1
إِذَا أَكَلَ أَحَدُكُمْ طَعَاماً فَلْيَقُلْ بِسْمِ اللَّهِ, فَإِنْ نَسِيَ فِي أَوَّلِهِ فَلْيَقُلْ بسمِ اللَّهِ فِي أَوَّلِهِ وَآخِرِهِ
Atakapokula mmoja wenu chkula basi aseme: ''Bismi LLaah'' ''Kwa jina la Mwenyezi Mungu.'' Na akisahau mwanzo wake, basi aseme: ''Bismi LLaahi fii awwalihi wa a'khirihi'' ''Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzo wake na mwisho wake.''
Chanzo: Abu Dawud 3/347, At-Tirmizi 4/288.
2
مَنْ أَطْعَمَهُ اللَّهُ الطَّعَامَ فَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِيهِ وَأَطْعِمْنَا خَيْراً مِنْهُ, وَمَنْ سَقَاهُ اللَّهُ لَبَناً فَلْيَقُلْ اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِيهِ وَزِدْنَا مِنْهُ
Yeyote ambaye Mwenyezi Mungu amemruzuku chakula aseme: ''Ewe Mwenyezi Mungu tubariki katika chakula hiki na tulishe bora kuliko hiki.'' Na yeyote ambae ameruzukiwa maziwa basi aseme: ''Ewe Mwenyezi Mungu tubarikie kinywaji hiki na utuzidishie.''
Chanzo: At-Tirmizi 5/506.