Noor
Kiswahili
Noor / Dua / Swala / Dua ya rukuu

Dua ya rukuu

Swala · 5 dua

Dua ya rukuu 0:00
Sikiliza
1

سُبْحانَ رَبِّيَ الْعَظِيمِ (ثلاث مرات)

Ametakasika Mola wangu aliye Mtukufu. (Utasema mara tatu)

Chanzo: Abu Dawud, Ibn Majah, An-Nasa'i, At-Tirmizi, Ahmad, Sahih At-Tirmizi (Al-Albani) 1/83.

2

سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ, اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي

Kutakasika ni kwako, Ewe Mwenyezi Mungu Mola wetu, na sifa njema zote ni zako, Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe.

Chanzo: Al-Bukhari 1/99, Muslim 1/350.

3

سُبُّوُحٌ, قُدُّوسٌ, رَبُّ المَلاَئِكَةِ وَالرُّوحِ

Mwingi wa kutakaswa, Mtakatifu, Mola wa Malaika na Jibriil.

Chanzo: Muslim 1/353, Abu Dawud 1/230.

4

اللَّهُمَّ لَكَ رَكَعْتُ, وَبِكَ آمَنْتُ, وَلَكَ أَسْلَمْتُ, خَشَعَ لَكَ سَمْعِي, وَبَصَرِي, وَمُخِّي, وَعَظْمِي, وَعَصَبِي, [وَمَا استَقَلَّتْ بِهِ قَدَمِي]

Ewe Mwenyezi Mungu kwako nimerukuu, na Wewe nimekuamini, na kwako nimejisalimisha, umenyenyekea kwako usikizi wangu, na uoni wangu, na ubongo wangu, na mfupa wangu, na hisia zangu, na ambacho kimesimama juu ya miguu yangu.

Chanzo: Muslim 1/534, Abu Dawud, An-Nasa'i, At-Tirmithi.

5

سُبْحَانَ ذِي الْجَبَرُوتِ, وَالْمَلَكُوتِ, وَالْكِبْرِيَاءِ, وَالْعَظَمَةِ

Ametakasika Mwenye Utawala na Ufalme, na Ukubwa, na Utukufu.

Chanzo: Abu Dawud 1/230, An-Nasa'i, Ahmad.