Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Layl
92

Al-Layl — Usiku

اللَّيۡلِ
Za Makka Aya 21
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ

Wallaili izaa yaghshaa

Naapa kwa usiku unapo funika!

Aya 2

وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ

Wannahaari izaa tajalla

Na mchana unapo dhihiri!

Aya 3

وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ

Wa maa khalaqaz zakara wal unthaa

Na kwa Aliye umba dume na jike!

Aya 4

إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ

Inna sa'yakum lashattaa

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.

Aya 5

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ

Fa ammaa man a'taa wattaqaa

Ama mwenye kutoa na akamchamngu,

Aya 6

وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ

Wa saddaqa bil husnaa

Na akaliwafiki lilio jema,

Aya 7

فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ

Fasanu yassiruhoo lilyusraa

Tutamsahilishia yawe mepesi.

Aya 8

وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ

Wa ammaa mam bakhila wastaghnaa

Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,

Aya 9

وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ

Wa kazzaba bil husnaa

Na akakanusha lilio jema,

Aya 10

فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ

Fasanu yassiruhoo lil'usraa

Tutamsahilishia yawe mazito!

Aya 11

وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ

Wa maa yughnee 'anhu maaluhooo izaa taraddaa

Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?

Aya 12

إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ

Inna 'alainaa lal hudaa

Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.

Aya 13

وَإِنَّ لَنَا لَلْءَاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ

Wa inna lanaa lal Aakhirata wal oolaa

Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.

Aya 14

فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًۭا تَلَظَّىٰ

Fa anzartukum naaran talazzaa

Basi nakuonyeni na Moto unao waka!

Aya 15

لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى

Laa yaslaahaaa illal ashqaa

Hatauingia ila mwovu kabisa!

Aya 16

ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Allazee kazzaba wa tawallaa

Anaye kadhibisha na kupa mgongo.

Aya 17

وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى

Wa sa yujannnabuhal atqaa

Na mchamngu ataepushwa nao,

Aya 18

ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ

Allazee yu'tee maalahoo yatazakkaa

Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.

Aya 19

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍۢ تُجْزَىٰٓ

Wa maa li ahadin 'indahoo min ni'matin tujzaaa

Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.

Aya 20

إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ

Illab tighaaa'a wajhi rabbihil a 'laa

Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.

Aya 21

وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ

Wa lasawfa yardaa

Naye atakuja ridhika!