Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Fajr
89

Al-Fajr — Alfajiri

الفَجۡرِ
Za Makka Aya 30
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلْفَجْرِ

Wal-Fajr

Naapa kwa alfajiri,

Aya 2

وَلَيَالٍ عَشْرٍۢ

Wa layaalin 'ashr

Na kwa masiku kumi,

Aya 3

وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ

Wash shaf'i wal watr

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

Aya 4

وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ

Wallaili izaa yasr

Na kwa usiku unapo pita,

Aya 5

هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌۭ لِّذِى حِجْرٍ

Hal fee zaalika qasamul lizee hijr

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

Aya 6

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Alam tara kaifa fa'ala rabbuka bi'aad

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

Aya 7

إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ

Iramaa zaatil 'imaad

Wa Iram, wenye majumba marefu?

Aya 8

ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَٰدِ

Allatee lam yukhlaq misluhaa fil bilaad

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

Aya 9

وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ

Wa samoodal lazeena jaabus sakhra bil waad

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

Aya 10

وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ

Wa fir'awna zil awtaad

Na Firauni mwenye vigingi?

Aya 11

ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَٰدِ

Allazeena taghaw fil bilaad

Ambao walifanya jeuri katika nchi?

Aya 12

فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ

Fa aksaroo feehal fasaad

Wakakithirisha humo ufisadi?

Aya 13

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ

Fasabba 'alaihim Rabbuka sawta 'azaab

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

Aya 14

إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ

Inna Rabbaka labil mirsaad

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

Aya 15

فَأَمَّا ٱلْإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ

Fa ammal insaanu izaa mab talaahu Rabbuhoo fa akramahoo wa na' 'amahoo fa yaqoolu Rabbeee akraman

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

Aya 16

وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَٰنَنِ

Wa ammaaa izaa mabtalaahu faqadara 'alaihi rizqahoo fa yaqoolu Rabbeee ahaanan

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

Aya 17

كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ

Kalla bal laa tukrimooo nal yateem

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

Aya 18

وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ

Wa laa tahaaaddoona 'alaata'aamil miskeen

Wala hamhimizani kulisha masikini;

Aya 19

وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًۭا لَّمًّۭا

Wa taakuloonat turaasa aklal lammaa

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

Aya 20

وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّۭا جَمًّۭا

Wa tuhibboonal maala hubban jammaa

Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

Aya 21

كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّۭا دَكًّۭا

Kallaaa izaaa dukkatil ardu dakkan dakka

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

Aya 22

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّۭا صَفًّۭا

Wa jaaa'a Rabbuka wal malaku saffan saffaa

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

Aya 23

وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍۢ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ

Wa jeee'a yawma'izim bi jahannnam; Yawma 'iziny yatazakkarul insaanu wa annaa lahuz zikraa

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

Aya 24

يَقُولُ يَٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى

Yaqoolu yaa laitanee qaddamtu lihayaatee

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

Aya 25

فَيَوْمَئِذٍۢ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌۭ

Fa Yawma izil laa yu'azzibu 'azaabahooo ahad

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

Aya 26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌۭ

Wa laa yoosiqu wasaaqa hooo ahad

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

Aya 27

يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ

Yaaa ayyatuhan nafsul mutma 'innah

Ewe nafsi iliyo tua!

Aya 28

ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةًۭ مَّرْضِيَّةًۭ

Irji'eee ilaa Rabbiki raadiyatam mardiyyah

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

Aya 29

فَٱدْخُلِى فِى عِبَٰدِى

Fadkhulee fee 'ibaadee

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

Aya 30

وَٱدْخُلِى جَنَّتِى

Wadkhulee jannatee

Na ingia katika Pepo yangu.