Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Adh-Dhuha
93

Adh-Dhuha — Mchana

الضُّحَىٰ
Za Makka Aya 11
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَٱلضُّحَىٰ

Wad duhaa

Naapa kwa mchana!

Aya 2

وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ

Wal laili iza sajaa

Na kwa usiku unapo tanda!

Aya 3

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Ma wad da'aka rabbuka wa ma qalaa

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

Aya 4

وَلَلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ

Walal-aakhiratu khairul laka minal-oola

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

Aya 5

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ

Wa la sawfa y'uteeka rabbuka fatarda

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

Aya 6

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًۭا فَـَٔاوَىٰ

Alam ya jidka yateeman fa aawaa

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

Aya 7

وَوَجَدَكَ ضَآلًّۭا فَهَدَىٰ

Wa wa jadaka daal lan fahada

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

Aya 8

وَوَجَدَكَ عَآئِلًۭا فَأَغْنَىٰ

Wa wa jadaka 'aa-ilan fa aghnaa

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

Aya 9

فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ

Fa am mal yateema fala taqhar

Basi yatima usimwonee!

Aya 10

وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ

Wa am mas saa-ila fala tanhar

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

Aya 11

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ

Wa amma bi ni'mati rabbika fahad dith

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.