Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Balad
90

Al-Balad — Mji

البَلَدِ
Za Makka Aya 20
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

لَآ أُقْسِمُ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ

Laaa uqsimu bihaazal balad

Naapa kwa Mji huu!

Aya 2

وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ

Wa anta hillum bihaazal balad

Nawe unaukaa Mji huu.

Aya 3

وَوَالِدٍۢ وَمَا وَلَدَ

Wa waalidinw wa maa walad

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

Aya 4

لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِى كَبَدٍ

Laqad khalaqnal insaana fee kabad

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

Aya 5

أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌۭ

Ayahsabu al-lai yaqdira 'alaihi ahad

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

Aya 6

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًۭا لُّبَدًا

Yaqoolu ahlaktu maalal lubadaa

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

Aya 7

أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

Ayahsabu al lam yarahooo ahad

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

Aya 8

أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ

Alam naj'al lahoo 'aynayn

Kwani hatukumpa macho mawili?

Aya 9

وَلِسَانًۭا وَشَفَتَيْنِ

Wa lisaananw wa shafatayn

Na ulimi, na midomo miwili?

Aya 10

وَهَدَيْنَٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ

Wa hadaynaahun najdayn

Na tukambainishia zote njia mbili?

Aya 11

فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ

Falaq tahamal-'aqabah

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

Aya 12

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ

Wa maaa adraaka mal'aqabah

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

Aya 13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Fakku raqabah

Kumkomboa mtumwa;

Aya 14

أَوْ إِطْعَٰمٌۭ فِى يَوْمٍۢ ذِى مَسْغَبَةٍۢ

Aw it'aamun fee yawmin zee masghabah

Au kumlisha siku ya njaa

Aya 15

يَتِيمًۭا ذَا مَقْرَبَةٍ

Yateeman zaa maqrabah

Yatima aliye jamaa,

Aya 16

أَوْ مِسْكِينًۭا ذَا مَتْرَبَةٍۢ

Aw miskeenan zaa matrabah

Au masikini aliye vumbini.

Aya 17

ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ

Summa kaana minal lazeena aamanoo wa tawaasaw bissabri wa tawaasaw bilmarhamah

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

Aya 18

أُو۟لَٰٓئِكَ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ

Ulaaa'ika As-haabul maimanah

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

Aya 19

وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا هُمْ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ

Wallazeena kafaroo bi aayaatinaa hum as-haabul Mash'amah

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

Aya 20

عَلَيْهِمْ نَارٌۭ مُّؤْصَدَةٌۢ

Alaihim naarum mu'sadah

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.