Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Ash-Shams
91

Ash-Shams — Jua

الشَّمۡسِ
Za Makka Aya 15
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا

Wash shamsi wa duhaa haa

Naapa kwa jua na mwangaza wake!

Aya 2

وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا

Wal qamari izaa talaa haa

Na kwa mwezi unapo lifuatia!

Aya 3

وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا

Wannahaari izaa jallaa haa

Na kwa mchana unapo lidhihirisha!

Aya 4

وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا

Wallaili izaa yaghshaa haa

Na kwa usiku unapo lifunika!

Aya 5

وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا

Wassamaaa'i wa maa banaahaa

Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!

Aya 6

وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا

Wal ardi wa maa tahaahaa

Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!

Aya 7

وَنَفْسٍۢ وَمَا سَوَّىٰهَا

Wa nafsinw wa maa sawwaahaa

Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!

Aya 8

فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا

Fa-alhamahaa fujoorahaa wa taqwaahaa

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,

Aya 9

قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا

Qad aflaha man zakkaahaa

Hakika amefanikiwa aliye itakasa,

Aya 10

وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا

Wa qad khaaba man dassaahaa

Na hakika amekhasiri aliye iviza.

Aya 11

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ

Kazzabat Samoodu bi taghwaahaaa

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,

Aya 12

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا

Izim ba'asa ashqaahaa

Alipo simama mwovu wao mkubwa,

Aya 13

فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَٰهَا

Faqaala lahum Rasoolul laahi naaqatal laahi wa suqiyaahaa

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

Aya 14

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا

Fakazzaboohu fa'aqaroohaa fadamdama 'alaihim Rabbuhum bizambihim fasaw waahaa

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

Aya 15

وَلَا يَخَافُ عُقْبَٰهَا

Wa laa yakhaafu'uqbaahaa

Wala Yeye haogopi matokeo yake.