Noor
Kiswahili
Noor / Qurani / Al-Humaza
104

Al-Humaza — Msengenyaji

الهُمَزَةِ
Za Makka Aya 9
Sikiliza sura 0:00
Sikiliza · Mishary Rashid Alafasy

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

Aya 1

وَيْلٌۭ لِّكُلِّ هُمَزَةٍۢ لُّمَزَةٍ

Wai lul-li kulli hu mazatil-lumaza

Ole wake kila safihi, msengenyaji!

Aya 2

ٱلَّذِى جَمَعَ مَالًۭا وَعَدَّدَهُۥ

Al-lazi jama'a maalaw wa'addadah

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

Aya 3

يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخْلَدَهُۥ

Yahsabu anna maalahu akhladah

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

Aya 4

كَلَّا ۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِى ٱلْحُطَمَةِ

Kalla layum ba zanna fil hutamah

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

Aya 5

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحُطَمَةُ

Wa maa adraaka mal-hutamah

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

Aya 6

نَارُ ٱللَّهِ ٱلْمُوقَدَةُ

Narul laahil-mooqada

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

Aya 7

ٱلَّتِى تَطَّلِعُ عَلَى ٱلْأَفْـِٔدَةِ

Al latee tat tali'u 'alalafidah

Ambao unapanda nyoyoni.

Aya 8

إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌۭ

Innaha 'alaihim moosada

Hakika huo utafungiwa nao

Aya 9

فِى عَمَدٍۢ مُّمَدَّدَةٍۭ

Fee 'amadim-mu mad dadah

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.