat
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
Wa ilas samaaa'i kaifa rufi'at
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
Wa ilal jibaali kaifa nusibat
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
Wa ilal ardi kaifa sutihat
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌۭ
Fazakkir innama anta Muzakkir
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
Lasta 'alaihim bimusaitir
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Illaa man tawallaa wa kafar
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ
Fa yu'azzibuhul laahul 'azaabal akbar
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ
Innaa ilainaaa iyaabahum
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
Summa inna 'alainaa hisaabahum
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!