Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Ghashiya
88

Al-Ghashiya — Lenye Kufunika

الغَاشِيَةِ
Za Makka Aya 26
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ

Hal ataaka hadeesul ghaashiyah

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

Aya 2

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ

Wujoohuny yawma 'izin khaashi'ah

Siku hiyo nyuso zitainama,

Aya 3

عَامِلَةٌۭ نَّاصِبَةٌۭ

'Aamilatun naasibah

Zikifanya kazi, nazo taabani.

Aya 4

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةًۭ

Taslaa naaran haamiyah

Ziingie katika Moto unao waka -

Aya 5

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍۢ

Tusqaa min 'aynin aaniyah

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

Aya 6

لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍۢ

Laisa lahum ta'aamun illaa min daree'

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

Aya 7

لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍۢ

Laa yusminu wa laa yughnee min joo'

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

Aya 8

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاعِمَةٌۭ

Wujoohuny yawma 'izin naa'imah

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

Aya 9

لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌۭ

Lisa'yihaa raadiyah

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

Aya 10

فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍۢ

Fee jannatin 'aaliyah

Katika Bustani ya juu.

Aya 11

لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةًۭ

Laa tasma'u feehaa laaghiyah

Hawatasikia humo upuuzi.

Aya 12

فِيهَا عَيْنٌۭ جَارِيَةٌۭ

Feehaa 'aynun jaariyah

Humo imo chemchem inayo miminika.

Aya 13

فِيهَا سُرُرٌۭ مَّرْفُوعَةٌۭ

Feehaa sururum marfoo'ah

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

Aya 14

وَأَكْوَابٌۭ مَّوْضُوعَةٌۭ

Wa akwaabum mawdoo 'ah

Na bilauri zilizo pangwa,

Aya 15

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌۭ

Wa namaariqu masfoofah

Na matakia safu safu,

Aya 16

وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ

Wa zaraabiyyu mabsoosah

Na mazulia yaliyo tandikwa.

Aya 17

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ

Afalaa yanzuroona ilalibili kaifa khuliqat

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

Aya 18

وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ

Wa ilas samaaa'i kaifa rufi'at

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

Aya 19

وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ

Wa ilal jibaali kaifa nusibat

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

Aya 20

وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ

Wa ilal ardi kaifa sutihat

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

Aya 21

فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌۭ

Fazakkir innama anta Muzakkir

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

Aya 22

لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ

Lasta 'alaihim bimusaitir

Wewe si mwenye kuwatawalia.

Aya 23

إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Illaa man tawallaa wa kafar

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

Aya 24

فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ

Fa yu'azzibuhul laahul 'azaabal akbar

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

Aya 25

إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ

Innaa ilainaaa iyaabahum

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

Aya 26

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم

Summa inna 'alainaa hisaabahum

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!