وَٱلْعَٰدِيَٰتِ ضَبْحًۭا
Wal'aadi yaati dabha
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
وَٱلْعَٰدِيَٰتِ ضَبْحًۭا
Wal'aadi yaati dabha
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
فَٱلْمُورِيَٰتِ قَدْحًۭا
Fal moori yaati qadha
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
فَٱلْمُغِيرَٰتِ صُبْحًۭا
Fal mugheeraati subha
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
فَأَثَرْنَ بِهِۦ نَقْعًۭا
Fa atharna bihee naq'a
Huku wakitimua vumbi,
فَوَسَطْنَ بِهِۦ جَمْعًا
Fawa satna bihee jam'a
Na wakijitoma kati ya kundi,
إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٌۭ
Innal-insana lirabbihee lakanood
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌۭ
Wa innahu 'alaa zaalika la shaheed
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلْخَيْرِ لَشَدِيدٌ
Wa innahu lihubbil khairi la shadeed
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
۞ أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِى ٱلْقُبُورِ
Afala ya'lamu iza b'uthira ma filquboor
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِى ٱلصُّدُورِ
Wa hussila maa fis sudoor
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّخَبِيرٌۢ
Inna rabbahum bihim yauma 'izil la khabeer
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!